Tunahitaji mwelekeo na dira Sasa

Tunahitaji mwelekeo na dira Sasa

Shayu

Platinum Member
Joined
May 24, 2011
Posts
608
Reaction score
1,655
Elimu ya uzalishaji mali na utoaji huduma ni sehemu ndogo sana ya maarifa lakini maarifa yaliyo makubwa ni jinsi gani watu wetu watakuwa na uwezo wa kuishi kwa pamoja na kujenga mahusiano yaliyo mema miongoni mwao kwa kufanya hivi taifa letu litakuwa na uwezo wa kubaki muda mrefu na kukua kwasababu bila kutengeneza elimu itakayojenga mahusiano yetu kama watu wa taifa moja hatutaweza kufika popote.

Ni Elimu hii ambayo itatujenga kuwa na mwelekeo mmoja kama taifa badala ya kuwa watu wa taifa moja wenye mielekeo tofauti. Ni lazima kuwe na kitu kilichotuunganisha kama Taifa na kutufanya tuwe na mwelekeo mmoja na elimu tunayoitoa iwe yenye msaada kwa huko tunakotaka kwenda kama taifa kwakuwa kama elimu yetu haitaelekezwa katika mkondo fulani bali tukawa tunazalisha tu watu na kuwaacha, elimu hii haitasaidia kitu. Ni lazima tutengeneze mkondo na tuzalishe watu ili wafuate mkondo huo na sio kuzalisha watu na kuwatupa hii ni sawa sawa na kupanda mbegu bila mpangilio mzuri shambani.

Elimu yetu isiwe tu kwaajili ya kufanya watu wapate ajira na kupata mlo wa kila siku bali iwe ni sehemu ya mkakati wa kulifikisha Taifa hili sehemu fulani. Kwasababu sisi kama watanzania kuna sehemu fulani lazima tufike kwa pamoja, kuna sehemu tunataka kwenda na hatutafika kama muundo wa elimu tunayoitoa utakuwa haujapangiliwa kutufikisha huko.

Sisi kama Taifa ni lazima tuwe na mwelekeo hili haliepukiki ni lazima tuwe na sehemu miongoni mwa Mataifa. Haiwezekani tukawa tunatengeneza wasomi na elimu yenye mlengo wa manufaa binafsi badala ya ukombozi wa Taifa hili si sahihi na hatutakuwa na mwelekeo kama taifa kama tutakuwa na aina hii ya mawazo. Tunahitaji ukombozi mpya wa fikra utakao tuweka huru na kujitambua kuhusu utaifa wetu na umoja wetu. Tunahitaji mwelekeo na dira Sasa!
 
Hicho unachoongelea ndio mpango mzima utakaoweza kututoa kutoka point A to B, naunga mkono hoja kwa sasa hakuna dira kama taifa na hapa hakuna wakuvuna lawama zaidi ya uongozi uliopo madarakani. Watu wengi washabiki wa serikali wanapenda kutetea maswala ya namna hii kwa kuonyesha uwingi wa vyuo na idadi ya wahitimu leo ukilinganisha na zama za nyuma.

Kitu ambacho hawakigusii ni kwamba zamani tulikuwa tukitoa wahitimu wachache lakini wengi walikuwa directed kwenye sector moja kwa moja, wasomi walizalishwa kutokana na uwezo wa uchumi na market labour zilizokuwepo. Leo idadi ya wahitimu kubwa ambao wanasoma bure na mikopo ya serikali wengi wana miaka mingi sasa ajira hawajapata kwa upande mwengine huu ni utumiaji mmbaya wa resources unless labda somebody is funding these ambitions indirectly kupitia hiyo misaada ya donors.

Kuwe na misaada kusiwe na misaada jinsi serikali inavyo fund elimu hasa ya juu kuna umuhimu wa kuwa na dira na kutoa wahitimu wengi ambao wanaweza pelekwa sehemu. Inabidi kuwe na plan ambayo hipo coordinated kati ya sera kuu, wizara ya elimu na vyuo vikuu.

Kwa mfano leo chini ya kilimo kwanza unaenda toa ma sociologist halafu ujui huwapeleke wapi kwanini wahusika hawakulifikiria hili. Nadhani inabidi sasa tuwe na coordination inayo eleweka leo wakulima wengi sana wanafaidika na sera za kilimo kwanza, matatizo ya chakula yanapungua hila sasa mazao yanaoza. Solution inayotumika nikuwafundisha wakulima ujasiriamali mara baada wanapovuna si swala baya, lakini unajiuliza kwenye nchi ambayo imejaa vijana wengi wasio na ajira kwanini serikali isiwekeze na hawa vijana ndio waingie kuwa wajasiriamali na kuongeza wigo la ushiriki katika uchumi wa taifa.

Ili kufikia huko sasa unajikuta na vyuo vinalenga sana kwenye course za kilimo kama ni uchumi au biashara course nyingi zijikite na kilimo ambapo wahitimu wataweza ona opportunities na kuweza hata kutoa mapendekezo ya kuboresha changamoto hili waweze shiriki kifaida maana watakuwa wamesoma ie upatikanaji wa mikopo, changamoto za usafiri, soko etc, hili wahusika waweze kuja na sera mbadala za ku adress hizo changamoto.

