KERO Tumeamua Jiji la (Dar) lipambwe na chupa za Energy drink? au wazalishaji wa bidhaa hizo wapo juu ya Sheria

KERO Tumeamua Jiji la (Dar) lipambwe na chupa za Energy drink? au wazalishaji wa bidhaa hizo wapo juu ya Sheria

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Kwa kipindi cha hivi karibuni kwenye maeneo mbalimbali nchini hususani ndani ya Jiji la Dar es salaam kumekuwepo na wimbi kubwa la kuenea kwa taka za chupa za plastiki za rangi hasa zinazotokana na vinywaji vya 'Energy drink' hali ambayo inaendelea kushamiri zaidi.

Katika uchunguzi wangu ambao nimeufanya kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, nimebaini kwenye kila hatua tano hadi 10 kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na chupa hizo.

Lakini katika hali ya kushangaza zaidi chupa hizi unazikuta hata kwenye mitaro ya maji hali ambayo inapelekea plastiki hizo kusafirishwa mpaka kwenye vyanzo vya maji na kupelekea kuweka hatarini uhai wa viumbe vinavyoishi kwenye maji pamoja na afya ya binadamu ambao wamekuwa wakitegemea vyanzo hivyo kupata huduma mbalimbali ikiwemo maji na samaki.

Naweza kuwa nipo sahihi kwa asilimia kubwa kusema kwamba, Jiji la Dar es Salaam kwa sasa ni kama limepambwa na chupa za rangi za plastiki, na sababu ni kutokana na chupa hizi kuonekana kila kona kama sio kila upande.

Suala hili limenifanya nirejee kauli ya aliyekuwa Mkurugenzi wa NEMC,Dkt. Samuel Gwamaka Mafwenga ambayo alitoa Mwezi November 2023 akiwataka wazalishaji wa bidhaa zinazotumia chupa za rangi kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wa kurejeleza chupa hizo ili zisiendelee kuharibu mazingira.

Pia baada kusikiliza kauli hiyo niliamua kupitia miongozo mbalimbali kuona inaelekeza nini kwenye suala kama hili linalogusa ustawi wa mazingira.
photo_2024-05-21_18-23-11.jpg

photo_2024-05-21_18-23-21.jpg

photo_2024-05-21_18-23-12.jpg
Miongozo hiyo kuanzia kwenye Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, mwongozo wa uthibiti wa taka ngumu kwa kutumia dhana ya punguza, tumia tena na rejeleza wa mwaka 2021 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 kwa ujumla wake inawataka wazalishaji wa taka hususani wawekezaji kushiriki kulinda mazingira kutokana na bidhaa wanazozalisha kwenda sokoni hasa zile zinazoweza kurejelezwa.

Kimamlaka nchini waliopewa dhamana ya kusimamia utekelezwaji wa Sheria na miongozo hiyo ni Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), lakini jambo la kushangaza zaidi suala la chupa za rangi kuzagaa mtaani limekuwa la kawaida na hatusikii wazi wahusika wakiwajibika licha ya kero hiyo, jambo ambalo linaacha maswali.

Unaweza kujiuliza kwamba hivi wahusika ambao ni wawekezaji wenye viwanda vinavyozalisha chupa za rangi wapo juu ya Sheria au mamlaka zimekosa meno ya kun'gata (kuwawajibisha kuzingatia Sheria na miongozo).

Kinyume na hivyo labda kama kuna jambo nyuma ya pazia, maana hali sio shwari hii ni kero ambayo kama haitapatiwa ufumbuzi wa haraka Dar es Salaam na maeneo mengine hususani ya majiji na miji yatazidi kupambwa na taka hizo ambazo ni hatari kwa ustawi wa mazingira.
photo_2024-05-21_18-25-06.jpg

photo_2024-05-21_18-25-05.jpg
Kama NEMC wamekuwa wakitoa matamko lakini hali bado ni changamoto basi mamlaka za juu zaidi kupitia Wizara yenye dhamana haina budi kuchukua hatua ya kufuatilia nini kinakwamisha uwajibikaji stahiki ili kama kuna uzembe kwa wasimamizi wa Sheria na miongozo au wazalishaji wawajibike ili mazingira yetu yaendelee kubakia salama japokuwa tumechelewa.

Ni muhimu viwanda vinavyozalisha chupa za rangi hasa vinywaji vya 'energy drink' kuhakikisha vinakuwa na teknolojia rafiki ya kurejeleza taka zinazotokana na bidhaa baada ya kwenda sokoni, na hili linatakiwa kuwekewa mkazo zaidi na kusimamia kwa ukaribu.


