Tumejiandaa vipi na Sensa 2022? Njoo tuzungumze

Tumejiandaa vipi na Sensa 2022? Njoo tuzungumze

Tajiri Kichwa

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2017
Posts
9,021
Reaction score
22,016
Kila mmoja anafahamu kuwa tarehe 23 mwezi agosti 2022 kutakua na sensa ya watu na makazi katika nchi yetu. Ni jambo jema maana kwa mujibu wa serikali yetu wanasema inawasaidia wao kutambua wingi Wa watu kwa usawa au mgawanyo wa maendeleo.

Kuna maswali baadhi ya kujiuliza je iyo sensa inatupa taarifa stahiki. Tutazame swala la idadi ya watu. Mujibu tunayosikia idadi ya watu itahesabiwa kupitia maeneo walipolala usiku wa kuamkia tarehe 23 agosti.

Kuna maswali ya kuuliza au kujiuliza vipi wale wanatarajia kusafiri kwenda nje ya nchi hivi karibuni, siku ya sensa itawakuta hawako nchini? Vipi wale walio masomoni karibu mwaka au miaka tunapataje idadi yao.? Je vipi wale wasio na makazi wanaolala barabarani na mitaani? Je, vipi wale madereva ambao hufanya safari zao usiku mfano gari binafsi na gari za mizigo?. Naona kuna kundi kubwa linaenda kukosa haki ya kuhesabiwa.

Je, tumejianda kukusanya idadi tuu au na taarifa muhimu zinginezo, Mfano kufahamu idadi ipi ya watu haijaweza kufikiwa na huduma ya bima.? Je ni watanzania wangapi wametengwa na huduma za kibenki au kifedha? Je ni idadi ipi ya watu waliowekwa nje ya mnyororo wa ajira?

Kwangu sensa naona tunafanya kama ilivyo desturi ya mtu kufanya shughuli ya kumbukumbu kila tarehe fulani inapofika.

Karibu kwa mtazamo au maoni kuhusu sensa. Mfano wewe kwenye dodoso ungependa wakusanye taarifa zipi zaidi.
 
Kwa mujibu wa sensa hii makundi yote ya watu watahesabiwa hadi walio nje ya nchi kama wanafunzi taarifa zao zitapatikana sensa hii inataka kujua sio tu idadi ya watu pia shughuli za uchumi za watu,wenye bima za afya na wasio nazo,wafanyakazi za ndani, wafanyabiashara, machinga, wenye nida na wasio na nida inaenda mbali sana na kutaka jua wenye vifaa au vitu mwananchi anavyo miliki na anavitumia kwa ajili gani, fursa ya ajira zikoje, je mwananchi anatafuta kazi na alitafuta kazi gani kwa muda fulani alipata ama alikosa,mwananchi aliaacha shule ni kwa sababu gani? Ulihama toka mkoa mmoja kwenda nyingine kwa sababu zipi.

Sensa inagusia mambo mengi sana na uchambuzi wa hizo taarifa ndio inawapa serikali dila ya maendeleo na utoaji wa huduma za jamii uwe na uelekeo upi.

Sensa ni muhimu kwa maendeleo ya taifa. Wananchi watoe taarifa sahihi na wajiandae kuhesabiwa.
 
Kuamshana usingizini hiyo ni kipengele kigumu kwangu, labda wangeweka posho ya mahojiano....ila tutajitahidi kujibu kadri tuwezavyo
 
Kwakweli kwangu labda waje saa mbili wakija saa tatu nimefunga mlango na nimepanda kitandani na taa zote nimezima watagonga wabonyee na wakija mchana hawanikuti nipo kazini na watoto kama hiyo siku hawataenda shule ndiyo watakaowapa ushirikiano ambao hawajui chochote!

Tusisumbuane tu
 
Kwa mujibu wa sensa hii makundi yote ya watu watahesabiwa hadi walio nje ya nchi kama wanafunzi taarifa zao zitapatikana sensa hii inataka kujua sio tu idadi ya watu pia shughuli za uchumi za watu,wenye bima za afya na wasio nazo,wafanyakazi za ndani,wafanyabiashara, machinga,wenye nida na wasio na nida inaenda mbali sana na kutaka jua wenye vifaa au vitu mwananchi anavyo miliki na anavitumia kwa ajili gani,fursa ya ajira zikoje,je mwananchi anatafuta kazi na alitafuta kazi gani kwa muda fulani alipata ama alikosa,mwananchi aliaacha shule ni kwa sababu gani? Ulihama toka mkoa mmoja kwenda nyingine kwa sababu zipi.
Sensa inagusia mambo mengi sana na uchambuzi wa hizo taarifa ndio inawapa serikali dila ya maendeleo na utoaji wa huduma za jamii uwe na uelekeo upi.

Sensa ni muhimu kwa maendeleo ya taifa. Wananchi watoe taarifa sahihi na wajiandae kuhesabiwa.

Tutarudi kukumbushana kwa yaliyotajwa hapo kama yataulizwa kwenye dodoso.

Vipi wale ambao itatukuta porini tukikata miti na kuchoma mkaa ambako tunakaa hadi week huko. Huoni siku iyo tutakosa haki yetu.

Je wale madereva wa safari ndefu wanaondoka jioni na kutembea usiku mzima. Wakilala ni kwenye gar watahesabiwa vipi?
 
Back
Top Bottom