The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 747
- 2,112
Hapa chini ni nyaraka zenye taarifa binafsi za mtu ambaye anaonekana aliomba nafasi ya kazi mahali fulani, lakini baada ya nyaraka zake kuisha kuisha umuhimu wakazitelekeza kiholela. Sijui waliuza hizo karatasi au walitupa watu wakaokota, haieleweki. Ila sasa zinapatikana kwa akina mama wauza vitumbua.
Jambo hili sijui lizungumzwe mara ngapi! Taasisi nyingi bado zinafeli sana katika suala la kuhifadhi au kuteketeza nyaraka ambazo zina taarifa binafsi za watu kwa njia inayofaa. Badala yake, wanazitupa nyaraka hizo kiholela au bila ya kuchukua tahadhari, hali inayoweza kusababisha taarifa hizo kuangukia mikononi mwa watu wasiostahili.
Hii inaweza kuwa na madhara makubwa sana, sana kwa faragha na usalama wa watu, kwani taarifa binafsi kama vile majina, namba za simu, anuani, matokeo ya shule, taarifa za vitambulisho vya taifa, au taarifa za kifedha n.k zinaweza kutumiwa vibaya na wahalifu au watu wenye nia mbaya.
Soma Pia:
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) mmelifungia hili vioo? Ingawa taarifa nyingi zinahamia mtandaoni, lakini bado kuna haja ya kushughulikia vema hawa wanaotusambazia taarifa zetu mtaani kiholela. Onesheni mfano kwa taasisi kadhaa wengine wajifunze.
Jambo hili sijui lizungumzwe mara ngapi! Taasisi nyingi bado zinafeli sana katika suala la kuhifadhi au kuteketeza nyaraka ambazo zina taarifa binafsi za watu kwa njia inayofaa. Badala yake, wanazitupa nyaraka hizo kiholela au bila ya kuchukua tahadhari, hali inayoweza kusababisha taarifa hizo kuangukia mikononi mwa watu wasiostahili.
Hii inaweza kuwa na madhara makubwa sana, sana kwa faragha na usalama wa watu, kwani taarifa binafsi kama vile majina, namba za simu, anuani, matokeo ya shule, taarifa za vitambulisho vya taifa, au taarifa za kifedha n.k zinaweza kutumiwa vibaya na wahalifu au watu wenye nia mbaya.
Soma Pia:
- Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imezinduliwa, ianze na wale wanatumia taarifa za watu kwenye Vifungashio
- Taasisi za afya zitekeleze utunzaji salama wa taarifa za wagonjwa
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) mmelifungia hili vioo? Ingawa taarifa nyingi zinahamia mtandaoni, lakini bado kuna haja ya kushughulikia vema hawa wanaotusambazia taarifa zetu mtaani kiholela. Onesheni mfano kwa taasisi kadhaa wengine wajifunze.