Tumechoka matamko juu ya MSD, hatua za uwajibishwaji zifuatwe

Tumechoka matamko juu ya MSD, hatua za uwajibishwaji zifuatwe

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amegiza Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD) kufumuliwa na kusukwa upya ndani ya miezi sita hilo likienda sambamba na kuondoa watumishi waliokaa zaidi ya miaka 20.


Waziri Ummy amesema kumekuwapo na tuhuma kubwa za rushwa MSD na licha ya kuondoa wakuu wa idara bado kunahitajika mabadiliko makubwa illi kuiunda upya. Ikumbukwe hii sio mara ya kwanza kwa serikali kutoa maelekezo ya kufumua MSD, mara kwa mara maagizo ya kuifumua MSD yamekuwa yakijirudia.

Mei 9, mwaka huu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alifanya ziara MSD na kuagiza watuhumiwa wote wa ubadhirifu kama ulivyoainishwa na CAG wachukuliwe hatua, huku akiahidi kuwa TAKUKURU inafanyia kazi hoja zote zilizotolewa kuhusu bohari hiyo.

Aprili 14, mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan, alimteua Ofisa Mwandamizi wa Kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PWC), Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya MSD, pia alimteua Kiongozi Mkuu wa mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance, Ali Tukai, kuwa Mtendaji Mkuu wa MSD.

Rais Samia akitaka uwajibikaji kwa MSD ili kuwahudumia wananchi hasa kwa kupata dawa na vifaatiba muhimu kwa kuwa serikali inaelekeza fedha nyingi eneo hilo.

Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia, yalifanyika siku chache baada ya CAG, kubaini bohari hiyo ilishikilia zaidi ya Sh. bilioni 14 za hospitali kwa mwaka mzima bila kupeleka awa na vifaa tiba. Pia alibaini MSD ilifanya ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni tisa bila mkataba halali, pia ilifanya malipo ya Sh. bilioni 3.52 kwa wazabuni sita bila kufuata taratibu na kuitaarifu Bodi ya Zabuni ya MSD.

Aidha, walifanya zabuni 23 zenye thamani ya Sh. bilioni 8.55 nje ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa mtandao (TANePS) unaosimamiwa na Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), kinyume na ma- takwa ya sheria.

Walifanya malipo ya awali kiasi cha Sh. bilioni 14.89 kwa wazabuni watano bila mkataba wowote wa makubaliano mengine ambayo yali- bainisha msingi wa malipo ya awali. Aidha, waliendesha mchakato wa ununuzi na kutoa mkataba wa kusambaza Liquid Syrup' wenye thamani ya Sh. milioni 989 bila kush- irikisha Bodi ya Zabuni ya MSD. Pia walitumia Sh. milioni 215 kugharamia posho ya watumishi watatu waliokwenda China kwenye majadiliano ya kuleta mashine za Dialysis kwa siku 61.

Waziri Mkuu, Majaliwa alivyotembelea alisema walibaini kuna udhaifu wa usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi licha ya kwamba wamelipwa. Katika idara ya ununuzi walibaini kuwapo watumishi ambao sio wataalamu na kuagiza wote 16 kuondolewa na kuwekwa watumishi wenye taaluma hiyo. Kwa maelekezo hayo, inadhihirisha kuwa kuna tatizo kubwa ambalo hata serikali inaliona ni wakati wa kufanya uamuzi ambao utakwenda
kuondoa ufisadi unaodaiwa kuwapo.
Tayari CAG amethibitisha kuwapo kwa upigaji mkubwa, lakini hatua ambazo zimeendelea kuchukuliwa ikiwamo kubadilisha uongozi wa juu wa bohari bado hazijasaidia na sasa waziri anaeleza uwapo wa upigaji uliokithiri.

Tunaamini maelekezo ya Waziri Mkuu ni ya juu zaidi kuliko ya Waziri wa sekta husika.
Na pia tunaamini Waziri wa Sekta kuja na maelekezo mengine kabla ya kueleza yale ya awali yaliyotolewa na Waziri Mkuu utekelezaji wake umefikia wapi sio jambo zuri, hivyo ni muhimu serikali ikachukua hatua za utatuzi wa kudumu kuliko kuendelea kuja na maelekezo juu ya maelekezo

Kama tatizo limeonekana basi lishughulikiwe kwa kutumia mihimili muhimu ya serikali ambayo inaona kila mahali ili kuondoa majadiliano ya mara kwa mara kuhusu MSD kukosa vifaa tiba na dawa.huku wananchi wakiumia kwa kukosa vifaa tib ana dawa.

