Tumehamasishwa sana kuwa na bima za afya na kuielewa serikali; mbona dawa mhimu kwa jamii zimeondolewa kwenye bima ya afya hi?

Asante sana mleta mada kwa kuleta taarifa hii. Siyo hii tu hadi steipes za sukari wamezitoa yaani bima vile haina msada tena kwa wateja. Item zilizotolewa ni 180 na sio 18.
 
Asante sana mleta mada kwa kuleta taarifa hii. Siyo hii tu hadi steipes za sukari wamezitoa yaani bima vile haina msada tena kwa wateja. Item zilizotolewa ni 180 na sio 18.
Kwa maana nyingine watu wenye mahitaji ya hizo dawa na wanalipia Bima za afya kama hawana pesa ndio umauti unawajongelea!
Kwa hivi sasa vyombo vya kutetea wateja naona kama taasisi zinazohusika na kudhibiti uendeshaji wa mashirika vimepatwa na paralysis. Hivi taasisi inaachwa ili imalize watu bila ya chombo kinachodhititi uendeshaji wa Bima kufata mchakato wa malalamiko? Hivi wawakilishi wetu Bungeni wanaliona hilo? Au mpaka mheshimiwa Rais aingilie kati kama alivyofanya kwenye kikokotoo?
 
Furosemide ndio hiyo hiyo Lasix. Sasa mara unasema imetolewa na hapo hapo unasema inabaki
 
NHIF ni jipu kubwa sana, Mh. Rais wangu naomba uende pale Kurasini NHIF HQ plz, madudu yao ni mengi sana
 
Na inakuja Universal Health Coverage...CHF iliyoboreshwa itakuwa ni lazima.
 
Relax ndugu. Hayo marekebisho sio rasmi. Utekelezaji wake bado. Na msingi wa wao kuleta mapendekezo hayo sio wao kama wao NHIF, ni hao hao politicians.
 
Kuna mtegemezi wangu alinyimwa dawa alizokuwa akitumia na kuambiwa Sasa dawa haiko kwa Bima!
 
Mleta mada napenda kukusahihisha.
1. Furosemide ndio lasix. Kama ilivyo kwa methyldopa=aldomet, spironoloctone=aldactone etc. Hii ni kwa sababu dawa huwa ziko na generic name pamoja na commercial name.
2. Blood pressure is one of the vital signs and not a disease. When blood pressure deviates from normal and become high above the normal range a person becomes Hypertensive kwa hiyo pressure ni kitu kingine na hypertension ni kitu kingine
 
Lakini Maada kuu iko sahihi? Je hakuna dawa zilizoondolewa kwenye Bima? This is the matter plz!
 

Vitu vingine unavipotezea tu mkuu hatakama ni unajua sana cha msingi tu angalia ujumbe zaidi hizo mbwembwe nyingine sijui normaltensive , hypertension , blood pressure , tuachie sisi
 
Bima zote za afya zinabagua kutoa dawa nzuri hata za ngozi.

Ifike wakati Sasa Waziri wa afya aingilie na kusimamia kidete dawa zikubaliwe na bima.mwisho wa siku haitakuwa na maana Kama Nina inatoa Panadol tuu
Huu no utapeli na wizi kwa wananchi na wateja wao.
 
Kikubwa cha kujua taasisi zote hasa za gvt haziko kwa ajili ya kumkomboa mnyonge bali kumnyonya huku wakija na mwamvuli wa kusaidia.angalisia nssf,nhif,nic,tucta yaani ni unyonyaji na mateso.
Usije ukajichanganya kufanya kazi na serikali with ur money.Poleni wana bima.
 
Relax ndugu. Hayo marekebisho sio rasmi. Utekelezaji wake bado. Na msingi wa wao kuleta mapendekezo hayo sio wao kama wao NHIF, ni hao hao politicians.

Sasa atulie wakati hao NHIF ndo watekelezaji, tunapaswa kupiga kelele zote na vyombo vyote vya habari viandike habari hizi
 
Asante Sana kwa Maelezo mazuri sana. Ni kweli kabisa kuwa NHIF wamepunguza baadhi ya huduma walizokuwa wakitoa hapo mwanzo.
NHIF wanawataka Madaktari na watumishi wengine wa sekta ya afya kutoa huduma zilizo ndani ya mwongozo wa taifa wa matibabu (standard treatment guideline), kwa maana nyingine ni kwamba ukiandika dawa isiyokuwepo kwenye huo mwongozo Nhif hawatakulipa wewe mtoa huduma.

