Tume ya Katiba mbinu kuteka mjadala-Lissu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
219,468
Reaction score
911,184
Tume ya Katiba mbinu kuteka mjadala-Lissu


Na Reuben Kagaruki

MBUNGE wa Singida Magharibi, Bw. Tindu Lissu, amesema Tume ya Maalumu ya Katiba itakayoundwa na Rais Jakaya Kikwete, ni mbinu ya miaka yote ya
kuteka mijadala hatari kwa CCM na serikali na kuielekeza palipo salama.

Katika maoni yake kwenye mtandao wa Wanabidii jana na baadaye kulithibitishia gazeti hili kuwa hayo ni maoni yake binafsi na si msimamo wa chama, Bw. Lissu amesema mara mjadala unapoanzia nje ya chama au dola ni hatari kwa watawala, hasa pale ukiachwa ujiendee wenyewe bila kuingiliwa.

"Hapa ndipo watawala wanaingia kwa 'gear' ya Tume ya Katiba. Tume hiyo inajengewa hoja yenye maneno matamu na rais, inakolezwa utamu kwa kuwekwa mtu mmoja au wawili (kwa mfano 'mwanasheria aliyebobea)," alisema Bw. Lissu na kuongeza;

"Kwa hiyo, maneno kama 'Tume yenye uwakilishi wa makundi mbalimbali ya kiraia' ni chumvi tu inayopakwa kwenye mhogo mchungu ili ulike kirahisi."

Alisema wananchi wanaambiwa tuwe na subira hadi Tume ya Rais itakapomaliza kazi yake.

"Tunaaswa tuwe wavumilivu ili tule mbivu na katu tusiwe na jazba, munkari au kelele wakati mjadala unauawa pole pole kwa kupitia tume," alisema Bw. Lissu.

Alisema watu wachache wanaoendelea kupiga kelele kuwa mjadala umetekwa nyara, wanashambuliwa kuwa wanaonea wivu wale walioteuliwa kwenye Tume ya Rais, au wanaitwa walalamikaji tu wasiokuwa na lolote la kujenga au ni wakosoaji wa kila kitu kinachofanywa na mtukufu Rais hata kama kina maslahi kwa nchi.

Bw. Lissu alitoa mfano wa tume nyingi ambazo ziliwahi kuundwa, lakini ripoti zake hazijawahi kutekelezwa.
 

Tume ya JK ya kukusanya maoni hiyo ni yake sisi tunasubiri Bunge lipitishe sheria ya kuanzisha mchakato huu rasmi na upewe meno ya kisheria............mchakato huu uwe na mkutano wakikatiba wenye wajumbe ambao wapigakura tutawachagua rasmi kutuwakilisha kwa ajili ya suala hili tu..................
 
Mie namshangaa huyu Lissu, hoja ya Katiba mpya nchi hii hakuianzisha yeye, watu wamefikia hata kutoa rasimu ya Katibu miaka 10 nyuma, jee na yeye alikuwa akiiteka hiyo kujitakia umaarufu kupitia katiba na kujaribu kuifanya ni hoja yake binafsi?

WaTanzania wachache wamesema inatakiwa katiba mpya miaka mingi iliopita, wengine ndio kwanza wameliona hilo na kuingia kwa gea ya kasi, wengine wanasema irekebishwe na wengine wamefikia kusema CCM ndio kikwazo cha katiba mpya Kikwete kayona hayo na kawasikiliza wote na kaamuwa iundwe tume ili imridhishe kila mwenye kiu kuhusu katiba, nalo hilo pia ni kosa? Ama kweli, watu wanashangaza sana.

Karata za siasa zipo nyingi sana, na ilikuwa ni vizuri huyu Lissu akaanza kwa ng'anda badala ya turufu, kwani turufu ikishachezwa ndio imekwenda hiyo, hairudi. Angoje karata zipigwe tena.

Ndio kwanza kafika jamvini, hata hajakaa sawa kupigiana na wenzake yeye anatupa jike? Kikarata unaolewa mapema. Pole Lissu, ngoja karata zipigwe upya. Na safari hii uwe makini kwa kuanza na ng'anda.
 

Nadhani hujasoma alichokiandika Tundu Lisu, halafu kwa nini siku zote unakuwa mswahili swahili kwamba kila anaetoa hoja fulani against CCM/ JK basi ni wivu, kutafuta umaarufu au njaa???????. That is a trend ambayo umekuwa ukiionyesha kila siku. Man up bro!! Hizo rhetoric za kina Makamba, JK hazitatufikisha popote! If u are against hoja ya mwenzio basi toa yako na siku zote lete solution sio kutoa toa povu tu kila wakati kama mabishano ya kwenye kahawa.

 
Mh. Dar Es Salaam, Sijapenda gea uliyoingia nayo. Huko ni kujisifu kusiko na sababu ya msingi. Kama wewe ulitangulia mbona mambo hayakwenda. Sasa ina maana unataka uwazibe mdomo watu wenye mawazo yao? Hata kama una hoja hapa sio mahali pa kujisifia kwa vile tunajua umri wa mtu au kuwepo kwa mtu kwenye jambo fulani sio kigezo cha umaarufu wala busara. Wape watu nafasi ya kutoa maoni yao wala huna haki ya kuwasemea wengine na kuwakebehi kwa umri wao au upya wao kwenye jambo fulani.
 
Mnyika go ahead na ile hoja Binafsi.
 
Mnyika go ahead na ile hoja Binafsi.

Ofcourse kuna kila haja na after all si tunaambiwa kwamba bunge ni muhimili mwingime wa dola? Kwa hiyo Mnyika kuendelea na hiyo hoja binafsi ni okay kabisaaaa!!!!!
 
Jamani sina hakika km katiba ya sasa wengi wetu mmebahatika kuiona,achilia mbali kuipitia kabisa...nadhani tuipitie kwanza kisha tutoe comments za kitu tunachokifaham...kuna swala la haki za binadamu na uhuru binafsi wa mtu..ambapo ni kipengele tu ktk ibara mojawapo ya katiba..kuna maswali najiuliza hapa:-
1.Je katiba hii tunayotaka ishughulikie vipi ndoa za jinsia moja?
2.Je ifike mahali mtoto ampandishe mzazi kizimbani kwa kukatazwa kufanya jambo lisilo adilifu(ambalo ni uhuru wake binafsi)?
3.Katiba ya sasa inataja eneo la Tanzania kua pamoja na visiwa vya Zanzibar,choko choko nyingi za kutaka kuwepo katiba tatu tumezisikia muda mrefu,je hii iwe kisu cha mwisho kutugawa mafungu mafungu?
4.Ukomo wa madaraka ya Rais!......

Haya na mengine mengi tu ni muhimu tukayaangalia kwanza....ndiyo maana nashauri tusome Katiba ya sasa iliyotungwa 1977 hadi April 30 2000 na marekebisho ya vifungu vyake yaliyofanyika tokea hapo hadi sasa...
 


trush
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…