Tuna watoto 4, wote kwa operesheni, mimba ya 5 (na mke alishafunga kizazi)

Tuna watoto 4, wote kwa operesheni, mimba ya 5 (na mke alishafunga kizazi)

yutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
1,668
Reaction score
1,017
Habari wadau,

Mimi na mke wangu tuko kwenye ndoa mwaka wa 17 sasa na tumejaaliwa kupata watoto wanne wote wa kike.

Kutokana na uzazi wa mke wangu kujifungua kwa operesheni mara kwa mara madaktari hospitali ya mwananyamara walitushauri kuwa mke wangu afunge kizazi kwani mimba zaidi ya nne kwa operesheni itahatarisha uhai wake na mtoto pia endapo ataendelea kuzaa.

Kweli tulikaa na mke wangu japo tulitaka kuendelea kuzaa walau tupate mtoto wa kiume tukaona ni vizuri kufuata ushauri wa madaktari na kufanya kama walivyotushauri kwa kufunga kizazi.

Mwezi na siku na kadhaa zilizopita mke wangu alijisikia vibaya atukutilia maanani sana japo dalili zilikuwa ni za ujauzito kwani tuna miaka minne toka alipojifungua na kufunga kizazi.

Lakini hali hiyo iliendelea mpaka tulipoenda hospitali na kugundulika ana ujauzito wa miezi 3 na manesi walisema tayari hiyo mimba ni kubwa na kutokana na mishono aliyoshonwa tayari ni tatizo na kwa kifupi haitawezekana kujifungua salama eidha mtoto afe mama apone au mama afe mtoto apone
nilipopata hizi habari nilishtuka na kuhuzunika sana.

Nakuja mbele yenu wanajamvi mnipe ushauri mwenye uzoufu na masuala kama haya naamini kabisa inawezekana madaktari hawakufanya kazi yao ipasavyo katika kufunga kizazi lakini tayari tatizo limeshatokea, je tuuwe kiumbe au kilichopo tumboni au tufanyaje?"

Ushauri tafadhari.
 
pole sana mkuu kwa mtihani huo uliokupata...

sacrifice your child for the survival of your children..

kuna vitu vingine ni vigumu sana kuvielezea katika maisha..
 
pole sana mkuu kwa mtihani huo uliokupata...

sacrifice your child for the survival of your children..

kuna vitu vingine ni vigumu sana kuvielezea katika maisha..
asante @Exel
 
wacha washauri watiririke.............POLE SANA...naamini yatapita
 
pole sana mkuu kwa mtihani huo uliokupata...

sacrifice your child for the survival of your children..

kuna vitu vingine ni vigumu sana kuvielezea katika maisha..


Amani iwe nawe popote ulipo
 
Poleh sana mkuu,okoa maisha ya mama ili mlee wote watoto waliopo
 
Habari wadau,
"mimi na mke wangu tuko kwenye ndoa mwaka wa 17 sasa
na tumejaaliwa kupata watoto wanne wote wa kike. kutokana na uzazi wa
mke wangu kujifungua kwa operesheni mara kwa mara madaktari hosp ya
mwana nyamara walitushauri kuwa mke wangu afunge kizazi kwani mimba
zaidi ya nne kwa operesheni itahatarisha uhai wake na mtoto pia endapo
ataendelea kuzaa. kweli tulikaa na mke wangu japo tulitaka kuendelea
kuzaa walau tupate mtoto wa kiume tukaona ni vizuri kufuata ushauri wa
madaktari na kufanya kama walivyotushauri kwa kufunga kizazi.
mwezi na siku na kadhaa zilizopita mke wangu alijisikia vibaya
atukutilia maanani sana japo dalili zilikuwa ni za ujauzito kwani tuna
miaka minne toka alipojifungua na kufunga kizazi, lakini hali hiyo
iliendelea mpaka tulipoenda hospitali na kugundulika ana ujauzito wa
miezi 3 na manesi walisema tayari hiyo mimba ni kubwa na kutokana na
mishono aliyoshonwa tayari ni tatizo na kwa kifupi haitawezekana
kujifungua salama eidha mtoto afe mama apone au mama afe mtoto apone
nilipopata hizi habari nilishtuka na kuhuzunika sana.
nakuja mbele yenu wanajamvi mnipe ushauri mwenye uzoufu na masuala kama
haya naamini kabisa inawezekana madaktari hawakufanya kazi yao ipasavyo
katika kufunga kizazi lakini tayari tatizo limeshatokea, je tuuwe kiumbe
au kilichopo tumboni au tufanyaje?"
ushauri tafadhari.

Duuh!
Pole mkuu. MKE wako kwanza kabla ya mtoto! Nadhani umeelewa.
 
Hivi hili linahitaji ushauri wa kila mtu au ni emergency na inahitaji "medical/surgicical/gyn-obs" immediate intervention????!!!!!!

Akitokea mtu akakuambia acha mimba ikue sababu huo ni muujiza utakubali????!!!
 
Hivi hili linahitaji
ushauri wa kila mtu au ni emergency na inahitaji
"medical/surgicical/gyn-obs" immediate intervention????!!!!!!

Akitokea mtu akakuambia acha mimba ikue sababu huo ni muujiza
utakubali????!!!

Toa ushauri, acha kuuliza maswali mkuu.
 
okoa maisha ya mama mkuu.
na ingekuwa ni nchi za wenzetu hiyo hosp ingekulipa hela ndefuuu sana ni uzembe wa daktari
 
Abortion sometime can be legalized under emergency case like this,no way out
 
Toa ushauri, acha kuuliza maswali mkuu.

The fact kuwa ni suala tata la afya yeye kalileta MMU na kutaka ushauri wa jumla kwa jambo ambalo kashaambiwa kuwa ni hatari linanifanya nimuulize maswali na katika kuyajibu ndio akili itamkaa sawa!!!!!!
 
Pole sana...kwani Tanzania hakuna hosp.inayoweza kuokoa maisha ya mama na mtoto?
 
Mkuu mpaka umekuja kwenye jamvi naamini jibu unalo kuwa mama anatakiwa kubaki dhidi ya mtoto.
Ila inaelekea una hamu sana na huyo mtoto anayefanyiwa ukandarasi hapo tumboni ndio maana umeomba ushauri!! Mimi nimekuelewa kuwa JE hamna njia za kuokoa maisha ya mama na mtoto wote waweze kuishi salama???
Cha muhmu nenda hospital zenye madaktari bingwa wa uzazi na kaombe ushauri zaidi !! LaBda kuna njia inaweza fanyika...
 
Mungu anaweza kufanya miujiza muombe utashinda nenda hosp kubwa watakushauri ikishindikana bas waitoe bd mapema
 
Back
Top Bottom