Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,540
Kama Taifa, Watanzania tumepoteza uimara na umadhubuti wa kudai kwa nguvu uwajibikaji.
Kama Taifa, tumeruhusu uongozi mbovu kushikilia dhamana ya kuliongoza Taifa.
Tumefanya hilo kwa hiari yetu wenyewe na kama watu tuliologwa au kupagawa, kila miaka mitano tumewachagua watu wale wale miaka nenda rudi, tukiamini kwa dhati ahadi za tunaowakabidhi hatamu za uongozi kuwa watatuongoza kwa ufanisi, uimara na kwa haki na kutulinda kwa ngao imara katika vita dhidi ya umasikini, ujinga, maradhi na uhalifu.
Lakini tumekubaliana na kauli mbiu nyingi kila siku na hata sasa ya kudai Katiba mpya kama kigezo cha kurahisisha safari yetu ya maendeleo na kujenga jamii imara yenye kutii Sheria na kuwajibika.
Lakini tatizo si Katiba, hata kama tukiiangalia kwa Kiti cha Urais na kudai ana madaraka na nguvu nyingi.
Kwani Raisi kazi yake ni nini?
Ni sisi kama Taifa tumeshindwa kuwajibisha viongozi na kuwalazimisha wawe watii wa sheria, wawe makini kwenye kazi zao na kubwa ni dhamana ya kuongoza Taifa katika safari ya kujenga na kulinda Utaifa na Taifa letu.
Majemedari wetu ni legelege, hawana utashi wa kupigana vita kwa niaba yetu, wanadai silaha hazitoshi, na sisi tunakubali haraka haraka bila kufanya Tathmini ya ujemedari wao na tunaafiki eti lazima tununue silaha mpya!
Kuna maana gani kununua silaha mpya kama majemedari wetu hawana moyo au ari ya kuwa mstari wa mbele kutuongoza vitani?
Silaha mpya zitatulinda vipi kama majemedari hawana mipango na mbinu zinazoeleweka na zenye umakini kupigana vita?
Je tumesahau tulipowakubalia walizike Azimio la Arusha na siasa ya Chama Kimoja kwa kudai Ujamaa na Kujitegemea na Chama kimoja villikuwa matatizo ya maendeleo yetu na vilitufanya kuwa masikini?
Mwaka 1992, majemedari waliuzika Ujamaa na Azimio, wakazika siasa za chama kimoja. Azimio jipya la Matumaini la Zanzibar likazaliwa, mfumo wa mpya wa siasa wa vyama vingi ukazaliwa.
(Tukasahau na kujisahau kuwa majemedari walikuwa wale wale!)
Leo hii, miaka 22 baada ya "Katiba" mpya ya 1992, bado tuko palepale na hatua za kupiga maendeleo zimezidi kuwa fupi na zisizo na uwiano!
Umasikini unashamiri, Ujinga umeongezeka, Maradhi hayaishi, uhalifu (ufisadi, uzembe,ufujaji, kutokuwajibika) umekuwa jambo la kawaida na linapewa enzi na mbaya zaidi tumegeuka kwa Taifa tegemezi na lenye matumizi mabaya ya fedha na deni kubwa la kutisha.
Sasa tujiulize, tujisute, tumelilia rasimu mpya na kuweka vipengele vingi vya upendeleo na lengo kuu tunadai Katiba mpya itaondoa kero na kutustawisha kama Taifa!
Swali na wazo langu la Jumamosi hii ni hili: ni kwa uhakika gani Katiba mpya itatubadilisha kama watu tukaamka na kubaini kuwa majemedari wetu hawatufai ?
Tunanunua silaha mpya ya nini ikiwa Jeshi na majemedari ni wale wale ambao ni wazembe, wabinafsi, wavivu, hawana ufanisi na kila siku kutoa visingizio kuficha udhaifu wao au kulinda maslahi yao?
Iweje tuwaamini majemedari wetu ( angalizo- si CCM pekee, CUF, Chadema na kadhalika) kweli wako tayari safari hii kujitoa mhanga kutuongoza vitani na kulilinda Taifa letu?
Je wakishindwa kuwajibika kwa dhati, tuunde tume au kamati kuchunguza na kuandika Katiba mpya, au kanuni na Sheria mpya?
Jihoji nafsi yako upigapo kura yako: iwe ni kutaka Katiba mpya, Tamisemi 2014 au Uchaguzi Mkuu 2015!
