Tuna mtoto wa miezi saba, mke wangu mjamzito. Ushauri pliiiz!

Imethibitika kitaalam mtoto anaweza endelea kunyonya mpaka week chache kabla mamake hajazaa
Cha muhim ni usafi wenu mnapokutana muoge kabla kamjashika watoto
 
Duh kumbe inawezekana kuendelea kunyonyesha wakati mama ana ujauzito :thumbup:
 

Watoto wanaokua namna hii wana raha yake kuliko waliopishana sana
 

Good ideal nathani mkuuu atafuata ushauri wakoo…
 
mangatara
Kumbe hakuna shida kama mtoto bado mdogo, ngoja na mimi niongeze mwingine ili tupumzike mapema,maana wa kwangu ana miezi kumi.
 
Last edited by a moderator:
AAAhhhhh mbona hiyo kawaida saaaana....kuna mchizi mkewe kapata ujauzito wakati ana mtoto wa miezi mmoja na nusu halafu kajifungua mapacha......wewe vipi..
 
kwa kweli Mkuu Ndaba hata mimi nilikuonea huruma sana,msalimie Nas
 
Kumbe hakuna shida kama mtoto bado mdogo,ngoja na mimi niongeze mwingine ili tupumzike mapema,maana wa kwangu ana miezi kumi

Wilddog;
Umechelewa mno! Loh! Angalia; tuseme unataka watoto 2 au 4. Ukachukua plan hii: Mkapata hao watoto kila mwaka, mkeo atasumbuliwa kulea vichanga kwa miaka 5 tu katika maisha yake yote. Mnafungia mtoto wa 4 anakuwa huru na kusahau shida za kulea mara baada ya mwaka 1 tu.
Mtoto anatembea na kucheza na wakubwa zake. Nyiye mmesahau mambo ya kugumia vichanga. Mama anapata nguvu ya ajab na anakuwa na afya yake bado angali kijana. Wengine wanasema apate mtoto baada ya miaka 2. Tukitaka watoto 4 inamaana utatumia miaka 8. Huo uzee wote wa nini? Plan yangu mnachukua only 5 years mmesahau na anakuwa bado kijana tu.
Kama ni watoto 2 tu hata watu hawataamini kama aliwahi kuzaa. Tuwafundishe watu kutokana na experience si nadharia
 
Illovo

Kanisani wamegeuka madaktari, hospitali hakuna kilombero? Hawa wamama ndio maana wanapigwa miti hovyo na viongozi wa makanisa�� matatizo ya ndani kwako unampeleka kanisani ili iweje?

Nirudi kwenye mada. Hili sio tatizo lingekua kwangu ningefurahi maana watoto watakua pamoja. Biashara ya kuzaa na kukaa mpaka mtoto aombe mdogo wake haipendezi. Mtoto anyonye tu hakuna madhara, doctor atawashauri lini aache kunyonya.
Mama ale vyakula vya kumpa nguvu, doctor pia anaweza kuwashauri. Hamna sababu ya ku panic.
 
Last edited by a moderator:
Mliotoa ushauri unaostahili kwa huyu mwenzetu hongeza zenu nyingi sana. Inafurahisha na kutia moyo sana kuwasoma watu kama nyie ambao mko tayari hata kushare experience zenu ili kumhakikishia huyu mwenzetu kila kitu kitakuwa shwari. :yo: :yo::yo::yo::yo:
 
Happened to me, mtoto ana miezi saba mimba ina miezi miwili na kuna mtoto mwingine ana miaka miwili na miezi miwili. Niliendelea kumnyonyesha mtoto hadi mimba ikafika miezi nane.

Cha muhimu mama ale vizuri, balanced diet sio uji na mtori. Kitu kingine muwe organised pangilieni vitu nyumbani kwenu hasa nguo za watoto na vifaa vyao vingine. Hautaamini how stressful it can be unatafuta socks ya mtoto usiione. Dont panic inawezekana sana na hautaamini watakavyokua upesi. All the best.
 
wewe sio wa wanza na wala hutakuwa wa mwisho,inawatokea wanandoa wengi hasa kwa mtoto wa kwanza na wa pili huwa hawapishani sana,fuata shauri umepewa hapo juu!kila la kheri.
 
Ongea na mtaalam wako wa afya atakushauri vizuri lakini imeshatokea kwa watu wengi na mambo yameenda vizuri tuu
 
kawaida tu mbona hiyo mkuu!raha sana ukizaa fasta maana unawahi kupumzika zinabaki bata tu
 
Ongea na mtaalam wako wa afya atakushauri vizuri lakini imeshatokea kwa watu wengi na mambo yameenda vizuri tuu

ahaha!hiyo avatar yako ni shida aisee!hizo boxing kama floyd
 
Kiukweli nimefarijika sana na ushauri wenu wa kunitia moyo, sina neno zuri la kuwashukuru zaidi au cha kuwalipa. Ila tu mwenyezi mungu awabariki na kuwatia nguvu!
 
mwache azae ci mliendekeza ngono zembe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…