Tumpe Mkude uhuru wake

Albinoomweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2016
Posts
3,433
Reaction score
8,585


Anaandika @exaud_msaka_habari

Kiukweli inawezekana Mkude ana mambo yake, ila baadhi ya sisi wanahabari na sisi tuna mambo yetu makubwa sana

Leo kuna watu wamenitumia Vitu DM kuwa sjui mkude kafuta picha alizovaa jezi za Simba zote nikasema sawa, Nikaona watu wameanza kupost tena watu naowaheshimu kabisa nikasema hebu ngoja nikaone

Naingia kwenye Page yake nakuta kafuta mpaka picha za mtoto wake na picha zake nyingine zote hadi aliyompost Kahata na hakuwa amevaa jezi kafuta

Cha ajabu ameacha Picha yake ya Profile kavaa zake jezi ya simba na hatujaiona, Ameacha utambulisho wake BIO kuwa yupo Simba na Taifa Stars na hatujaona hiyo

NIMEJIULIZA YAFUATAYO

1. Siku hizi mchezaji kufuta picha yake instagram ni Habari?

2. Kwanini story yetu haijamalizia kuwa ameacha picha ya Profile na BIO yake vile vile (lengo letu nini)

Alafu kesho tunakaa kwenye Redio tunasema wachezaji wazawa hawajitumi, hawana adabu na maneno kibao, wakati tunamzushia na kumchongea hatuoni uzawa wake? Wakati mwingine mtu unaona aibu kusema ni Mwanahabari yani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…