Vilevile serikali za mitaa badala ya kuendela na tamaduni za tender ni vyema wakawa na timu zao za ma-architectures, planners, na namna za kuongeza mapato yao hata kwa vijijini maana kwa sasa naona ni manispaa za mjini tu ndio zinazofaidika zaidi, vijijini changamoto wao ni kujenga mashule tu mi naona more needs to be done kuahikikisha there is inclusiveness of all tanzanians hata vijijini kuna mbinu za kujiongezea mapato katika serikali zao na kutoa ajira nyingi tu zaidi ya mabwana shamba.

Something has to be done tupo kwenye karne ambayo hatuhitaji kuwa wabunifu vile case studies zimejaa leo na there is enough archive from developed nations on the stage we are and how they evolved from there, kuwa na resources tulizokuwa nazo na kubaki maskini ni uzembe tu kutoka kwa wahusika there is no other justification.
 
Hili suala niliwahi kuligusia mwezi January ktk post yangu kwa Facebook . Ni suala zito na ndio kikwazo kikubwa cha kwanza kwa maendeleo ya Taifa letu, ndipo hayo mengine yanafuata. Sioni sababu ya kupigania Katiba Kabla ya Elimu, Elimu ingeanza kwanza hata Katiba bora ingepatika bila Shaka, hii Katiba ya sasa bila Elimu kwanza ni kazi bure, Haitatusaidia
 
Hili suala niliwahi kuligusia mwezi January ktk post yangu kwa Facebook . Ni suala zito na ndio kikwazo kikubwa cha kwanza kwa maendeleo ya Taifa letu, ndipo hayo mengine yanafuata. Sioni sababu ya kupigania Katiba Kabla ya Elimu, Elimu ingeanza kwanza hata Katiba bora ingepatika bila Shaka, hii Katiba ya sasa bila Elimu kwanza ni kazi bure, Haitatusaidia

Umesomeka Andrew nami naamini hivyo pia.
 
Hicho unachoongelea ndio mpango mzima utakaoweza kututoa kutoka point A to B, naunga mkono hoja kwa sasa hakuna dira kama taifa na hapa hakuna wakuvuna lawama zaidi ya uongozi uliopo madarakani. Watu wengi washabiki wa serikali wanapenda kutetea maswala ya namna hii kwa kuonyesha uwingi wa vyuo na idadi ya wahitimu leo ukilinganisha na zama za nyuma.

Kitu ambacho hawakigusii ni kwamba zamani tulikuwa tukitoa wahitimu wachache lakini wengi walikuwa directed kwenye sector moja kwa moja, wasomi walizalishwa kutokana na uwezo wa uchumi na market labour zilizokuwepo. Leo idadi ya wahitimu kubwa ambao wanasoma bure na mikopo ya serikali wengi wana miaka mingi sasa ajira hawajapata kwa upande mwengine huu ni utumiaji mmbaya wa resources unless labda somebody is funding these ambitions indirectly kupitia hiyo misaada ya donors.

Kuwe na misaada kusiwe na misaada jinsi serikali inavyo fund elimu hasa ya juu kuna umuhimu wa kuwa na dira na kutoa wahitimu wengi ambao wanaweza pelekwa sehemu. Inabidi kuwe na plan ambayo hipo coordinated kati ya sera kuu, wizara ya elimu na vyuo vikuu.

Kwa mfano leo chini ya kilimo kwanza unaenda toa ma sociologist halafu ujui huwapeleke wapi kwanini wahusika hawakulifikiria hili. Nadhani inabidi sasa tuwe na coordination inayo eleweka leo wakulima wengi sana wanafaidika na sera za kilimo kwanza, matatizo ya chakula yanapungua hila sasa mazao yanaoza. Solution inayotumika nikuwafundisha wakulima ujasiriamali mara baada wanapovuna si swala baya, lakini unajiuliza kwenye nchi ambayo imejaa vijana wengi wasio na ajira kwanini serikali isiwekeze na hawa vijana ndio waingie kuwa wajasiriamali na kuongeza wigo la ushiriki katika uchumi wa taifa.

Ili kufikia huko sasa unajikuta na vyuo vinalenga sana kwenye course za kilimo kama ni uchumi au biashara course nyingi zijikite na kilimo ambapo wahitimu wataweza ona opportunities na kuweza hata kutoa mapendekezo ya kuboresha changamoto hili waweze shiriki kifaida maana watakuwa wamesoma ie upatikanaji wa mikopo, changamoto za usafiri, soko etc, hili wahusika waweze kuja na sera mbadala za ku adress hizo changamoto.

Vilevile serikali za mitaa badala ya kuendela na tamaduni za tender ni vyema wakawa na timu zao za ma-architectures, planners, na namna za kuongeza mapato yao hata kwa vijijini maana kwa sasa naona ni manispaa za mjini tu ndio zinazofaidika zaidi, vijijini changamoto wao ni kujenga mashule tu mi naona more needs to be done kuahikikisha there is inclusiveness of all tanzanians hata vijijini kuna mbinu za kujiongezea mapato katika serikali zao na kutoa ajira nyingi tu zaidi ya mabwana shamba.

Something has to be done tupo kwenye karne ambayo hatuhitaji kuwa wabunifu vile case studies zimejaa leo na there is enough archive from developed nations on the stage we are and how they evolved from there, kuwa na resources tulizokuwa nazo na kubaki maskini ni uzembe tu kutoka kwa wahusika there is no other justification.
Umeeleweks
 
Back
Top Bottom