Disclaimer: Sehemu kubwa ya andiko hili imetoka kwenye Gazeti la Nipashe toleo namba 0581019
Untitled design (16).jpg
 
pale hata umpeleke Ummy mwenyewe akawe Director hakuna muujiza atafanya tatizo la MSD ni mfumo mbovu wa manunuzi na 20% za viongozi
 
Hii MSD ni pasua kichwa sana, JPM aliweka mpaka Wanajeshi hapo lakini waapi, Rais Samia ana kazi kubwa sana ya kufanya hapa
 
Nchi ya majizi hii, upigaji kila kona….. jitahidi kukwapua popote ulipo ili upunguze kulalamika.
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amegiza Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD) kufumuliwa na kusukwa upya ndani ya miezi sita hilo likienda sambamba na kuondoa watumishi waliokaa zaidi ya miaka 20.


Waziri Ummy amesema kumekuwapo na tuhuma kubwa za rushwa MSD na licha ya kuondoa wakuu wa idara bado kunahitajika mabadiliko makubwa illi kuiunda upya. Ikumbukwe hii sio mara ya kwanza kwa serikali kutoa maelekezo ya kufumua MSD, mara kwa mara maagizo ya kuifumua MSD yamekuwa yakijirudia.

Mei 9, mwaka huu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alifanya ziara MSD na kuagiza watuhumiwa wote wa ubadhirifu kama ulivyoainishwa na CAG wachukuliwe hatua, huku akiahidi kuwa TAKUKURU inafanyia kazi hoja zote zilizotolewa kuhusu bohari hiyo.

Aprili 14, mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan, alimteua Ofisa Mwandamizi wa Kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PWC), Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya MSD, pia alimteua Kiongozi Mkuu wa mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance, Ali Tukai, kuwa Mtendaji Mkuu wa MSD.

Rais Samia akitaka uwajibikaji kwa MSD ili kuwahudumia wananchi hasa kwa kupata dawa na vifaatiba muhimu kwa kuwa serikali inaelekeza fedha nyingi eneo hilo.

Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia, yalifanyika siku chache baada ya CAG, kubaini bohari hiyo ilishikilia zaidi ya Sh. bilioni 14 za hospitali kwa mwaka mzima bila kupeleka awa na vifaa tiba. Pia alibaini MSD ilifanya ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni tisa bila mkataba halali, pia ilifanya malipo ya Sh. bilioni 3.52 kwa wazabuni sita bila kufuata taratibu na kuitaarifu Bodi ya Zabuni ya MSD.

Aidha, walifanya zabuni 23 zenye thamani ya Sh. bilioni 8.55 nje ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa mtandao (TANePS) unaosimamiwa na Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), kinyume na ma- takwa ya sheria.

Walifanya malipo ya awali kiasi cha Sh. bilioni 14.89 kwa wazabuni watano bila mkataba wowote wa makubaliano mengine ambayo yali- bainisha msingi wa malipo ya awali. Aidha, waliendesha mchakato wa ununuzi na kutoa mkataba wa kusambaza Liquid Syrup' wenye thamani ya Sh. milioni 989 bila kush- irikisha Bodi ya Zabuni ya MSD. Pia walitumia Sh. milioni 215 kugharamia posho ya watumishi watatu waliokwenda China kwenye majadiliano ya kuleta mashine za Dialysis kwa siku 61.

Waziri Mkuu, Majaliwa alivyotembelea alisema walibaini kuna udhaifu wa usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi licha ya kwamba wamelipwa. Katika idara ya ununuzi walibaini kuwapo watumishi ambao sio wataalamu na kuagiza wote 16 kuondolewa na kuwekwa watumishi wenye taaluma hiyo. Kwa maelekezo hayo, inadhihirisha kuwa kuna tatizo kubwa ambalo hata serikali inaliona ni wakati wa kufanya uamuzi ambao utakwenda
kuondoa ufisadi unaodaiwa kuwapo.
Tayari CAG amethibitisha kuwapo kwa upigaji mkubwa, lakini hatua ambazo zimeendelea kuchukuliwa ikiwamo kubadilisha uongozi wa juu wa bohari bado hazijasaidia na sasa waziri anaeleza uwapo wa upigaji uliokithiri.

