Tumeshindwa kumwelimisha kijana wa Kitanzania?

Tumeshindwa kumwelimisha kijana wa Kitanzania?

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
[h=2]
icon1.png
Re: NDALICHAKO: kitu cha ZOMBI[/h]

quote_icon.png
By asigwa
Haya ndio watoto wenu wamejaza kwenye karatasi za kujibia mtihani wa kidato cha nne....

Tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele....

attachment.php






Msituko wa kufeli kwa kiwango kinachoshitua kwa vijana wetu, watoto wetu, katika mitihani ya kidato cha nne, ndio kwanza unaanza kueleweka.

Mshituko huu wa zaidi ya 60% ya vijana WOTE, kushindwa mitihani kunakupa mzazi jibu moja tu.

SERIKALI YETU IMESHINDWA KUMWELIMISHA KIJANA WA KITANZANIA.

Hapa hakuna sababu ya kuunda tume wala uchunguzi wakati Wizara ya Elimu. Wizara inayotakiwa kuandaa wataalamu wakesho ikiwa imeshindwa katika majukumu yake ya kimsingi.

Kwa matokeo yaliyoonekana mwaka huu, kuwepo kwa Wizara au kutokuwepo ni sawa tu.

Mbaya zaidi ni hiyo picha ya kiongozi wa juu katika Wizara mama Ndalichako kuonyesha jinsi wanafunzi wanavyochora vibonzo badala ya kujibu maswali ya mitihani.

Ni dhahiri kwamba mwanafunzi hakuandika jibu la mtihani kwa vile HAKUFUNDISHWA namna ya kujibu mitihani.

Lawama ni nyingi na ziko kila mahali lakini huu uozo uko ndani ya Wizara yenyewe ya Elimu.
Kiujumla tatizo hili si tukio la kushtukiza, matatizo ya sekta ya elimu yamejikusanya kwa miaka mingi, na sasa tunaona matokeo yake.
baadhi tu ya matatizo:
  • Fedha kidogo zinazo tengwa kwa ajili ya elimu kiujumla
  • walimu wachache waliopo kukosa motisha kufanya kazi
  • kuongezeka sana kwa wanafunzi amabako hakuwiani na huduma ya elimu kwa wanafunzi hao
Kwa ujumla sekta ya elimu haina mipango endelevu, na ya miaka mingi kutatua matatizo ya sekta hii.

Kuliko kuundiwa tume, Wizara yenyewe ikae chini, ijena na mapendekezo ya kuondoa aibu hii ambayo ni upotevu mkubwa wa resource inayohitajika huko mbeke ya safari- resource ya vijana wasomi na wataalam wa baadaye.

Najiuliza, wahandisi wa baadaye kutengeneza barabara watatoka wapi?
Madaktari je?
Wachumi tunao wahitaji?
Waalimu na hata askari wenye utaalam, polisi wenye weledi?

Tusichezee resource hii muhimu, serikali inaombwa kuzingatia kurekebisha tatizo hili.
 
mkuu nakuunga mkono sana tu mambo ya tume hayasaidii kitu ni kupoteza muda mi naomba waziri aachie ngazi ampishe mwingine kwa kuanzia alafu hatua ya pili serikali iwaombe radhi walimu bila kupindisha hilo litasaidia tatu suala ya maslahi ya mwalimu yashukughulikiwe haraka wakati mkakati wa muda mrefu unaandaliwa mfano kubadili mfumo wa elimu na elimu tanzania kutoka elimu ya vyeti mpaka ufahamu. hapo itasaidia.
 
Kuliko kuundiwa tume, Wizara yenyewe ikae chini, ijena na mapendekezo ya kuondoa aibu hii ambayo ni upotevu mkubwa wa resource inayohitajika huko mbeke ya safari- resource ya vijana wasomi na wataalam wa baadaye.

Najiuliza, wahandisi wa baadaye kutengeneza barabara watatoka wapi?
Madaktari je?
Wachumi tunao wahitaji?
Waalimu na hata askari wenye utaalam, polisi wenye weledi?

Tusichezee resource hii muhimu, serikali inaombwa kuzingatia kurekebisha tatizo hili.

Kwanza kabisa, hatua ya kwanza ni ya kujiuzulu kwa waziri wa elimu na naibu wake. Wameshaonyesha kwa kiwango kikubwa sana kushindwa kuimudu wizara hii na hata kama mapendekezo au maazimio mazuri yatafikiwa hawataweza kuyasimamia yakatokea, wamepwaya.

Pili, Spika awatake radhi watanzania kwa kupitisha/kuhalalisha mtaala batili bungeni na hivyo kuzima mjadala wa mabadiliko/uboreshaji wa mtaala bungeni. Hii itatoa nafasi ya mfumo wa elimu yetu kuangaliwa kwa upya ili uweze kuleta mabadiliko kwa wanaoipata.

Serikali ipange na kuamua kulitatua tatizo la mfumo wa elimu, sio tu kuanzia kwenye matokeo bali maeneo yote yanayoizunguka wizara hii ikiwemo maslahi na mazingira ya waalimu na mazingira ya kusomea wanafunzi kwa ujumla.

Madhara ya tatizo la mfumo wa elimu hauishii tu kwenye kukosa wataalam, japo naona sasa hivi tunaimport CIA/FBI sasa sijui baadae tutaimport wataalam kwenye kila idara? Hawa watu waliofeli watakapokuja uraiani wakakutana na hizi siasa za nani achinje sijui ukristo mara uislam, unategemea nchi itakua kwenye hali gani? Hatutaweza kukaa kujadili hali ya maendeleo ya nchi wakati hakuna amani.

Elimu ni nguzo muhimu sana katika taifa lolote lile kujikwamua kimaendeleo.
 
Kujiuzulu kwa Waziri inaweza kuwa si suluhisho, na pengine angebaki pale pale kusahihisha makosa ambayo ni dhahiri yametokea
 
Kujiuzulu kwa Waziri inaweza kuwa si suluhisho, na pengine angebaki pale pale kusahihisha makosa ambayo ni dhahiri yametokea

Kila kiongozi wa CCM huwa anataka kubaki hapo hapo kurekebisha makosa. Umefika sasa wakati wa viongozi kukubali kuwajibika kwa kujiuzulu ili kuacha ujumbe kwa atakayekalia kiti chake kuwa ukifanya mchezo umekwenda. Hivi unategemeaje mtu aliyepewa uwaziri kwa kuwa ni swahiba wa mkulu eti elete mabadiliko ya kweli??

Watanzania tusiendelee kujidanganya kuwa chini ya utawala wa CCM kuna siku elimu itaboreshwa. Suluhisho ni kuikataa CCM na kuwapa nafasi watu wengine kutuongoza. Its time for Change
 
Back
Top Bottom