Tunahitaji nini?

Chauro

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2010
Posts
2,968
Reaction score
1,478
Huwa tunahitaji nini kuwaonyesha wenzetu kuwa tunawapenda na kuwathamini?

Je huwa tunahitaji kuwadanganya mara zote ili kuwapa faraja kwa yale ambayo hatuyafanyi ili kuwamiinisha na kuendelea kutuamini wakati sivyo?

Je kuna ubaya wa kuwa mkweli kwa mwenzako?

Nahitaji sana mawazo yenu ili niweze jifunza kitu nimeanza kuamini labda uongo una faida kuliko ukweli na kitu ambacho sipendi kukiamini.
 
Mhhh!!! It seems there's something bothering you, ukiamua kusema uongo sema uongo, ukiamua kusema ukweli sema ukweli it's all upon you
 
Chauro, kama unampenda utamjali..
ni sentensi fupi sana lakini ukiichambua ndio majibu.
utapenda awe na furaha
utamlinda na magonjwa na hatari mablimbali
uta muheshimu
utamsaidia
 
Nah,naamini kwenye ukweli lakini ni vipi pale ukweli unapotaka kulazimishwa kuwa uongo.


Mhhh!!! It seems there's something bothering you, ukiamua kusema uongo sema uongo, ukiamua kusema ukweli sema ukweli it's all upon you
 
Reactions: Mbu
Thanks ,pamoja na kufanya yote hayo ni vipi kwa wale wanaonekana hawakuamini kabisa hata ukisema unaenda dukani yeye anaamini ulikuwa na jingine hata kama hufikiri wala hujawahi fanya hayo.

Chauro, kama unampenda utamjali..
ni sentensi fupi sana lakini ukiichambua ndio majibu.
utapenda awe na furaha
utamlinda na magonjwa na hatari mablimbali
uta muheshimu
utamsaidia
 
Nah,naamini kwenye ukweli lakini ni vipi pale ukweli unapotaka kulazimishwa kuwa uongo.
Unajua unapomwambia mtu ukweli yeye akalazimisha uonekane uongo wewe muache hivyo hivyo maana ukiendelea kung'ang'ania unaweza kuonekana labda na wewe unalazimisha maana siku zote uongo na ukweli hujitenga sasa kama mtu hataki kuamini wewe endelea na ndio maana mimi mtu wa hivyo huwa namwambia vice versa ukweli namwambia uongo na uongo namwambia ukweli maana inakuwa imeishakuwa kero
 
Thanks ,pamoja na kufanya yote hayo ni vipi kwa wale wanaonekana hawakuamini kabisa hata ukisema unaenda dukani yeye anaamini ulikuwa na jingine hata kama hufikiri wala hujawahi fanya hayo.
Dah, hako ni kaugonjwa,
tatizo mtu anakua hajiamini na alichonacho
anadhani anaweza kuibiwa, i mean haamini kwamba amekumiliki na ww umempenda yy tu
Jaribu kumuhusisha step by step kama vile:
Nitakwenda sokoni baadae,
ukiwa sokoni mpigie nipo sokoni kuna maembe utapenda kwe leo
leo daladala zinasumbua nipo stand
njoo unipokee basi nakaribia
 
chauro, analyse the situation then you can lie, but kumbuka uongo wako unaweza kukugeuka baadae
 
Dah we acha tu kuna wengine wameumbwa kuonekana wahalifu tu,ngoja wamaliziee kaijumaa humu.

Hivi sangapi saahizi au ndio ijumaa yenyewe?
 
Mapenzi hayana formulae... na namnukuu JF member Arsene Wenger "Mapenzi kitu cha ajabu saana" kweli kabisa un predictable tokana na the fact kua kila mwanadamu kazaliwa na hulka/tabia tofauti, kalelewa mazingira tofauti na ana tofauti na mwanadamu mwingine yule yeyote, hivo waweza fanya hili kwa huyu and it works... ukaenda na hilo hilo kwa mwingine na it does not....

However...

Huwa tunahitaji nini kuwaonyesha wenzetu kuwa tunawapenda na kuwathamini?


Personally hapa mimi huona ni matendo.... Actions speaks louder than words... na nafikiri msemo wa mapenzi kikohozi ilitokana na hii fact; huwezi sema unampenda mwenzio bila kuonesha kwa kumjali, kusikiliza, kumthamini na kumfanyia yale yoote ambayo wapenzi (mtu in love) hufanya... mradi isiwe ya kukithiri ama kua too demanding toka kwa mwenzio kufanya the same...

Je huwa tunahitaji kuwadanganya mara zote ili kuwapa faraja kwa yale ambayo hatuyafanyi ili kuwamiinisha na kuendelea kutuamini wakati sivyo?

Uongo una nafasi yake katika kufanikiwa/kushamiri kwa mahusiano... Kuna topic juzi kati hapa ilikuwepo jamvini na copy na kupaste (topic "Kanidanganya kwa nia nzuri" ) kuhusiana na jinsi nichukuliavo uongo katika mahusiano....


Je kuna ubaya wa kuwa mkweli kwa mwenzako?

Kua mkweli daima is the best option... for a relationship to succeed fully inategemea trust... but kama nilivo eleza katika hio green post sometimes uongo hauepkiki....
 
Thanks Ashadii vipi kwa wale wanaotaka kulazimisha uongo kuwa kweli uwa unawahandle vipi.

 
Uongo si mzuri,ila kuna sehemu kwenye mapenzi lazima u aply ka uongo japo kidogo ili mambo yaeze kwenda sawa, kumbuka watu hupenda uongo kuliko kuambiwa ukweli,kwa mfano mumeo anaweza kuwa mbaya wa sura japo umempenda kama alivyo, akiwa anaenda kazini unamwambia you look handdsome, au your the most handsome man i've ever seen. si unaona kabisa na yeye anafurahi lakini akifika kwenye gari anajiangalia kwenye site mirror na kuguna mhhhhhh
 
Chauro,

haya mambo magumu saana mabinti wa kileo usipo wadanganya hawakuamini kabisa,

unampompamba kwa uwongo ndio anakuona wa maana na upo makini
 
Kweli kuna visifa vya uongo huwa vinachochea mapenzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…