Tunaamini maelekezo ya Waziri Mkuu ni ya juu zaidi kuliko ya Waziri wa sekta husika.
Na pia tunaamini Waziri wa Sekta kuja na maelekezo mengine kabla ya kueleza yale ya awali yaliyotolewa na Waziri Mkuu utekelezaji wake umefikia wapi sio jambo zuri, hivyo ni muhimu serikali ikachukua hatua za utatuzi wa kudumu kuliko kuendelea kuja na maelekezo juu ya maelekezo

Kama tatizo limeonekana basi lishughulikiwe kwa kutumia mihimili muhimu ya serikali ambayo inaona kila mahali ili kuondoa majadiliano ya mara kwa mara kuhusu MSD kukosa vifaa tiba na dawa.huku wananchi wakiumia kwa kukosa vifaa tib ana dawa.

Disclaimer: Sehemu kubwa ya andiko hili imetoka kwenye Gazeti la Nipashe toleo namba 0581019View attachment 2305641
Chukua. Chako. Mapema.
Karbn tufanze ujasiriamali wa ku-supply mchicha mkavu.
Km hao popo huko juu hawaogopi kuua wananchi tusiogope eti 'kuvunja sheria' kwa "kujiMalawi" chap!
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amegiza Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD) kufumuliwa na kusukwa upya ndani ya miezi sita hilo likienda sambamba na kuondoa watumishi waliokaa zaidi ya miaka 20.


Waziri Ummy amesema kumekuwapo na tuhuma kubwa za rushwa MSD na licha ya kuondoa wakuu wa idara bado kunahitajika mabadiliko makubwa illi kuiunda upya. Ikumbukwe hii sio mara ya kwanza kwa serikali kutoa maelekezo ya kufumua MSD, mara kwa mara maagizo ya kuifumua MSD yamekuwa yakijirudia.

Mei 9, mwaka huu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alifanya ziara MSD na kuagiza watuhumiwa wote wa ubadhirifu kama ulivyoainishwa na CAG wachukuliwe hatua, huku akiahidi kuwa TAKUKURU inafanyia kazi hoja zote zilizotolewa kuhusu bohari hiyo.

Aprili 14, mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan, alimteua Ofisa Mwandamizi wa Kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PWC), Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya MSD, pia alimteua Kiongozi Mkuu wa mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance, Ali Tukai, kuwa Mtendaji Mkuu wa MSD.

Rais Samia akitaka uwajibikaji kwa MSD ili kuwahudumia wananchi hasa kwa kupata dawa na vifaatiba muhimu kwa kuwa serikali inaelekeza fedha nyingi eneo hilo.

Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia, yalifanyika siku chache baada ya CAG, kubaini bohari hiyo ilishikilia zaidi ya Sh. bilioni 14 za hospitali kwa mwaka mzima bila kupeleka awa na vifaa tiba. Pia alibaini MSD ilifanya ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni tisa bila mkataba halali, pia ilifanya malipo ya Sh. bilioni 3.52 kwa wazabuni sita bila kufuata taratibu na kuitaarifu Bodi ya Zabuni ya MSD.

Aidha, walifanya zabuni 23 zenye thamani ya Sh. bilioni 8.55 nje ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa mtandao (TANePS) unaosimamiwa na Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), kinyume na ma- takwa ya sheria.

Walifanya malipo ya awali kiasi cha Sh. bilioni 14.89 kwa wazabuni watano bila mkataba wowote wa makubaliano mengine ambayo yali- bainisha msingi wa malipo ya awali. Aidha, waliendesha mchakato wa ununuzi na kutoa mkataba wa kusambaza Liquid Syrup' wenye thamani ya Sh. milioni 989 bila kush- irikisha Bodi ya Zabuni ya MSD. Pia walitumia Sh. milioni 215 kugharamia posho ya watumishi watatu waliokwenda China kwenye majadiliano ya kuleta mashine za Dialysis kwa siku 61.

Waziri Mkuu, Majaliwa alivyotembelea alisema walibaini kuna udhaifu wa usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi licha ya kwamba wamelipwa. Katika idara ya ununuzi walibaini kuwapo watumishi ambao sio wataalamu na kuagiza wote 16 kuondolewa na kuwekwa watumishi wenye taaluma hiyo. Kwa maelekezo hayo, inadhihirisha kuwa kuna tatizo kubwa ambalo hata serikali inaliona ni wakati wa kufanya uamuzi ambao utakwenda
kuondoa ufisadi unaodaiwa kuwapo.
Tayari CAG amethibitisha kuwapo kwa upigaji mkubwa, lakini hatua ambazo zimeendelea kuchukuliwa ikiwamo kubadilisha uongozi wa juu wa bohari bado hazijasaidia na sasa waziri anaeleza uwapo wa upigaji uliokithiri.