Tamko lililotolewa na NEMC, Novemba 2023

Pia Soma:
~
NEMC imetoa mwezi mmoja kwa viwanda vinavyozalisha Chupa za plastiki zenye rangi kuweka utaratibu wa kukusanya na kuhifadhi chupa hizo
~ Mo Dewji asema wameanzisha Kampeni ya kukusanya chupa za rangi nyeusi, wameshakusanya tani 21
~ NEMC ipige marufuku chupa za plastiki za rangi kuzalisha bidhaa kama energy drink
 
Serikali ikisimama kama ilivyokuwa vifungashio vya plastiki kipindi kile hata hizi chipa za energy zitatokomea.
Pia nadhani chupa za energy hazinunuliwi vinginevyo wale ndugu wanaokusanya chupa na kwenda kuuza kwa kg wasingeziacha.
 
TZ bana, sasa hao wanywaji wanaokunywa na kutupa hovyo hamuwaoni? Jifunzeni ustaarabu waTz acheni kusingizia watu kwa matatizo yenu ya kukosa ustaarabu. Sio hizo chupa tu vitu vingi watu wanatumia halafu wanatupa tu barabarani.
Watupe wapi sasa?
Serikali haiwezi kukwepa hizi lawama.

Hizo nchi au maeneo waliofanikiwa kudhibiti uchafu ni pamoja na kuweka vyombo vya kukusanya huo uchafu karibu kila pahala..

Chupa za azam kuna kipindi zilikua zinaokotwa na kurudishwa, shida ni hizi za Mo extra aloo kila kona zipo.
Waokota machupa nao hawaziokoti,( sijui kwanini).
Hizi ndio janga kubwa, kama zikitafutiwa utaratibu basi hii adha itapungua sana.

Sio rahisi kukuta kopo la maji barabarani limezagaa.
 
Watupe wapi sasa?
Serikali haiwezi kukwepa hizi lawama.

Hizo nchi au maeneo waliofanikiwa kudhibiti uchafu ni pamoja na kuweka vyombo vya kukusanya huo uchafu karibu kila pahala..

Chupa za azam kuna kipindi zilikua zinaokotwa na kurudishwa, shida ni hizi za Mo extra aloo kila kona zipo.
Waokota machupa nao hawaziokoti,( sijui kwanini).
Hizi ndio janga kubwa, kama zikitafutiwa utaratibu basi hii adha itapungua sana.

Sio rahisi kukuta kopo la maji barabarani limezagaa.
Wewe unatupa wapi takataka zako? Tupa sehemu sahihi, wastaarabu huwa wanatembea na chupa za maji au hizo za energy drink mpaka wapate sehemu sahihi ya kutupa. Wabongo sio wastaarabu ukiwa kwenye gari utaona tu chupa zinatupwa kutoka madirishani hapo unalaumu serikali?

Waokota chupa wanaokota clear chupa tu ndio zinakubalika kwenye recycling, zenye rangi hazikubaliwi hivyo hazinunuliwi.
 
Wewe unatupa wapi takataka zako? Tupa sehemu sahihi, wastaarabu huwa wanatembea na chupa za maji au hizo za energy drink mpaka wapate sehemu sahihi ya kutupa. Wabongo sio wastaarabu ukiwa kwenye gari utaona tu chupa zinatupwa kutoka madirishani hapo unalaumu serikali?

Waokota chupa wanaokota clear chupa tu ndio zinakubalika kwenye recycling, zenye rangi hazikubaliwi hivyo hazinunuliwi.
Weka mazingira sahihi, ustaarabu unafunzwa huzaliwi nao.

Hao unaona wanatupa hovyo wao wanaona ni sahihi, ukiweka dustbins maeneo mengi mtu anatupaje hovyo na mahali sahihi anapaona.
Sometimes watu wanajifunza kwa kuona tu.
 
TZ bana, sasa hao wanywaji wanaokunywa na kutupa hovyo hamuwaoni? Jifunzeni ustaarabu waTz acheni kusingizia watu kwa matatizo yenu ya kukosa ustaarabu. Sio hizo chupa tu vitu vingi watu wanatumia halafu wanatupa tu barabarani.
Watz tumekosa sana ustaarabu, lakini pia wazalishaji wa taka hizi wanawajibika pakubwa katika kuzoa taka hizi. Muuza machungwa mwenyewe anatembea na kikapu cha kuwekea maganda na asipokuwa nacho tunammind.
 
Unaweza kujiuliza kwamba hivi wahusika ambao ni wawekezaji wenye viwanda vinavyozalisha chupa za rangi wapo juu ya Sheria au mamlaka zimekosa meno ya kun'gata (kuwawajibisha kuzingatia Sheria na miongozo).
Wazalishaji hawana uwajibikaji wowote kuhusu masalia ya bidhaa. Ukinunua nanasi sokoni, hakuna sheria inayombana aliyekuuzia afuatilie ni wapi mtumiaji atayatupa mabaki. Suala kubwa hapo ni kuwabana watumiaji, na sheria ndogo ndogo za mamlaka ya miji zipo kabisa
 
Kwa kipindi cha hivi karibuni kwenye maeneo mbalimbali nchini hususani ndani ya Jiji la Dar es salaam kumekuwepo na wimbi kubwa la kuenea kwa taka za chupa za plastiki za rangi hasa zinazotokana na vinywaji vya 'Energy drink' hali ambayo inaendelea kushamiri zaidi.

