Johnson Alex Otieno
Senior Member
- Mar 14, 2013
- 172
- 57
Hodi wana jukwaa.
Katika kipindi hiki cha harakati za wagombea na vyama vyao kuendelea kunadi kampeni zao ili kupata uhalali wa kuunda serikali zikiendelea bado najikuta nina maswali mengi ya kujiuliza.
Moja ya maswali yangu ni je serikali tutakayoipa mamlaka ya kuongoza nchi na wananchi itatulinda sisi wananchi na Mali zetu?
Msingi wa swali langu ni matukio tuliyoyasikia kupitia vyombo vyetu vya habari katika kipindi cha miaka mitano, katika kipindi hiki tumeshuhudia mengi haya ni baadhi tu
1. Kutekwa kwa watu muhimu na maarufu nchini, katika kipindi cha miaka mitano tumeshuhudia watu wakitekwa na kufichwa na watu wasiojulikana, mfano wasanii, wafanya biashara na waandishi wa habari.
Je serikali tutakayoiweka madarakani itatulinda dhidi ya uhalifu huu wa ubinadamu na Mali zao?
2. Mauaji ya hovyo hovyo, kwa miaka mitano tumeona ndg zetu na watanzania wenzetu wakiumizwa na watu wasiojulikana, serikali ya awamu ya tano ilishindwa kuwabaini hawa wasiojulikana, je tutoe fursa kwa walioshindwa kuwabaini watu wasiojulikana ili hali moja ya wajibu wa serikali ni kutulinda?
Naomba mnieleze nimpe nani kura yangu kwa maana napata wasiwasi wa kesho ya watanzania na Mali zao.
3. Je hizi kesi za uhujumu uchumi nani atazitatua kwa sheria na haki? Kwa miaka mitano nimesikia watanzania wakishitakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi, kwa mtazamo wangu nataka serikali tutakayoipa mamlaka iheshinu misingi ya kisheria na isiingilie uhuru wa nguzo zingine za nchi, serikali inayoamini yenyewe ndio nguo iliyojichimbia zaidi haina uhalali wa kuendelea kuongoza watanzania.
4. Maagizo kutoka juu, nataka tumchague mtu atakayekomesha hili neno, ndg zetu wanasota magerezani na vituo vya Polisi kwa kauli hii, aidha haki zao zinakanyangwa kwa maigizo kutoka juu, naomba kujua ni nani kati ya wagombea tulionao atakayekomesha maigizo kutoka juu?
5. Ni mgombea gani atakaye ruhusu uhuru wa waandishi wa habari na vyombo vyao,? Mathalani bunge letu tukufu kwa sasa wananchi hatuna fursa ya kujua kinachoendelea kwa kadri ya maagizo ya wachache, niambie ni nani nimpe kura ili arejeshe bunge mbashara na uhuru wa waandishi wa habari na vyombo vyao?
6. Niambieni nani ataongeza mshahara na kuamsha Ari kwa wafanyakazi wa umma, kwa miaka mitano woga na kujipendekeza vimetamalaki, nani ataweza kuhamasisha wafanyakazi hawa wafanye kazi kwa majibu wa taaluma zao?
7. Ni nani atatoa fursa za ajira kwa vijana bila kujali itikadi za vyama, kwa miaka mitano vijana wanalia na wasio na majina makubwa ndo hawana kabisa matumaini ya kesho zao.
Nambieni nani atarejesha tumaini kwa vijana wanyonge?
8. Naomba mnielekeze na nielewe Hivi kweli yupo mtu atakayeleta mabadiliko ya tozo kwa wafugaji na wakulima? Hivi yupo mtu atakayeregeza kodi kwa wafanyabiashara? Mtu huyo naomba kumjua ili nikampe kura yangu October 28.
Niambie ni nani atajibu na kuondoa mambo haya,?
Nataka kiongozi atakayewajua na kuwashughulikia watu wasiojulikana, awalete kwa wananchi na mahakama zetu ziwatendeee kwa kadri ya sheria zetu.
Nataka kiongozi atakayetambua kwamba mamlaka zote zinatoka kwa wananchi na akili hilo kwa maneno na matendo yake.
