Tumeshindwa kuumiliki ulimwengu wetu kwa kuutamaani ulimwengu wa Hadithi

Tumeshindwa kuumiliki ulimwengu wetu kwa kuutamaani ulimwengu wa Hadithi

third eye chakra

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2023
Posts
713
Reaction score
1,745
🌳TUMESHINDWA KUUMILIKI ULIMWENGU WETU KWA KUUTAMANI ULIMWENGU WA HADITHI.🌳

Ulimwengu wa kweli umetengenezwa katika hadithi isiyo furahisha sana, unaonekana ni ulimwengu ulio jaa mateso ya kila namna, kisha Ulimwengu wa NADHARIA ndiyo umejaa raha za kila namna na umeitwa ulimwengu mpya (PARADISO au PEPONI)

Ulimwengu wa nadharia ndiyo umejenga watu watumwa KIIMANI, kwakua wanatamanishwa kitu ambacho mtamanishaji hajawahi kukiona zaidi ya simulizi katika simulizi zenye sanaa ya ULAGHAI msimuliaji wa Mwanzo katika swali la tukifa tunaenda wapi?

Ulimwengu mpya ni mtazamo ulio jiamini, mtazamo ulio wajaza watu imani kupita kiasi hata kufikia hatua ya kuhitaji Ulimwengu wa kweli ufike mwisho, kwakua ndani yao Kuna matumaini kupita kiasi matumaini ya udanganyifu wa ulimwengu uliopakwa rangi

Kilicho tushinda katika Ulimwengu huu wa kweli ni baada ya kutofungua kurasa zake zote, kwakua tangia tungali wadogo tulifunguliwa kurasa za Ulimwengu mpya wa nadharia na Wale Wenye Kutunga Hadithi za Ulimwengu Huo, kisha Wakatupa Ukomo wa Kurasa za Fikra ili tusisome zaidi ya Kurasa walizitufunilia.

Ulimwengu wa kweli hauwezi kuwa tulivu ikiwa tayari uhuru wake tumeupa Ulimwengu mpya wa hadithi, Ulimwengu ambao tayari umefunga sehemu yetu ya mawazo.

Huu msemo wa "SISI SIO WA ULIMWENGU HUU" umetunyima Akili ya kushindwa kuimiliki dunia kimantiki na kutupa umiliki wa giza wa imani, Lakini Umiliki wa Dunia Umebaki Mikononi mwa Wale Watunzi wa Ulimwengu mpya Wa Nadharia Ambao hata wao hawajawahi kuufikia. tunahitaji mtazamo mzuri kuhusu Ulimwengu wa Kweli, tunahitaji mwanzo ambao unathibitisha kuwapo kwetu si makosa na hata kufa kwetu si dhambi.

Lazima tupate mtazamo wa kimantiki ili tuweze kuunda hatima yetu nje kabisa ya Imani ila ndani kabisa ya ulimwengu wa kweli usio tugawa. Tunahitaji utambuzi utakao tutoa katika Akili bandia za Imani na Kisha Tukaishi katika Msingi Imara wa Asili yetu.

Tunahitaji kumiliki madhaifu/udhaifu wetu na kufanya vyema bila kuusingizia ulimwengu na Shetani. Kuufanya Ulimwengu wa kweli kuwa ni dhaifu na mchafu kuliko Ulimwengu mpya wa hadithi ni kuonesha jinsi ambavyo TUNA IKANDAMIZA ASILI YETU HALISI katika asili ya Imani.
🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Haina mbaya kuwa na kitu bora cha kufikirika tunachokitamani na kukiendea.

Ni vizuri kuwa na maono mema, sema tunahitaji tu kuwa na ujuzi wa kwamba: huo ulimwengu mpya tutauleteleza sie wenyewe. Yaani tupo tunaifanya kazi ya kuijenga pepo/paradiso yetu kwa shughuli zetu za kila siku, mafikirio yetu na kila tunachofanya. Eaaaaasy.

Nasema hivyo kwa sababu hata kwenye mahusiano ni hivyohivyo.
1. Ambao hawajawahi kusimuliwa hadithi za maisha mema kifamilia, uwezekano mkubwa kuteseka kifamilia/ndoa. Hawana ndoto wala 'vision' ya mambo mema katika ubora wake 'ideal family, marriage'
2. Waliosoma vitabu na kusimuliwa hadithi/series za maisha mazuri ya ndoa na raha zake wana machaguo mawili;
A. Kuamini maisha hayo yapo mahala pengine na inatokea tu kwa hivyo wanabaki kuteseka kuyatafuta au kuyasubiri, hawafaidi sasa hivi na baadaye inazidi kuwa mbaya.
B. Kuamini kwamba ni wao ndio wana jukumu la kuyatengeneza maisha ya ndoa na familia wanazosimuliwa kwenye hadithi tamu, hawa wana uwezekano mkubwa sana wa kufaudu saa hii na baadaye pia.
 
Mwanadamu amepewa upeo ili afikiri so umefikiri vema. Kwakua kila mtu anahaki yakufikiri basi yampasa kufikiri ili kupata majibu ya maswali yake ajiulizayo.
Swali ni je kama haupo ulimwengu mpya na huu tulio nao ndo pekee ukifa basi nin hatima ya ulimwengu huu kwa jinsi unavyo jiendesha sasa?
Mambo yamebadilika kwa kiasi kikubwa hata watu kuivuka mipaka ya asili je unataka kusema mwisho wa haya yote ninini?
Huu ndo ulimwengu original na hakuna mwingine katika fikra zako je twaweza kuubadilisha na kuuunda upya ?
Je unaamini miujiza na kama huamini je unaamini kiini macho na kama huamin je haya yote yanasababishwa nanin had kutokea?
Nataka kujua tuamin hakuna ulimwengu mpya so tuishi tukila raha za maisha maana kufa mara moja je kuna haja gan ya kutenda wema dunian kisha ufe stori yako ifutwe?
Kuna haja gan ya kujali wengine wakati kufa mara moja?
Ukijibu maswali haya vema naweza nkakuunga mkono

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asili ya binadamu tunapenda kufarijiwa,
Tunapenda kupokea habari za kuliwaza,

Tumekuwa wavivu wa kufikiri

Inafikia hatua mtu anakana watu anaowaona akiungana na mungu asiyemuona.
Yote kwa yote kila mtu ana haki ya kuamini anachoamini.
 
Kuna watu wanashindwa kabisa kuishi maisha yao halisi kwaajili ya maisha ya kusadikika wakifa

Just imagine mtu anakatili maisha yake anavaa bomu kijiua akiamini atakwenda kula bata la milele akifa..... 😂😂😂
 
Back
Top Bottom