Uchaguzi 2020 TUME: Pamoja na kwamba kupiga kura hiari, Serikali imeingia gharama kubwa sana. Tunawasihi Watanzania wakapige kura

Hakuna ambacho haiwezekani bali wanakataa ili kuiba kura kwa urahisi na bila complications...
 
Issue sio tehama peke yake hapa.

Walipotangaza watu wajiandikishe na kuhakiki taarifa mapema walitaka wajue pia idadi ya wapiga kura kwa kila kituo ili waweze kupanga rasilimali zitakazotoshana nao ikiwa ni pamoja na vifaa, wasimamizi, muda na hata majengo pia.

Leo wakiruhusu kila mtu apige kura sehemu yoyote kuna vituo vitakua na wapiga kura wachache au kukosa kabisa huku vingine vikizidiwa na idadi kubwa ya wapiga kura

Kikubwa tarehe inajulikana na siku ya kupiga kura hakuna kazi twendeni tulikojiandikishia tukatimize wajibu
 
Wale ambao madiwani na wabunge wao tayari wameteuliwa na tume watawapigia nani?
 
Sasa kwa nini mnampotezea muda "mbeligiji"!!! Mkuu kura yako muhimu sana, tafadhali tukapige kura 28/10/2020, Tumchague rais asiye na vinasaba vya mabeberu!
 
Hima Watanzania baada ya Tume kutimiza waji wao sasa ni Haki yetu sisi kuitumia fursa hiyo kujitokeza kwa wingi kwaajili ya upigaji kura. Tukapige kura kuwachagua wale ambao tunadhani watasimamia Ilani na kutekel;eza yale waliyotuahidi kwa manufaa ya taifa letu na vizazi vyetu vijavyo.
 
Ni kweli kabisa gharama za uchaguzi ni kubwa Sana kwa hiyo tukifanya mzaha uchaguzi ukaharibika ni upotezaji wa pesa za watanzania
 
Ni kweli kabisa gharama za uchaguzi ni kubwa Sana kwa hiyo tukifanya mzaha uchaguzi ukaharibika ni upotezaji wa pesa za watanzania
Pia ambao wanadhamana ya usimamizi was mchakato huu wahakikishe wanatenda haki vinginevyo.Yote yaliyofanyika yatapoteza maana mbali na kuwa gharama kubwa imetumika.
 
Asitufokee
 
Mwambie mahera, uchaguzi huu hautamuacha salama akileta useng.e
 
Mkuu inaruhusiwa ku-share hiyo link?
 
Sawa tumekusoma. Pamoja na kutumia hizo gharama kubwa. Ninyi mhakikishe vitendea kazi vya kupigia kura vinafika maeneo yote husika mapema. Sio kituo kinafunguliwa box zinafika saa nane mchana na pili kuhakikisha kuna umeme au generator kiuweza kuhakiki uhesabuji wakura. Polisi hawahusiki maswala ya kupiga kura zaidi ya usalama wa watu nje ya kituo wasipigane.
Tanesco waache kukata umeme na wasimamizi wawe smart na kuharakisha zoezi la upigaji kura. Sio mpiga kura anafika anaambiwa jina halipo! Upangwe utaratibu wa hatua kwa hatua na haki itendeke..
 
Ujinga mkubwa wa NEC mnachezea uchaguzi, mnawachagulia watu kwa kuwaengua wagombea halafu mnasema watu wajitokeze kwa wingi kupiga kura?! Inaudhi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…