Wick
JF-Expert Member
- Dec 19, 2012
- 8,313
- 12,170
Wengi wetu tulikuwa tunamchukulia Kiranga kama mtu asiyependa dini lakini kupitia mjadala aliourudisha juzi Deadbody na badae mods wakafanya yao kuunga na thread ya RGforever nimeweza kuelewa kumbe mkuu Kiranga ule mtazamo wake juu ya dini upo upande gani. Kama alivosema yeye ni libertan basi nampongezi kuuona mwanga-nusu ingawa nasikitika hajaweza kujua Mungu anayeona ni blasiphemy yawezekana akawa anamuona katika views/mtazamo tofauti.
Nachokushauri mkuu Kiranga pitia na mada ya theism katika muda wako uweze jua au tuweze eleweshana huyu Mungu katika view ingine isiyohusisha sadaka😉. Mimi ni Muumini katika mfumo wa Deism sababu niiliona/nilifatilia mantiki yake. statement yako imenifikirisha sana na tukitumia concept ya logical reassoning nachelea sema (ingawa siruhusiwi hukumu), Kiranga umeutumia ubongo wako vizuri; you gotta seat in Heaven.
- wick
Mods msihamishe, huu sio uzi wa dini shubaaamit!!!!...
Nachokushauri mkuu Kiranga pitia na mada ya theism katika muda wako uweze jua au tuweze eleweshana huyu Mungu katika view ingine isiyohusisha sadaka😉. Mimi ni Muumini katika mfumo wa Deism sababu niiliona/nilifatilia mantiki yake. statement yako imenifikirisha sana na tukitumia concept ya logical reassoning nachelea sema (ingawa siruhusiwi hukumu), Kiranga umeutumia ubongo wako vizuri; you gotta seat in Heaven.
Mimi ni libertarian.
Napenda uhuru. Watu wawe huru. Kuishi huru. Kufanya biashara huru. Kuamini huru.
Hata mambo yanayosemwa ni ya dini za kishenzi, au za Mungu ambaye hayupo, yanaweza kuwa na maana sana. Mambo ya dini yamejaa allegory, mythology na busara nyingi mahali pengine. Hata kama Mungu hayupo naweza kuelewa kwa nini watu wanahitaji dini. Hili halinifanyi niseme Mungu yupo.
Mathalani. Kuna dini nyingi sana za asili, hata huku Africa tulikoitwa bara la giza, zenye kanuni nyingi nzuri za kutoua wanyama bila sababu, kutokata miti. Nitatoa mbili hizo tu kama mfano. Sasa Waafrika wamefanya haya mambo kwa miaka na miaka, maelfu kwa maelfu. Mtu anayechukulia dini literary atasema hawa watu washenzi. Wanaabudu miti na wanyama.
Lakini kuna upande wa pili wa uchambuzi wa dini kama hizi. Mtu anaweza kusema dini za kuabudu miti na kukataza usikatwe ovyo zimesaidia jk maintain ecological balance na kuhifadhi mazingira. Siku hizi tumeziacha na hii ni moja ya sababu ukataji miti holela umeongezeka na mvua zinaweza kukosekana baadhi ya maeneo. Uuaji holela wa wanyama umeharibu ecological cycle. Watu wanasoma sayansi wanaona hatari za pool of species kuwa reduced, endangered species kuongezeka, au hata unnatural imbalance ya mating population katika wanyama fulani. Mambo haya haya yakisemwa na wazungu/wasomi tunasikliza na kusema yana maana, lakini tukimkuta babu anakataa mti wake usikatwe tunasema mshenzi anaabudu mti.
Kwa hiyo mimi natetea uhuru wa watu kuabudu. Lakini pia, uhuru wa kuabudu kwa kiasi kikubwa ni kitu cha faragha. Ukiabudu kwako, kanisani kwako, msikitini kwako sawa. Ukianzisha mjadala JF kujadili uwepo wa Mungu, halafu ukaniambia mti wa Mbuyu ni Mungu mjuzi wa yote na mwenye uwezo wote na upendo wote, nitakupinga sana.
Kwa maana utakuwa umeshaingilia dini yangu ya kutafuta ukweli kwa uchunguzi.
Kwa hiyo mtu akisema leo Tanzania imepiga marufuku wanaoabudu miti, nitapinga habari hiyo na kusema hawa watu wana haki ya kikatiba Tanzania na pia kimataifa wanatetewa na Universal Declaration of Human Rights iliyopitishwa December 10 1948 kama sikosei, na Tanzania tumetia sahihi kulikubali Azimio hili zuri sana.
Nitaitetea imani hii. Uhuru wa kuabudu si kitu cha kuchezea.
Lakini mtu wa imani hii akija hapa kujadili na kusema mti wa kwao ni Mungu, nitampinga vikali sana kwa facts.
- wick
Mods msihamishe, huu sio uzi wa dini shubaaamit!!!!...