Bado na ngoja msaada kwa wajuzi wa siasa wanieleze kura yangu nimpe nani.
Katika kipindi hiki cha harakati za wagombea na vyama vyao kuendelea kunadi kampeni zao ili kupata uhalali wa kuunda serikali zikiendelea bado najikuta nina maswali mengi ya kujiuliza.
Moja ya maswali yangu ni je serikali tutakayoipa mamlaka ya kuongoza nchi na wananchi itatulinda sisi wananchi na Mali zetu?
Msingi wa swali langu ni matukio tuliyoyasikia kupitia vyombo vyetu vya habari katika kipindi cha miaka mitano, katika kipindi hiki tumeshuhudia mengi haya ni baadhi tu
1. Kutekwa kwa watu muhimu na maarufu nchini, katika kipindi cha miaka mitano tumeshuhudia watu wakitekwa na kufichwa na watu wasiojulikana, mfano wasanii, wafanya biashara na waandishi wa habari.
Je serikali tutakayoiweka madarakani itatulinda dhidi ya uhalifu huu wa ubinadamu na Mali zao?
2. Mauaji ya hovyo hovyo, kwa miaka mitano tumeona ndg zetu na watanzania wenzetu wakiumizwa na watu wasiojulikana, serikali ya awamu ya tano ilishindwa kuwabaini hawa wasiojulikana, je tutoe fursa kwa walioshindwa kuwabaini watu wasiojulikana ili hali moja ya wajibu wa serikali ni kutulinda?
Naomba mnieleze nimpe nani kura yangu kwa maana napata wasiwasi wa kesho ya watanzania na Mali zao.
3. Je hizi kesi za uhujumu uchumi nani atazitatua kwa sheria na haki? Kwa miaka mitano nimesikia watanzania wakishitakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi, kwa mtazamo wangu nataka serikali tutakayoipa mamlaka iheshinu misingi ya kisheria na isiingilie uhuru wa nguzo zingine za nchi, serikali inayoamini yenyewe ndio nguo iliyojichimbia zaidi haina uhalali wa kuendelea kuongoza watanzania.
4. Maagizo kutoka juu, nataka tumchague mtu atakayekomesha hili neno, ndg zetu wanasota magerezani na vituo vya Polisi kwa kauli hii, aidha haki zao zinakanyangwa kwa maigizo kutoka juu, naomba kujua ni nani kati ya wagombea tulionao atakayekomesha maigizo kutoka juu?
5. Ni mgombea gani atakaye ruhusu uhuru wa waandishi wa habari na vyombo vyao,? Mathalani bunge letu tukufu kwa sasa wananchi hatuna fursa ya kujua kinachoendelea kwa kadri ya maagizo ya wachache, niambie ni nani nimpe kura ili arejeshe bunge mbashara na uhuru wa waandishi wa habari na vyombo vyao?
6. Niambieni nani ataongeza mshahara na kuamsha Ari kwa wafanyakazi wa umma, kwa miaka mitano woga na kujipendekeza vimetamalaki, nani ataweza kuhamasisha wafanyakazi hawa wafanye kazi kwa majibu wa taaluma zao?
7. Ni nani atatoa fursa za ajira kwa vijana bila kujali itikadi za vyama, kwa miaka mitano vijana wanalia na wasio na majina makubwa ndo hawana kabisa matumaini ya kesho zao.
Nambieni nani atarejesha tumaini kwa vijana wanyonge?
8. Naomba mnielekeze na nielewe Hivi kweli yupo mtu atakayeleta mabadiliko ya tozo kwa wafugaji na wakulima? Hivi yupo mtu atakayeregeza kodi kwa wafanyabiashara? Mtu huyo naomba kumjua ili nikampe kura yangu October 28.
Niambie ni nani atajibu na kuondoa mambo haya,?
Nataka kiongozi atakayewajua na kuwashughulikia watu wasiojulikana, awalete kwa wananchi na mahakama zetu ziwatendeee kwa kadri ya sheria zetu.
Nataka kiongozi atakayetambua kwamba mamlaka zote zinatoka kwa wananchi na akili hilo kwa maneno na matendo yake.
Bado na ngoja msaada kwa wajuzi wa siasa wanieleze kura yangu nimpe nani.