Kama Taifa, tumeruhusu uongozi mbovu kushikilia dhamana ya kuliongoza Taifa.
Tumefanya hilo kwa hiari yetu wenyewe na kama watu tuliologwa au kupagawa, kila miaka mitano tumewachagua watu wale wale miaka nenda rudi, tukiamini kwa dhati ahadi za tunaowakabidhi hatamu za uongozi kuwa watatuongoza kwa ufanisi, uimara na kwa haki na kutulinda kwa ngao imara katika vita dhidi ya umasikini, ujinga, maradhi na uhalifu.
Lakini tumekubaliana na kauli mbiu nyingi kila siku na hata sasa ya kudai Katiba mpya kama kigezo cha kurahisisha safari yetu ya maendeleo na kujenga jamii imara yenye kutii Sheria na kuwajibika.
Lakini tatizo si Katiba, hata kama tukiiangalia kwa Kiti cha Urais na kudai ana madaraka na nguvu nyingi.
Kwani Raisi kazi yake ni nini?
Ni sisi kama Taifa tumeshindwa kuwajibisha viongozi na kuwalazimisha wawe watii wa sheria, wawe makini kwenye kazi zao na kubwa ni dhamana ya kuongoza Taifa katika safari ya kujenga na kulinda Utaifa na Taifa letu.
Majemedari wetu ni legelege, hawana utashi wa kupigana vita kwa niaba yetu, wanadai silaha hazitoshi, na sisi tunakubali haraka haraka bila kufanya Tathmini ya ujemedari wao na tunaafiki eti lazima tununue silaha mpya!
Kuna maana gani kununua silaha mpya kama majemedari wetu hawana moyo au ari ya kuwa mstari wa mbele kutuongoza vitani?
Silaha mpya zitatulinda vipi kama majemedari hawana mipango na mbinu zinazoeleweka na zenye umakini kupigana vita?
Je tumesahau tulipowakubalia walizike Azimio la Arusha na siasa ya Chama Kimoja kwa kudai Ujamaa na Kujitegemea na Chama kimoja villikuwa matatizo ya maendeleo yetu na vilitufanya kuwa masikini?
Mwaka 1992, majemedari waliuzika Ujamaa na Azimio, wakazika siasa za chama kimoja. Azimio jipya la Matumaini la Zanzibar likazaliwa, mfumo wa mpya wa siasa wa vyama vingi ukazaliwa.
(Tukasahau na kujisahau kuwa majemedari walikuwa wale wale!)
Leo hii, miaka 22 baada ya "Katiba" mpya ya 1992, bado tuko palepale na hatua za kupiga maendeleo zimezidi kuwa fupi na zisizo na uwiano!
Umasikini unashamiri, Ujinga umeongezeka, Maradhi hayaishi, uhalifu (ufisadi, uzembe,ufujaji, kutokuwajibika) umekuwa jambo la kawaida na linapewa enzi na mbaya zaidi tumegeuka kwa Taifa tegemezi na lenye matumizi mabaya ya fedha na deni kubwa la kutisha.
Sasa tujiulize, tujisute, tumelilia rasimu mpya na kuweka vipengele vingi vya upendeleo na lengo kuu tunadai Katiba mpya itaondoa kero na kutustawisha kama Taifa!
Swali na wazo langu la Jumamosi hii ni hili: ni kwa uhakika gani Katiba mpya itatubadilisha kama watu tukaamka na kubaini kuwa majemedari wetu hawatufai ?
Tunanunua silaha mpya ya nini ikiwa Jeshi na majemedari ni wale wale ambao ni wazembe, wabinafsi, wavivu, hawana ufanisi na kila siku kutoa visingizio kuficha udhaifu wao au kulinda maslahi yao?
Iweje tuwaamini majemedari wetu ( angalizo- si CCM pekee, CUF, Chadema na kadhalika) kweli wako tayari safari hii kujitoa mhanga kutuongoza vitani na kulilinda Taifa letu?
Je wakishindwa kuwajibika kwa dhati, tuunde tume au kamati kuchunguza na kuandika Katiba mpya, au kanuni na Sheria mpya?
Jihoji nafsi yako upigapo kura yako: iwe ni kutaka Katiba mpya, Tamisemi 2014 au Uchaguzi Mkuu 2015!