Tunaamini maelekezo ya Waziri Mkuu ni ya juu zaidi kuliko ya Waziri wa sekta husika.
Na pia tunaamini Waziri wa Sekta kuja na maelekezo mengine kabla ya kueleza yale ya awali yaliyotolewa na Waziri Mkuu utekelezaji wake umefikia wapi sio jambo zuri, hivyo ni muhimu serikali ikachukua hatua za utatuzi wa kudumu kuliko kuendelea kuja na maelekezo juu ya maelekezo

Kama tatizo limeonekana basi lishughulikiwe kwa kutumia mihimili muhimu ya serikali ambayo inaona kila mahali ili kuondoa majadiliano ya mara kwa mara kuhusu MSD kukosa vifaa tiba na dawa.huku wananchi wakiumia kwa kukosa vifaa tib ana dawa.

Disclaimer: Sehemu kubwa ya andiko hili imetoka kwenye Gazeti la Nipashe toleo namba 0581019View attachment 2305641



Niliandika hii


Mwaka 2016 nilienda Tanzania baada ya kukaa muda mrefu US. Rafiki yangu ambaye nilisoma naye Primary alikuwa ndiyo auditor mkubwa pale MSD hivyo bila mimi kujua aliongea na Managing Director kuhusu kupata watu wenye ujuzi na kampuni za kusambaza madawa kama MSD

Wakati na maongezi yao yule rafiki yangu akampa email Lauren Bwanankuru ili aweza kufanya mahojiano ya mwanzo ya nafasi ya Director pale wakati wa likizo yangu Tanzania. Wakati huo nilikuwa nafanya kazi kampuni kubwa ya usambazaji ya US ambayo ipo Ohio Cardinal Health: Healthcare Solutions, Logistics & Supplies. Nikapanga siku ya kwenda kwenye mahojiano ili ikiwekana nifanye kazi pale kama Director.

Baada ya kufika pale huyu Managing Director ambaye naye alikuwa bado ni kijana, tulianza kuongea na kuhojiana:
1. Unarudi lini TZ? Nikamwambia nitarudi nikipata kazi siwezi kuacha kazi na kurudi bila kuwa na uhakika
2. Boss: Natafuta Directors lakini ni mpaka tutume maombi serikalini lakini nimependa sana uzoefu wako
3. Mimi: Asante. Je, Directors wote wako wapi? Siwaoni hapa.
4. Boss: Wamesimamishwa na hii bodi mpya kupisha uchunguzi!

Niliogopa na kuanza kuuliza maswali:
1. Mimi: Sasa nataka nijue boss Je hawa Directors wanaripoti kwako au kwa bodi? Boss akasema kwangu mimi
2. Mimi: Je, Director wanafanya kazi kwa kupitia list ya malengo ya mwaka (company goals). Boss hapana
3. Mimi: Hivyo mtu yeyote wizarani kama mkurugenzi, katibu au waziri anaweza akaja na kumsimamisha kazi Director yeyote ? Boss ndiyo

Nikamwangalia usoni nikamwambia moja kwa moja nakuonea huruma sana. Mimi sitaweza kufanya kazi hapa bila kujali pesa au mafao yenu kwasababu zifuatazo:

1. Kwanza inashangaza viongozi kusimamishwa na bodi wakati wewe hujasimamishwa na wanaripoti kwako
2. Inaelekea ukiwa Director kila mtu ni boss wako na sio wewe pekee. Hii mimi sioni kama ni utaratibu mzuri
3. Usipokuwa na malengo ya kampuni na kila Director kujua majukumu yake ya mwaka ni rahisi sana kwa mtu kuja na kunifukuza bila sababu kwa kutafuta sifa tu. Mimi siwezi kuweka familia yangu kwenye mazingira hayo sina shida ya kazi kiasi hicho.

Aliniangalia na kunishangaa kiasi nilivyokuwa wazi kwake. Nikamwambia kazi yako ngumu na wanavopenda sifa nakushauri utafute wakili mzuri maana sio muda utatengenezewa kesi Boss akacheka! Mimi niko clean.

Niliyosema yote yametokea! Kuna utaratibu mbaya kwenye hizi kampuni na ni ngumu sana kupata watu wazuri kwasababu ya siasa.
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, amegiza Bodi ya Wakurugenzi ya Bohari ya Dawa (MSD) kufumuliwa na kusukwa upya ndani ya miezi sita hilo likienda sambamba na kuondoa watumishi waliokaa zaidi ya miaka 20.