Katika uchunguzi wangu ambao nimeufanya kwenye maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam, nimebaini kwenye kila hatua tano hadi 10 kuna uwezekano mkubwa wa kukutana na chupa hizo.

Lakini katika hali ya kushangaza zaidi chupa hizi unazikuta hata kwenye mitaro ya maji hali ambayo inapelekea plastiki hizo kusafirishwa mpaka kwenye vyanzo vya maji na kupelekea kuweka hatarini uhai wa viumbe vinavyoishi kwenye maji pamoja na afya ya binadamu ambao wamekuwa wakitegemea vyanzo hivyo kupata huduma mbalimbali ikiwemo maji na samaki.

Naweza kuwa nipo sahihi kwa asilimia kubwa kusema kwamba, Jiji la Dar es Salaam kwa sasa ni kama limepambwa na chupa za rangi za plastiki, na sababu ni kutokana na chupa hizi kuonekana kila kona kama sio kila upande.

Suala hili limenifanya nirejee kauli ya aliyekuwa Mkurugenzi wa NEMC,Dkt. Samuel Gwamaka Mafwenga ambayo alitoa Mwezi November 2023 akiwataka wazalishaji wa bidhaa zinazotumia chupa za rangi kuhakikisha wanakuwa na utaratibu wa kurejeleza chupa hizo ili zisiendelee kuharibu mazingira.

Pia baada kusikiliza kauli hiyo niliamua kupitia miongozo mbalimbali kuona inaelekeza nini kwenye suala kama hili linalogusa ustawi wa mazingira.
Miongozo hiyo kuanzia kwenye Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, mwongozo wa uthibiti wa taka ngumu kwa kutumia dhana ya punguza, tumia tena na rejeleza wa mwaka 2021 pamoja na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 kwa ujumla wake inawataka wazalishaji wa taka hususani wawekezaji kushiriki kulinda mazingira kutokana na bidhaa wanazozalisha kwenda sokoni hasa zile zinazoweza kurejelezwa.

Kimamlaka nchini waliopewa dhamana ya kusimamia utekelezwaji wa Sheria na miongozo hiyo ni Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), lakini jambo la kushangaza zaidi suala la chupa za rangi kuzagaa mtaani limekuwa la kawaida na hatusikii wazi wahusika wakiwajibika licha ya kero hiyo, jambo ambalo linaacha maswali.

Unaweza kujiuliza kwamba hivi wahusika ambao ni wawekezaji wenye viwanda vinavyozalisha chupa za rangi wapo juu ya Sheria au mamlaka zimekosa meno ya kun'gata (kuwawajibisha kuzingatia Sheria na miongozo).

Kinyume na hivyo labda kama kuna jambo nyuma ya pazia, maana hali sio shwari hii ni kero ambayo kama haitapatiwa ufumbuzi wa haraka Dar es Salaam na maeneo mengine hususani ya majiji na miji yatazidi kupambwa na taka hizo ambazo ni hatari kwa ustawi wa mazingira.
Kama NEMC wamekuwa wakitoa matamko lakini hali bado ni changamoto basi mamlaka za juu zaidi kupitia Wizara yenye dhamana haina budi kuchukua hatua ya kufuatilia nini kinakwamisha uwajibikaji stahiki ili kama kuna uzembe kwa wasimamizi wa Sheria na miongozo au wazalishaji wawajibike ili mazingira yetu yaendelee kubakia salama japokuwa tumechelewa.

Ni muhimu viwanda vinavyozalisha chupa za rangi hasa vinywaji vya 'energy drink' kuhakikisha vinakuwa na teknolojia rafiki ya kurejeleza taka zinazotokana na bidhaa baada ya kwenda sokoni, na hili linatakiwa kuwekewa mkazo zaidi na kusimamia kwa ukaribu.

View attachment 2996198
Tamko lililotolewa na NEMC, Novemba 2023

Pia Soma:
- NEMC imetoa mwezi mmoja kwa viwanda vinavyozalisha Chupa za plastiki zenye rangi kuweka utaratibu wa kukusanya na kuhifadhi chupa hizo
Jiji la Dar es Salaam wanaishi watu wachafu kuliko kawaida.
 
Hao Wazalishaji Wanakula Pamoja Na Viongozi Wanaohusika Na Mazingira. Yani Ukichunguza Kwenye Malipo Wamo Wanapewa Mpunga. Wee Piga Kelele Uwezavyo Lakini Hakuna Anayejali.
 
TZ bana, sasa hao wanywaji wanaokunywa na kutupa hovyo hamuwaoni? Jifunzeni ustaarabu waTz acheni kusingizia watu kwa matatizo yenu ya kukosa ustaarabu. Sio hizo chupa tu vitu vingi watu wanatumia halafu wanatupa tu barabarani.
 
Back
Top Bottom