Kwa Mana hiyo ndio maana watoa huduma wanakataa kutoa huduma hizo ambazo hawataweza kulipwa na Nhif japokuwa zinasaidia wagonjwa na hata kama Wagonjwa hao walizitumia awali. Watoa huduma wamelalamika sana kwa Nhif lakini nao Nhif wanawarushia mpira wizara ya afya ambao ndio hutengeneza huo mwongozo wa matibabu kupitia kwa wataalamu mbalimbali kutoka hospitali zetu kubwa km muhimbili.

Sintofahamu ipo hapa: pamoja na kuwa nhif hawalipi huduma ambazo ziko nje ya huo mwongozo lakini kwa hospitali kubwa Kama muhimbili, Bugando na kcmc wanalipwa hata kama wakitoa huduma kwa Wagonjwa zilizo nje ya mwongozo huo pia Nhif imeweka tabaka la maafisa ambao wao watatakiwa kupewa huduma yoyote bila kujari ipo kwenye mwongozo wa matibabu, mfano Wafanyakazi wa nmb, bot, wabunge, mawaziri and the like.
So hiyo issue ipo hivyo ndg zangu.
 
Hii NHIF wanafanya biashara na wao wanatarajia kutoa gawio kwa serikali kama mashirika mengine kwa hiyo ni lazima wabane dawa za wagonjwa. Kaazi kwelikweli.
 
Kwa kusema haya sitaki kuonekana natetea NHIF. Mimi nitaongelea uelewa wangu juu ya "Insurance Industry" NHIF ni shirika la umma ambalo inafanya biashara ya bima ya afya. Biashara ya bima inafanyikaje? Biashara ya bima ni ya kucheza na probability. Kiasi unachotumia pale unapoumwa kinaweza kikawa zaidi ya kiasi utachochangia. Bima wanakusanya hela kwa kutegemea kwamba only small population ya wachangiaji wataumwa. Ukienda nchi za wenzetu kwanza ile premium inategemea na umri. Ukiwa kijana utalipa hela kidogo sababu probability ya kuumwa ni ndogo. Ukiwa mtu mzima premium inaweza ikawa kubwa sababu probability ya kuumwa inakuwa kubwa. Na jambo lingine wana uwezo wa kukufanyia assesment kabisa kabla hawajakubali kujua risk factors zako.

Sasa hapa kwetu kuna kamchezo kamezuka, unakuta mtu anaenda kukata bima wakati tayari anajijua ana chronic condition, kama kisukari au presha. Kwa wenzetu wakikupima wakakuta tayari una tatizo la presha, basi na premium inaweza ikawa kubwa. Sasa magonjwa haya yanaonekana kuwapata sana watu wazima, lakini huku kwetu hata vijana wa miaka chini ya 40 kwa sababu ya lifestyle. Kampuni ya Insurance ikishakuwa na wagonjwa wengi wa aina hii inakuwa katika risks zaidi ya kupata hasara, yaani asilimia kubwa ya wateja wao wanaumwa mara kwa mara, na magonjwa wanayoumwa yana gharama sana kwenye upande wa dawa. Hapa sasa ndo wanaanza kutengeneza hizo exclusion criteria kuondoa dawa za magonjwa ambayo ni chronic hasa pale idadi ya wagonjwa inapokuwa kubwa sana.

Pia jambo lingine wanachofanya kwenye insurance industry ni kuweka ceiling ya kiasi ambacho wapo tayari kulipa kwenye bili. Na hii ni kwa kampuni nyingi za bima duniani. Hivyo ndiyo strategy ya industry ya bima ilivyo. Ukitaka kujua kwamba bima wanaoperate kwa kuassess risk, we angalia kwanini kwenye "primary agriculture" bima zinakuwa hamna au kama zipo premium ni kubwa sana. Sababu kuu, ni kwamba kilimo kina risk kubwa ya majanga. Mfano mazao yanaweza kuharibika wakati wa kutafuta soko au yakaharibia shambani kutokana na mvua iliyopitiliza au mvua kuwa chini ya wastani. Hivyo ndivyo bima ilivyo. Kwa watu walisomea haya mambo wanaweza kufafanua zaidi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…