Pre GE2025 Tume ya taifa ya Uchaguzi yatoa onyo kwa wananchi watakaojiandikisha zaidi ya mara moja!

Pre GE2025 Tume ya taifa ya Uchaguzi yatoa onyo kwa wananchi watakaojiandikisha zaidi ya mara moja!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Mwenyekiti Tume huru ya Taifa ya uchaguzi, Jaji Mbarouk S. Mbarouk amesisitiza kuwa ni kosa kisheria mtu mmoja kujiandikisha jina lake la kupiga kura zaidi ya mara moja kwani kufanya hivyo ni kinyume na sheria.


Mbarouk ameyasema hayo leo 15 Desemba 2024 katika uzinduzi wa mkutano wa tume na Wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura uliofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

Mbarouk ameongeza kuwa zoezi la kujiandikisha kama mpiga kura linapaswa kufanyika kwa uangalifu na kwa kuzingatia sheria zilizopo.

"Ni kosa kubwa kisheria kwa mtu kujiandikisha mara mbili au zaidi na endapo ikitokea hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watakaoshirikiana katika vitendo hivyo na Ikumbukwe kuwa uchaguzi ni mchakato wa haki na tutahakikisha kuwa hakuna mtu atakayekosa haki ya kupiga kura wala mtu yeyote atakayejihusisha na udanganyifu", amesema Mbarouk

 
Mwenyekiti Tume huru ya Taifa ya uchaguzi, Jaji Mbarouk S. Mbarouk amesisitiza kuwa ni kosa kisheria mtu mmoja kujiandikisha jina lake la kupiga kura zaidi ya mara moja kwani kufanya hivyo ni kinyume na sheria.


Mbarouk ameyasema hayo leo 15 Desemba 2024 katika uzinduzi wa mkutano wa tume na Wadau wa uchaguzi kuhusu uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura uliofanyika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.

Mbarouk ameongeza kuwa zoezi la kujiandikisha kama mpiga kura linapaswa kufanyika kwa uangalifu na kwa kuzingatia sheria zilizopo.

"Ni kosa kubwa kisheria kwa mtu kujiandikisha mara mbili au zaidi na endapo ikitokea hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watakaoshirikiana katika vitendo hivyo na Ikumbukwe kuwa uchaguzi ni mchakato wa haki na tutahakikisha kuwa hakuna mtu atakayekosa haki ya kupiga kura wala mtu yeyote atakayejihusisha na udanganyifu", amesema Mbarouk

View attachment 3177678
Blood bastard, CCM ndio wanafanya hivyo, huyu ana ubavu wa kuwawajiisha.
 
Back
Top Bottom