Waziri Ummy amesema kumekuwapo na tuhuma kubwa za rushwa MSD na licha ya kuondoa wakuu wa idara bado kunahitajika mabadiliko makubwa illi kuiunda upya. Ikumbukwe hii sio mara ya kwanza kwa serikali kutoa maelekezo ya kufumua MSD, mara kwa mara maagizo ya kuifumua MSD yamekuwa yakijirudia.

Mei 9, mwaka huu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alifanya ziara MSD na kuagiza watuhumiwa wote wa ubadhirifu kama ulivyoainishwa na CAG wachukuliwe hatua, huku akiahidi kuwa TAKUKURU inafanyia kazi hoja zote zilizotolewa kuhusu bohari hiyo.

Aprili 14, mwaka huu, Rais Samia Suluhu Hassan, alimteua Ofisa Mwandamizi wa Kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PWC), Slaa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya MSD, pia alimteua Kiongozi Mkuu wa mradi wa USAID Global Health Supply Chain Technical Assistance, Ali Tukai, kuwa Mtendaji Mkuu wa MSD.

Rais Samia akitaka uwajibikaji kwa MSD ili kuwahudumia wananchi hasa kwa kupata dawa na vifaatiba muhimu kwa kuwa serikali inaelekeza fedha nyingi eneo hilo.

Mabadiliko yaliyofanywa na Rais Samia, yalifanyika siku chache baada ya CAG, kubaini bohari hiyo ilishikilia zaidi ya Sh. bilioni 14 za hospitali kwa mwaka mzima bila kupeleka awa na vifaa tiba. Pia alibaini MSD ilifanya ununuzi wa vifaa tiba vyenye thamani ya zaidi ya Shilingi bilioni tisa bila mkataba halali, pia ilifanya malipo ya Sh. bilioni 3.52 kwa wazabuni sita bila kufuata taratibu na kuitaarifu Bodi ya Zabuni ya MSD.

Aidha, walifanya zabuni 23 zenye thamani ya Sh. bilioni 8.55 nje ya mfumo wa ununuzi wa umma kwa mtandao (TANePS) unaosimamiwa na Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma (PPRA), kinyume na ma- takwa ya sheria.

Walifanya malipo ya awali kiasi cha Sh. bilioni 14.89 kwa wazabuni watano bila mkataba wowote wa makubaliano mengine ambayo yali- bainisha msingi wa malipo ya awali. Aidha, waliendesha mchakato wa ununuzi na kutoa mkataba wa kusambaza Liquid Syrup' wenye thamani ya Sh. milioni 989 bila kush- irikisha Bodi ya Zabuni ya MSD. Pia walitumia Sh. milioni 215 kugharamia posho ya watumishi watatu waliokwenda China kwenye majadiliano ya kuleta mashine za Dialysis kwa siku 61.

Waziri Mkuu, Majaliwa alivyotembelea alisema walibaini kuna udhaifu wa usambazaji wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi licha ya kwamba wamelipwa. Katika idara ya ununuzi walibaini kuwapo watumishi ambao sio wataalamu na kuagiza wote 16 kuondolewa na kuwekwa watumishi wenye taaluma hiyo. Kwa maelekezo hayo, inadhihirisha kuwa kuna tatizo kubwa ambalo hata serikali inaliona ni wakati wa kufanya uamuzi ambao utakwenda
kuondoa ufisadi unaodaiwa kuwapo.
Tayari CAG amethibitisha kuwapo kwa upigaji mkubwa, lakini hatua ambazo zimeendelea kuchukuliwa ikiwamo kubadilisha uongozi wa juu wa bohari bado hazijasaidia na sasa waziri anaeleza uwapo wa upigaji uliokithiri.

Tunaamini maelekezo ya Waziri Mkuu ni ya juu zaidi kuliko ya Waziri wa sekta husika.
Na pia tunaamini Waziri wa Sekta kuja na maelekezo mengine kabla ya kueleza yale ya awali yaliyotolewa na Waziri Mkuu utekelezaji wake umefikia wapi sio jambo zuri, hivyo ni muhimu serikali ikachukua hatua za utatuzi wa kudumu kuliko kuendelea kuja na maelekezo juu ya maelekezo

Kama tatizo limeonekana basi lishughulikiwe kwa kutumia mihimili muhimu ya serikali ambayo inaona kila mahali ili kuondoa majadiliano ya mara kwa mara kuhusu MSD kukosa vifaa tiba na dawa.huku wananchi wakiumia kwa kukosa vifaa tib ana dawa.

