Uchaguzi 2020 Tume ya uchaguzi na TAKUKURU zuieni kampeni hizi zisizo rasmi wakati huu

Uchaguzi 2020 Tume ya uchaguzi na TAKUKURU zuieni kampeni hizi zisizo rasmi wakati huu

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Hivi sasa kumezuka kampeni zisizo rasmi zinazofanywa na viongozi wa serikali na wa mashirika ya umma, kampeni hizi zimelenga eti kutatua matatizo ya wananchi ikiwa ni kutoa misaada na mikopo! Huu ni wakati wa kampeni za uchaguzi hivyo kampeni hizi zinaingiliana na kampeni rasmi.

Chaguzi zilizopita hazikuwahi kuingiliwa kwa kiasi hiki ambapo mgombea wa upinzani akitoa ahadi basi kesho atajitokeza viongozi wa serikali na kuanza kutatua tatizo hilo! Huu si mtindo mzuri kwenye wakati wa uchaguzi kwani baadhi yake ni rushwa za waziri kama kilichofanyika huko Mbeya kwa kutoa mikopo ya bajaji wakati huu.

Tume ya uchaguzi na TAKUKURU simamieni uchaguzi kufuatana na sheria na kanuni zake.
 
Duuuu

Kwa hiyo mwaka wa uchaguzi haitakiwi serikali wala mashirika ya umma kutoa huduma yoyote kwa wananchi!!

Je wanavyotoa misaada/mikopo hiyo wanamshawishi anaepewa msaada/mkopo kukichagua chama fulani cha siasa?
Shughuri hizi hufanywa ndani ya ofisi kati ya muombaji na mtoaji, si viwanjani kwenye mikutano.
 
Mkuu pamoja na uchaguzi lakini ni lazima shughili zote ziendelee kama ilivyokuwa kwa miaka mingine

Anazungumzia mwaka huu wa uchaguzi. Jikite kwenye mada! Kwani hao wanaofanya hii mikusanyiko mwaka huu, 2017 walikuwa wapi??
 
Kiukweli mwaka huu kuna shida sana! Tena jambo la ajabu nihaohao walisema kampeni za mwaka huu ni nyepesi lakini hali ipo tofauti kabisa, Lissu mmoja anapambana na makundi ya misafara ya kampeni karibu makundi matano yote ya chama kimoja tu, Huku Mgombea urais, kule makamu wa rais, huku waziri mkuu Majaliwa, kule waziri mkuu Pinda, hapa Rais mstaafu Kikwete! Na bado mawaziri wengine tena wakiwa sare za CCM wanapita kutaja mara serikali imetenga milioni 200 kiwanda cha kuchakata asali, huku waziri nishati akizungumzia umee tena wametawanyika nchi nzima wakati ratiba ya Tume imeonyesha mikutano ya mgombea urais na mgombea mwenza tu! Alafu wanajitapa eti wanafanya kampeni kisayansi, sayansi gani hiyo ya kutumia nguvu na jasho jingi kiasi hicho???!
Kwanza kitendo cha kutawanya misafara ya viongozi wote wa kitaifa nchi nzima mbali ya kuleta kero, pia inakwamisha shughuli za kiuchumi za wananchi wetu masikini ambao wengi maisha yao hutegemea shuguli zao za kila siku! Anapopita kiongozi kama rais au makamu wa rais au waziri mkuu, lazima njia na barabara mbalimbali zinazotumiwa na wananchi zinafungwa kwa muda kwa sababu za kiusalama na hivyo kusimamisha shughuli za wananchi, wengine, sasa inajitokeza hali kama hii kutamalaki karibu nchi nzima huku wakibadilishana mikoa , Je wananchi wazalishe saa ngapi???, Bora hata wangekuwa wanatumia usafiri wa anga1 Hii ni kero kubwa! Nashangaa tume ipo kimya!
 
Maji yako shingoni.wanaangaika kukinusuru chama kinachokaribia kukata roho.
Kiukweli mwaka huu kuna shida sana! Tena jambo la ajabu nihaohao walisema kampeni za mwaka huu ni nyepesi lakini hali ipo tofauti kabisa, Lissu mmoja anapambana na makundi ya misafara ya kampeni karibu makundi matano yote ya chama kimoja tu, Huku Mgombea urais, kule makamu wa rais, huku waziri mkuu Majaliwa, kule waziri mkuu Pinda, hapa Rais mstaafu Kikwete! Na bado mawaziri wengine tena wakiwa sare za CCM wanapita kutaja mara serikali imetenga milioni 200 kiwanda cha kuchakata asali, huku waziri nishati akizungumzia umee tena wametawanyika nchi nzima wakati ratiba ya Tume imeonyesha mikutano ya mgombea urais na mgombea mwenza tu! Alafu wanajitapa eti wanafanya kampeni kisayansi, sayansi gani hiyo ya kutumia nguvu na jasho jingi kiasi hicho???!
Kwanza kitendo cha kutawanya misafara ya viongozi wote wa kitaifa nchi nzima mbali ya kuleta kero, pia inakwamisha shughuli za kiuchumi za wananchi wetu masikini ambao wengi maisha yao hutegemea shuguli zao za kila siku! Anapopita kiongozi kama rais au makamu wa rais au waziri mkuu, lazima njia na barabara mbalimbali zinazotumiwa na wananchi zinafungwa kwa muda kwa sababu za kiusalama na hivyo kusimamisha shughuli za wananchi, wengine, sasa inajitokeza hali kama hii kutamalaki karibu nchi nzima huku wakibadilishana mikoa , Je wananchi wazalishe saa ngapi???, Bora hata wangekuwa wanatumia usafiri wa anga1 Hii ni kero kubwa! Nashangaa tume ipo kimya!
 
