Wakuu poleni kwa majukumu ya maisha. Naombeni msaada wenu Wa kitabibu...
Kuna mtu nimemueleza matatizo ya maumivu niliyo nayo mwilini ndo akaniagiza nikatafute mafuta ya black seeds oil kwamba takuwa tiba ya maumivu niliyo nayo
Kifupi ni kwamba nasikia maumivu kwenye tumbo la chini ya kitovu na mgongo unauma kwenye kiuno yakiambatana na kibofu cha mkojo kuuma pale mkojo unapokusanyika kidogo. Kingine ni maumivu ya shingo na mabega. Nimehudhuria hospital sana tena hospital kubwa na vipimo vyote nimepata lakini hakuna ugonjwa ulioonekana.
Nimepima hadi figo ziko sawa. Sasa ndo nikaagiziwa nikanunue hayo mafuta ya Black seeds oil.manake nimeambiwa yanatibu magonjwa zaidi ya ishirini ikiwemo king a dhidi ya ugonjwa Wa cancer.
Naombeni mwenye ujuzi na haya mafuta na kama alishawahi kuyatumia yakamsaidia; anipe mwongozo please. Asanteni. Karibuni Doctors Wa hili jukwaa.
Sent using
Jamii Forums mobile app