Tuna shida Kubwa sana ya Wataalam wa Magari katika Maeneo haya

SAE 40 Lita 4 wanauza kwa 28,000 wkt 5w-30 lita 4 nanunua kwa 60,000 mkuu.

Vp 5w-40 inaweza kua inauzwa sh. Ngapi?
Boss hio 5W30 kwa 60,000 ni very fair price. Achana na hizo SAE40 za 28,000. 5w40 same price na 5W30. Tumia 5W40 inaenda 10,000k mara tatu ya SAE40 huoni gharama inapungua? Ila kwa mazijgira yetu ikifika km5000 au 6000 badili
 
Boss hio 5W30 kwa 60,000 ni very fair price. Achana na hizo SAE40 za 28,000. 5w40 same price na 5W30. Tumia 5W40 inaenda 10,000k mara tatu ya SAE40 huoni gharama inapungua? Ila kwa mazijgira yetu ikifika km5000 au 6000 badili

Thnxs for the advice na hio bei ya elfu 60 naipataga kwenye duka 1 tu ,maduka ya wahindi lita 4 wanauza mpk 80,000.

Challenge niliyo nayo mkuu ni kwamba muda mwingi tunatumia gari ya kazini so inaweza ikapita miezi 3 sijamaliza hata km 2000.

Hapo unanishaurije mkuu?
 
Service huwa ni kwa km au muda(mwaka). Yaani kama umefikisha km10,000 hata ndani ya mwezi inabidi ufanye service AU kama mwaka umepita na gari umenitumia km2000 tu inabidi ufanye service.
 
Service huwa ni kwa km au muda(mwaka). Yaani kama umefikisha km10,000 hata ndani ya mwezi inabidi ufanye service AU kama mwaka umepita na gari umenitumia km2000 tu inabidi ufanye service.

Nilichokua namaanisha nimezoea kufanya service ya oil kila baada ya miezi 3,so nikawa nawaza nikitumia hizi oil za kwenda mpk km6000 ambazo pia ni expensive wkt sometimes ubize hata Km 2000 sifikishi,ndio maana nikawa nachek subsitute kwa cheap oil boss.
 
Ok unaweza kutumia hio ya km3000
 
Boss nna verosa 1g-fe recomended oil ni 5w-30 lkn ni expensive na upatikanaji wake sio sana,nataka nihamie kwenye SAE-40.

Unanishauri vp hapo mkuu?
Mkuu hizo oil zinapatikana sana madukani hata kwa wauzaji wa jumla shida yetu tumekalili baadhi ya kampuni kama hazina hizo oil na wewe hununui na pia kuhamia sae 40 haina athari yyt kwani wanashauri sana gari ikishatembea miles nyingi angalau uweke oil yenye viscosity kubwa kidogo kwa ajili ya kuilinda engine ya gari iweze kukaa kwa mda mrefu kidogo
 
Sory kampuni gani ambayo umekua unapata hizo oil za 5w-30 mkuu? Nasi twende huko
 
Kumbe una gari, Hongera sana mkuu wengine tunabanana na daladala zetu
 
Chamsingi ukishakua na gari kubali kataa lazima ujifunze kila kitu kinachohusu gari yako kuanzia tairi,oil ya kutumia,engine, suspension system n.k,.....ki bongo bongo hakuna mafundi wa kuweza kukidhi mahtaji yako kwa asilimia mia,mafundi wengi hawajaenda shule,na hawataki kujifunza,mimi kabla sijapeleka gari kwa fundi huwa nafanya utafiti kwanza sikurupuki,na hata ikitokea fundi kanipiga basi huyo ana bahati yake,maana nalijua gari langu nje ndani,......kuhusu oil najua most of engine oils hapa Dar ni feki, kwaiyo nachofanya naweka kama ni ya total wale wanazouza sheli,na nazingatia service kabla kms hazijaisha namwaga naeka nyingine,.....ukitaka uishiwe pesa na una gari jidai unaishi kiboss na gari, mafundi watakupiga hela hadi utaona,..mimi oil kila kitu huwa naenda nacho garage kazi ya fundi ni kumwaga na kuweka nyingine,simtumi fundi akanunue,...mimi fundi akiwa anatengenenza gari langu huwa anatamani nisiwepo maana kila anachofanya najua na vingine namuelekeza na vifaa naenda mwenyewe kununua labda iwe mbali,kiufupi mafundi hawanipendi maana nawachallenge sana,.....gari yangu iliwahi kuwa inawasha taa flani kwenye dashboard nikawa siielewi,nikapeleka gereji,nilitaka ninunulishwe gearbox mpya,fundi alisema gearbox imekufa,nikaondoka nikaendelea kufanya utafiti baadae nikagundua kuna boya la sensa kwenye gearbox lililegea hivyo kazi ilikua ni kuchomeka tu iingie kwa ndani zaidi,lakini fundi alisema ninunue gearbox mpya,...kuna fundi mwingine aliwahisema starter ya gari yangu imekufa maana gari ilizima kwa sababu ya betri kuwa down,akaja ku bust akashindwa,akasema bro hapa inabidi tutoe starter tuweke nyingine hii itakua imekufa,..nikaenda kuchaji betri kwenye umeme nikarudisha gari ikawaka bila shida ila yeye alisema ninunue starter mpya,....yapo mengi ila muda hautoshi!
USHAURI
Kabla hujaenda service fanya utafiti bongo mafundi wengi ni wapiga ramri tu hawana ujuzi na hawataki kuutafuta,watakumalizia pesa zako kwa kukuwekea oil au vifaa butu!
 
Unayosema ni kweli nakubaliana nawe kabisa.

 
Bro umezungumza vitu vingi sana na vya msingi ila cha kukusaidia sio kusema wauza oil wote wa mtaani wanauza oil feki hilo nalikataa ungesema baadhi yao wanauza feki kikubwa kuna wengine wanaenda kuchukua oder hapo kwenye vituo vya mafuta na kuuza dukani wajipatie kipato na pia kuhusu vifaa ni kweli mafundi wengi wana maduka yao ya spare hivyo ni bora akwambie kanunue kifaa hiki na sio kukwambia lete pesa tuweke atakuwekea vifaa vyake na kingine tupendelee kununua vifaa ambavyo ni genuine zaidi kuliko kukazana na mchina
 
Mimi kuna kifaa bora ninunue used kuliko cha dukani nachoambiwa ni original,most of them sio original....vifaa vingi original ni vile vilivyotoka na gari.....mimi nina mdogo wangu anauza oil Ilala ndio alinielekeza uhuni unaofanyika kwenye hizi oil tunazoaminishwa ni Og...
 
Ni kweli Mimi sijakataa kwamba uhuni aupo ila sio maduka yote kwa mtu ambae lengo lake ni kuwa mfanyabiashara mkubwa sidhani kama atakua na uhuni huo na maduka mengi ambayo yanauza genuine spare huwezi kukuta upuuzi kama huo bro na kuhusu oil angalau anakushauri kutumia za kampuni gani mkuu
 
Alisema bora kununua zile za Total wanazouza kwenye petrol station zao!
 
Alisema bora kununua zile za Total wanazouza kwenye petrol station zao!
Mimi sijaelewa wanachakachuaje kijana angalau ungetuweka sawa kidogo ili tupate maarifa ya kuzijua oil fake na original na tusipigwe pigwe huko mitaani
 
Mkuu naomba model ya gari yako, umri wake na kama imetembea zaidi ya km 100k au laa,
Matumizi ya oil yanatakiwa yaanzie kwenye specification ya manufacturer then kama hiyo grade haipo, then unaangalia alternative, naomba izo details nakusaidia sasa hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…