Tume ya Uchaguzi ya Namibia (ECN) yaeleza wasiwasi kuhusu idadi ndogo ya watu wanaojiandikisha kupiga kura Novemba 27, 2024

Tume ya Uchaguzi ya Namibia (ECN) yaeleza wasiwasi kuhusu idadi ndogo ya watu wanaojiandikisha kupiga kura Novemba 27, 2024

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Namibia.jpeg

Tume ya Uchaguzi ya Namibia (ECN) imeeleza wasiwasi wake kuhusu idadi ndogo ya watu wanaojiandikisha kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi ujao ikiwa zimebaki wiki mbili tu.

Hayo yamesemwa na afisa mkuu wa uchaguzi wa ECN Peter Shaama katika mkutano na waandishi wa habari.

Bwana Shaama amesema: “Ingawa tunakubali kuwa kumekuwa na ongezeko kidogo la idadi ya waliojitokeza kati ya wiki ya tarehe 1 hadi 6 Julai ikilinganishwa na wiki ya tarehe 24 hadi 29 Juni, tume bado inaona kwa wasiwasi idadi ndogo ya waliojitokeza nchi nzima hadi sasa,”

“Tume inawahimiza raia wote wa Namibia wanaostahili kupiga kura ambao bado hawajajisajili kufanya hivyo ndani ya wiki zilizobaki,” alisema.

Shaama alisema hakuna nafasi ya kuongeza muda wa kujiandikisha kupiga kura.

Usajili utaendelea nchi nzima na katika ofisi zote za kidiplomasia za Namibia nje ya nchi hadi tarehe 1 Agosti, Jumatatu hadi Jumamosi kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 1:00 usiku.

The Namibian
 
Upigaji kura katika Nchi za Kiafrika umekuwa ni kama kiini macho,waafrika tungelitambua hilo ni bora hizo fedha za kuchezea akili za watu zikapelekwa kwenye huduma za jamii moja kwa moja.
Vugu vugu zijazo zitakuwa ni za kukataa mambo ya chaguzi ili fedha zitumike kuinua maisha ya watu maskini.
 
Back
Top Bottom