Pre GE2025 Tume Uchaguzi: Wapigakura 594,494 wanatarajiwa wakuondolewa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura kwa kukosa sifa

Pre GE2025 Tume Uchaguzi: Wapigakura 594,494 wanatarajiwa wakuondolewa kwenye daftari la kudumu la mpiga kura kwa kukosa sifa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imesema kwa kuzingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022, inatarajia kuandikisha wapigakura wapya 5,586,433 sawa na asilimia 18.7 ya wapigakura 29,754,699 waliopo kwenye daftari baada ya uboreshaji uliofanyika mwaka 2019 mpaka 2020.

Mkurugenzi wa Uchaguzi Ramadhani Kailima amesema hayo kwenye mkutano wa tume hiyo na wadau wa uchaguzi uliofanyika mkoani Tanga leo Jumamosi Januari Mosi, 2025 na kusema kuwa wapigakura 4,369,531 inatarajiwa wataboresha taarifa zao katika zoezi hilo.

Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

"Amesema kuwa wapigakura 594,494 wanatarajiwa wakuondolewa kwenye daftari kwa kukosa sifa za kuendelea kuwepo kwenye daftari hivyo baada ya uboreshaji, inatarajiwa kuwa daftari litakuwa na jumla ya wapiga 34,746,638,"amesema Kailima.

 
Back
Top Bottom