Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 378
- 766
Kwa masikitiko makubwa ni fedhea kwa kampuni inayojishughulisha na uuzaji wa Virutubisho (Supplements) na bidhaa za usafi kama NeoLife kushindwa kuhifadhi Tarifa binafsi za wateja wake kama inavyotakiwa .
Asubuhi nimenunua vitumbua maeneo ya Mwenge kituoni na kifungashio kilichotumika kilikuwa ni fomu ya kampuni ya NeoLife ikiwa na tarifa binafsi za mmoja wa wateja wao.
Licha ya fomu hiyo kuandikwa herufi kubwa "Private and Confidential" lakini bado fomu hiyo ilikuwa inazagaa mitaani kama vifungashio vya vitumbua.
Fomu hiyoo ilikuwa na majina kamili ya mteja, tarehe yake ya kuzaliwa, aina ya dawa alizonunua, kiasi na lilipia shilingi ngapi pamoja na namba za simu.
Sasa najiuliza tarifa binafsi kama hizi zidondokea mikono mwa mikono ya wahuni si wanaweza kutumia hizi taarifa za huyu mtu vibaya jamani.
Taarifa hizi zinaweza kutumika kufanya uwizi na shughuli nyingine za kihalifu na hata mtu wingine anaweza kuiba utambulisho wa huyu mteja na kufanya uhalifu.
Basi mmengeficha au kufuta baadhi ya taarifa zake. Mnapaswa kuchukua hatua sahihi za kuteketeza taaarifa za wateja wenu badala ya kuuza haya makaratasi kama vifungashio.
Soma Pia: Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) itusaidie kushughulikia wanaosambaza taarifa zetu kiholela. Vyeti vyetu vinafungiwa kachori
Kwa mwenendo huu Kamati ya Tarifa Binafsi ni wakati wa kuchukua hatua taasisi zinzovujisha taarifa binafsi zinazovujisha taarifa binafsi za watu na pia kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu suala hili
Asubuhi nimenunua vitumbua maeneo ya Mwenge kituoni na kifungashio kilichotumika kilikuwa ni fomu ya kampuni ya NeoLife ikiwa na tarifa binafsi za mmoja wa wateja wao.
Licha ya fomu hiyo kuandikwa herufi kubwa "Private and Confidential" lakini bado fomu hiyo ilikuwa inazagaa mitaani kama vifungashio vya vitumbua.
Fomu hiyoo ilikuwa na majina kamili ya mteja, tarehe yake ya kuzaliwa, aina ya dawa alizonunua, kiasi na lilipia shilingi ngapi pamoja na namba za simu.
Sasa najiuliza tarifa binafsi kama hizi zidondokea mikono mwa mikono ya wahuni si wanaweza kutumia hizi taarifa za huyu mtu vibaya jamani.
Taarifa hizi zinaweza kutumika kufanya uwizi na shughuli nyingine za kihalifu na hata mtu wingine anaweza kuiba utambulisho wa huyu mteja na kufanya uhalifu.
Basi mmengeficha au kufuta baadhi ya taarifa zake. Mnapaswa kuchukua hatua sahihi za kuteketeza taaarifa za wateja wenu badala ya kuuza haya makaratasi kama vifungashio.
Soma Pia: Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) itusaidie kushughulikia wanaosambaza taarifa zetu kiholela. Vyeti vyetu vinafungiwa kachori
Kwa mwenendo huu Kamati ya Tarifa Binafsi ni wakati wa kuchukua hatua taasisi zinzovujisha taarifa binafsi zinazovujisha taarifa binafsi za watu na pia kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu suala hili