Kiukweli mwaka huu kuna shida sana! Tena jambo la ajabu nihaohao walisema kampeni za mwaka huu ni nyepesi lakini hali ipo tofauti kabisa, Lissu mmoja anapambana na makundi ya misafara ya kampeni karibu makundi matano yote ya chama kimoja tu, Huku Mgombea urais, kule makamu wa rais, huku waziri mkuu Majaliwa, kule waziri mkuu Pinda, hapa Rais mstaafu Kikwete! Na bado mawaziri wengine tena wakiwa sare za CCM wanapita kutaja mara serikali imetenga milioni 200 kiwanda cha kuchakata asali, huku waziri nishati akizungumzia umee tena wametawanyika nchi nzima wakati ratiba ya Tume imeonyesha mikutano ya mgombea urais na mgombea mwenza tu! Alafu wanajitapa eti wanafanya kampeni kisayansi, sayansi gani hiyo ya kutumia nguvu na jasho jingi kiasi hicho???!
Kwanza kitendo cha kutawanya misafara ya viongozi wote wa kitaifa nchi nzima mbali ya kuleta kero, pia inakwamisha shughuli za kiuchumi za wananchi wetu masikini ambao wengi maisha yao hutegemea shuguli zao za kila siku! Anapopita kiongozi kama rais au makamu wa rais au waziri mkuu, lazima njia na barabara mbalimbali zinazotumiwa na wananchi zinafungwa kwa muda kwa sababu za kiusalama na hivyo kusimamisha shughuli za wananchi, wengine, sasa inajitokeza hali kama hii kutamalaki karibu nchi nzima huku wakibadilishana mikoa , Je wananchi wazalishe saa ngapi???, Bora hata wangekuwa wanatumia usafiri wa anga1 Hii ni kero kubwa! Nashangaa tume ipo kimya!
Mkuu tume hii ya CCM? Mbona mnawaonea bure tu, unadhani wao watafanya nini kama sisi wananchi tuko kimya, kumbuka kateuliwa na huyo anayefanya hayo yote sasa unataka mbwa ambwekee boss wake
 
Mkuu tume hii ya CCM? Mbona mnawaonea bure tu, unadhani wao watafanya nini kama sisi wananchi tuko kimya, kumbuka kateuliwa na huyo anayefanya hayo yote sasa unataka mbwa ambwekee boss wake
Umejitahidi kumjibu. Pata pepsi baridi hapo ulipo...
 
Hivi sasa kumezuka kampeni zisizo rasmi zinazofanywa na viongozi wa serikali na wa mashirika ya umma, kampeni hizi zimelenga eti kutatua matatizo ya wananchi ikiwa ni kutoa misaada na mikopo! Huu ni wakati wa kampeni za uchaguzi hivyo kampeni hizi zinaingiliana na kampeni rasmi.

Chaguzi zilizopita hazikuwahi kuingiliwa kwa kiasi hiki ambapo mgombea wa upinzani akitoa ahadi basi kesho atajitokeza viongozi wa serikali na kuanza kutatua tatizo hilo! Huu si mtindo mzuri kwenye wakati wa uchaguzi kwani baadhi yake ni rushwa za waziri kama kilichofanyika huko Mbeya kwa kutoa mikopo ya bajaji wakati huu.

Tume ya uchaguzi na TAKUKURU simamieni uchaguzi kufuatana na sheria na kanuni zake.

Mkuu
Just record hayo matukio!
Nakumbuka kuna jimbo lilishatenguliwa huko Igunga-Igunga kisa daraja lilojengwa kipindi cha kampeni.
 
Mbona huwa naona magari yakipita mtaan wanatangaza habari za mikopo, kumbe huwa wanafanya makosa!!
Wamezuia magari hayo chini ya sheria za mazingira zinazozuia mitetemo japo tunaona upande mmoja ukitayatumia.
 
Back
Top Bottom