Tunahitaji kuzalisha ajira, kukuza uchumi, kupunguza umaskini na kuboresha hali za maisha. Je, tuanze na lipi?

Tunahitaji kuzalisha ajira, kukuza uchumi, kupunguza umaskini na kuboresha hali za maisha. Je, tuanze na lipi?

Masokotz

JF-Expert Member
Joined
Nov 26, 2018
Posts
3,713
Reaction score
6,121
Hiki ni kipindi cha siasa na kama kawaida huwa napenda sana kupita katika vijiwe vya kahawa kujadili kuhusu uelekeo wa siasa zetu na maendeleo yetu.

Katika vijiwe vyote nilivyopita pembeni ya kukuta watanzania wengi wakiwa bado na ile mitazamo ya ajabu ajabu kuhusu siasa na maendeleo kuna mambo manne ambayo yanajitokeza mara kwa mara ikiwamo. Ukosefu wa ajira,Ugumu wa maisha,hali Umaskini na hali ngumu ya uchumi.

Ukipita mjini na kuangalia idadi ya biashara ambazo zimefungwa unaweza kupata kihoro kwani ni kama vile tumegeuka TAIFA la WAMACHINGA na MAMA LISHE.mbaya zaidi wamachinga wengi wanauza bidhaa zile zile kutoka nchi zile zile.Kuanzia Posta,kariako,Tegeta,Sinza,etc.Hali ni ile ile.

Ukirudi mitaani huku idadi ya madalali imeongezeka,wa viwanja,nyumba etc na wanunuzi ni wachache.

Suala la kujiuliza ni Je kama TAIFA tufanye nini ili kubadilisha hali ya TAIFA letu?Tuanze na nini?
 
Mimimi nahitaji kusikia, Serikali itawezaje kutengeneza ajira angalau milioni moja ndani ya mwaka mmoja
Kwangu ni kipaumbele namba moja
 
Mada fikirishi;-
1. Kukuza Uchumi wa Taifa.
2. Kuleta maendeleo ya WATU
Kipi kianze au kipaumbele hapo kiwe kipi?

•Je, tunaweza kukuza uchumi wa watu bila kukuza uchumi wa Taifa?
Uchumi wa Taifa unakuzwa kwa kufanya maendeleo yapi, miundombinu ipi itakuza uchumi wa Taifa ili in the end uchumi wa mtu mmoja mmoja uwe imara.

•Nakubaliana na wewe, petty businesses zimekuwa nyingi, kila kona ni vibanda vya maji, juice, nguo, viatu.

•Tunahitaji kukuza uchumi ili kuachana na vibiashara vidogo vidogo, je tufanyaje ili kufikia hapo?

• Je, nchi za wenzetu, watu wa hali ya chini na kati, wasio na qualifications za kushindana katika soko la ajira wako wapi?

• Kwa nini wengi tumejazana katika "service industry"(utoaji huduma) na sio production industry?
 
Back
Top Bottom