Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi imefanya kikao na wadau wa kodi mkoani Iringa, ikilenga kupokea maoni na mapendekezo kuhusu changamoto za kodi na tozo mbalimbali zinazokwamisha maendeleo ya biashara.
Mjumbe wa Tume na Mwenyekiti wa kundi dogo la Tume, Balozi Mwanaidi Maajar, amesema kuwa lengo la mikutano hiyo ni kuhakikisha mfumo wa kodi unakuwa rahisi, wa haki, na wenye kuchochea maendeleo.
“Tunataka mfumo wa kodi uwe rafiki kwa walipakodi, uimarike kwa uwazi na usaidie kukuza biashara badala ya kuzuia maendeleo. Ushirikiano wenu wadau ni muhimu kufanikisha haya,” amesema Balozi Maajar.
Mjumbe wa Tume na Mwenyekiti wa kundi dogo la Tume, Balozi Mwanaidi Maajar, amesema kuwa lengo la mikutano hiyo ni kuhakikisha mfumo wa kodi unakuwa rahisi, wa haki, na wenye kuchochea maendeleo.
“Tunataka mfumo wa kodi uwe rafiki kwa walipakodi, uimarike kwa uwazi na usaidie kukuza biashara badala ya kuzuia maendeleo. Ushirikiano wenu wadau ni muhimu kufanikisha haya,” amesema Balozi Maajar.