Bima ya Afya ni mfumo wa kumwahidi kumrejeshea mwanachama hali ya Afya bira malipo pindi anapopata shida ya kiafya kwa kuuugua au kulazwa hospitalini hasa pale tu anapokuwa amelipia michango ya marejesho (premiums) kila mwezi au kwa mwaka.
Huko nyuma hasa miaka ya kuanzia 2010 kurudi nyuma; watu wengi walikuwa hawana elimu ya umuhimu wa Bima ya Afya. Hospitali nyingi zilikuwa hazipokei Bima ya Afya isipokuwa za Serikali na baadhi za watu binafsi. Pia mgonjwa mwenye Bima ya Afya alikuwa hapati huduma ya kurudhisha na ilikuwa si ya haraka kwani inasemekana alikuwa akithaminiwa mgonjwa mwenye Cash! Pia dawa nyingi zilikuwa hazijawekwa Kwenye Bima.
Hali hii iliwafanya watanzania kuidharau Bima na kutoona umuhimu wa kuwa nayo au kuwakatia wategemezi.
Kwa kipindi kirefu sasa toka miaka hiyo; Bima ya Afya ilikuwa imejizolea umaarufu sana na kupendwa na we ananchi kwani mgonjwa mwenye Bima ya Afya alikuwa akijisikia Fahari kuwa na Bima kwani hudumu zilikuwa Bomba. Dawa Kama zote zilikuwa zimewekwa Kwenye Bima. Pia kupitia tangazo la Serikali na mkazo wa Dada yetu Ummy Mwalimu la kuhamasisha watu kuwa na Bima za Afya; wananchi wengi waliona umuhimu wa kumiwa nayo.
Bima za Afya Kama NHIF; STRATEGIS, AAR, NSSF na ICF zimekuwa kimbilio kwa wananchi na kuwa mkombozi wao kwa huduma za matibabu. Hudumu ni nzuri tena ya kwaminika. Baadhi ya hospitali za Serikali na binafsi wamefanikiwa kutenganisha kabisa Vitengo vya matibabu; yaani kitengo cha wagonjwa wenye Bima za Afya na Kitengo cha wagonjwa wenye Cash. Na hii imekuwa msaada sana kwa matibabu. Hongera sana!
Kipindi hiki; wewe ni mtanzania gani ambae huna Bima ya Afya? Kila mtu atakushangaa na kukuonea huruma endapo umepatwa na tatizo la Afya au mtoto waki ama ndugu yako ameugua na huku ukiwa huna Bima ya Afya huku mfukoni huna hata Mia! Happy ndo utauona rangi zote!
Baada ya utangulizi huo,sasa niende Kwenye maada husika isemayo: " Tumehamasishwa sana kuwa na Bima za Afya na kuielewa Serikali; Mbona Dawa Mhimu kwa Jamii Zimeondolewa Kwenye Bima ya Afya!"
Ni kweli kuanzia mwezi ulopia Kama si mwezi wa nane, orodha ya dawa Kama 18 za magonjwa ya Pressure na Kisukari yameondolewa kwenye Bima.
Dawa hizo ni zile nzuri kweli kwa watumiaji kwani ndo zinazoonekana kuleta nafuu na kunesha kwa baadhi ya wagonjwa. Yaani hushusha au kupandisha fasta Presha na sukari. Hureta good regulation ya magonjwa hayo.
Wahenga walisema kizuri kina gharama; ni kweli dawa hizo ni za bei sana kwani huuzwa kwa Bei ya juu. Za Presha huuzwa hata tsh 36000 na zaidi kwa vidonge 30!
Kama wewe una Presha au Kisukari ama una ndugu; jirani au jamaa ana magonjwa hayo na ulikuwa unatimia kati ya Hizi dawa Sasa hutozipata yen bure kwa Bima Sasa utakuea unalipa Cash.
Dawa zenyewe ni Hizi Happ.
A. Dawa za Presha.
Dawa za Presha zilizoondolewa Kwenye Bima ni:
1. Bisoprolol Fumarate 5mg
2. Bisoprolol Fumarate 10mg
3. Termisatan 40 mg
4. Termisatan 80 mg
5. Termisatan 120 mg
6. Concor 5 mg
7. Concor 10 mg
8. Benicar 5mg, 10mg
9. Hydrochlorothiazide
10. Benicar
11. Lopressor
18. Furosemide
.....
Nb: Dawa zilizobaki Kwenye Bima ni Kama
- Lasix
- Losatan
- Amlodipine
- Alsatan
.......
B. Dawa za Sukali
Dawa za Presha zilizoondolewa Kwenye Bima ni:
1. Dipeptidyl peptidase
2. Amylinomimetic
3. Dopamine
...