Ni vizuri ukaongelea jambo ambalo unalitambua,
Unajua kundi la Wateule lilianza mwaka gani? Je ilikua kabla au baada ya Solo Thang kuzinguana na Kikosi?
Solo Thang alitekwa na Kikosi mwaka 2001 Pool Side - Kilimanjaro Hotel? Unajua ulikua ni uzinduzi wa album ya nani?
Mfalme wa Hip Hop una maanisha Afand Sele? Maana ndie peke yake aliyevishwa crown hiyo na shindano hilo halijawahi fanyika tena.
Ukiongela miaka ya 90' waliokua wanatamba haimaanishi ndio walikua wakali wa kughani, so kuna tofauti ya kutamba ( kuvuma) na kuwa mkali wa kuandika mistari, Saleh Jabri alitamba mwanzoni mwa miaka ya 90' je nae alikua mkali?
Ukiongela waliotamba miaka ya 90's -2000's wako wengi sana, ila kwa upande wa kuandika mistari yenye ujazo na kunata na mdundo , mitindo huru(free style) Hashim Dogo alikua anakimbiza.
Sikiliza jingle ya Radio One kipindi cha Dj show, sina uhakika kama bado kipo, utamsikia jamaa
Pia kumbuka miaka hiyo Radio One walikua wanatoa dakika 15 tu kwa nyimbo za bongo flava, hivyo wakali wengi tuliwajua kwa kusikliza mixtapa kitaani.
We jamaa hujui lolote maana hata nashindwa nianze wapi kukujibu maana ulivyoandika vyote uongo. ..kwa kuanza tu.....
Solo hakutekwa kilimanjaro pool side, that time alikuwa anafanya kazi times fm na yeye ndio alikuwa mc wa show ya times pale lang'ata kila jpili....alitekwa lang'ata pale kino makaburini, wakampakia kwenye pick up, na alijiokoa kwa kuruka kwenye gari. ..na msaada alipata kwa wamasai.
Kama una kumbukumbu utajua p funk aliwakusanya wapi wateule baada ya kufanya kitu kama star search.
Unasema hashimu alikuwa anakimbiza miaka ya 2000. ..., nitajie matamasha makubwa matano aliyowahi kupanda Hashim, hiyo jingle ya dj show we unaona ndio kipimo cha ukali? Hata solo alikuwa na jingle kwenye kipindi cha ijumaa cha abuu sadiq. ...hata papi kocha alikuwa na jingle na ilibamba kinoma.
We sidhani kama ulikuwa unafuatilia hiphop. ....radio one walikuwa na kipindi kila jpili cha bongo flavour tena kilikuwa chini ya mike muhagama. ...na that time Hashim alikuwa wa kawaida tu. ..
Kwa kifupi nataka nikwambie, Hashim hana hadhi ya kuitwa mfalme. ....maana kama ni freestyle hawezi kumgusa mangwear. ....freestyle za wasanii wengi kipindi kile hazikuwa zinamaliza dk 2 bila kuchanganya na mistari aliyotunga nyumbani (kumbuka that time kuingia studio ilikuwa issue so wengi walikuwa na mistari mingi kichwani).
Na kwa taharifa yako solo hajawahi zinguana na kikosi. .....ni misunderstanding tu za kikosi kudhani kuwa solo kawadiss.....ila kikubwa ni uwezo wa solo kipindi hicho. .....solo alivyoibuka hata Hashim alikuwa haingizi mguu kwa moto wa solo.