Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi: Ukitumia taarifa bInafsi za mtu bila idhini yake Faini Tsh. Milioni 100

Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi: Ukitumia taarifa bInafsi za mtu bila idhini yake Faini Tsh. Milioni 100

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Snapinst.app_481860549_17903465979121312_2939419438426086621_n_1080.jpg

Dkt. Noe Nnko
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imezitaka taasisi na mashirika kuwa makini katika matumizi ya taarifa za watu, kwani mtu yeyote ambaye taarifa zake zitatumika bila idhini anaweza kudai fidia ya hadi Sh. milioni 100, kwa mujibu wa sheria.

Akizungumza Machi 1, 2025, wakati wa kuwasilisha mada kuhusu teknolojia za ulinzi wa taarifa, changamoto zake, na umuhimu wa kuwa na sera za kusimamia taarifa binafsi kwa wanachama wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Mkurugenzi wa Tafiti za Ulinzi wa Taarifa na Teknolojia, Dk. Noe Nnko, amesema taasisi zote zinapaswa kuwa na afisa maalum wa kusimamia taarifa binafsi.

"Taasisi zinapaswa kuwa na afisa wa taarifa binafsi aliyefundishwa kutunza taarifa za watu kwa usahihi. Hata tarehe ya kuzaliwa ya mtu ni taarifa binafsi ambayo hairuhusiwi kutumiwa bila idhini," amesema Dk. Nnko.

Aidha, alisisitiza kuwa mtu ana haki ya kuomba taarifa zake ziondolewe kwenye tovuti, mitandao ya kijamii, au majukwaa mengine ikiwa zinatumika kinyume cha sheria.

Chanzo: Nipashe

Pia soma:
~ Ijue Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, sheria no. 11 ya mwaka 2022

~ Ma-MC wanaosambaza picha za Watu bila ridhaa waonywa
~ PDPC: Ukifika nyumba ya Kulala Wageni, marufuku kuandika unapotoka na unapokwenda
 
Wasomi wa kukremu shida. Hivi anayevujisha taarifa binafsi nchi hajulikani? Veggies ndo namba 1
 
Back
Top Bottom