Disclaimer: Sehemu kubwa ya andiko hili imetoka kwenye Gazeti la Nipashe toleo namba 0581019View attachment 2305641

Usipate tabu sana, UMMY MWALIMU na yule boyfriend wake wako kazini kuhakisha wanavuna MSD. Watabadilisha hadi vitasa kwa visingizio visivyo na mantiki ili mradi wapiga dili wao waingie MSD na kuanza kuuza kila kitu. Iko Siku hizi kelele za UMMY Watanzania watajua ukweli.
 
Niliandika hii


Mwaka 2016 nilienda Tanzania baada ya kukaa muda mrefu US. Rafiki yangu ambaye nilisoma naye Primary alikuwa ndiyo auditor mkubwa pale MSD hivyo bila mimi kujua aliongea na Managing Director kuhusu kupata watu wenye ujuzi na kampuni za kusambaza madawa kama MSD

Wakati na maongezi yao yule rafiki yangu akampa email Lauren Bwanankuru ili aweza kufanya mahojiano ya mwanzo ya nafasi ya Director pale wakati wa likizo yangu Tanzania. Wakati huo nilikuwa nafanya kazi kampuni kubwa ya usambazaji ya US ambayo ipo Ohio Cardinal Health: Healthcare Solutions, Logistics & Supplies. Nikapanga siku ya kwenda kwenye mahojiano ili ikiwekana nifanye kazi pale kama Director.

Baada ya kufika pale huyu Managing Director ambaye naye alikuwa bado ni kijana, tulianza kuongea na kuhojiana:
1. Unarudi lini TZ? Nikamwambia nitarudi nikipata kazi siwezi kuacha kazi na kurudi bila kuwa na uhakika
2. Boss: Natafuta Directors lakini ni mpaka tutume maombi serikalini lakini nimependa sana uzoefu wako
3. Mimi: Asante. Je, Directors wote wako wapi? Siwaoni hapa.
4. Boss: Wamesimamishwa na hii bodi mpya kupisha uchunguzi!

Niliogopa na kuanza kuuliza maswali:
1. Mimi: Sasa nataka nijue boss Je hawa Directors wanaripoti kwako au kwa bodi? Boss akasema kwangu mimi
2. Mimi: Je, Director wanafanya kazi kwa kupitia list ya malengo ya mwaka (company goals). Boss hapana
3. Mimi: Hivyo mtu yeyote wizarani kama mkurugenzi, katibu au waziri anaweza akaja na kumsimamisha kazi Director yeyote ? Boss ndiyo

Nikamwangalia usoni nikamwambia moja kwa moja nakuonea huruma sana. Mimi sitaweza kufanya kazi hapa bila kujali pesa au mafao yenu kwasababu zifuatazo:

1. Kwanza inashangaza viongozi kusimamishwa na bodi wakati wewe hujasimamishwa na wanaripoti kwako
2. Inaelekea ukiwa Director kila mtu ni boss wako na sio wewe pekee. Hii mimi sioni kama ni utaratibu mzuri
3. Usipokuwa na malengo ya kampuni na kila Director kujua majukumu yake ya mwaka ni rahisi sana kwa mtu kuja na kunifukuza bila sababu kwa kutafuta sifa tu. Mimi siwezi kuweka familia yangu kwenye mazingira hayo sina shida ya kazi kiasi hicho.

Aliniangalia na kunishangaa kiasi nilivyokuwa wazi kwake. Nikamwambia kazi yako ngumu na wanavopenda sifa nakushauri utafute wakili mzuri maana sio muda utatengenezewa kesi Boss akacheka! Mimi niko clean.

Niliyosema yote yametokea! Kuna utaratibu mbaya kwenye hizi kampuni na ni ngumu sana kupata watu wazuri kwasababu ya siasa.
Umesema vyema sana, kwa uzoefu wako huo, unadhani nini kiwe cha kwanza kurekebishwa na kuboreshwa pale?
 
Usipate tabu sana, UMMY MWALIMU na yule boyfriend wake wako kazini kuhakisha wanavuna MSD. Watabadilisha hadi vitasa kwa visingizio visivyo na mantiki ili mradi wapiga dili wao waingie MSD na kuanza kuuza kila kitu. Iko Siku hizi kelele za UMMY Watanzania watajua ukweli.
Tufungulie hii code, boyfriend ni nani?
 
Back
Top Bottom