Tunahitaji Tanzania Development Authority (TDA)

Tunahitaji Tanzania Development Authority (TDA)

ego

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2013
Posts
1,620
Reaction score
1,407
hatua ya kwanza katika maendeleo ya nchi ni kuwa na mipango endelevu, la pili ni kutekeleza mipango na la tatu ni kuwa na usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

kama taifa tunahitaji chombo kinachoratibu maendeleo ya taifa na kupanga mipango ya kitaifa ndio maana ni muhimu sana kwetu sisi kuunda TDA kwa ajili ya kuratibu maendeleo yetu.

chombo hiki ndio kipange mipango ya taifa na vyama vya siasa vipange ilani za kisiasa na mambo ya kitaifa iwe ni kupanga mbinu za kutekeleza mipango ya kimaendeleo ya taifa.

1.chombo hiki kikiwepo kitapunguza kauli mbiu za maendeleo bali wataweka mikakati ya kutekeleza mipango ya maendeleo.
2. chombo hiki kitapunguza safari za viongozi nje, bali chombo hiki ndicho kipangiwe ziara za mafunzo ambazo nina uhakika zitakuwa na tija tofauti na utalii tunaoufanya tudhani tunaenda kujifunza
3. chombo hiki kitaweka malengo na mikakati ya kitaifa yenye mantiki kulingana na uchumi wetu na kuweka mikakati ya utekelezaji.
4. chombo hiki ni lazima kiwe na sekita mbalimbali na sio kuchukua watu 30 eti wanapanga mipango ya taifa wanaishia kukopi na kupesti un realistic programs.
5. tuwe serious na chombo hiki kwa kukipa nguvu na kukiacha kifanye kazi kwa weledi sio kupeana kazi kwa kujuana na mwisho wa siku kipo kwa jina lakini kiuhalisia kinakuwa kama hakipo.

nafikiri aliyekuja na kauli mbiu ya maisha bora kwa kila mtanzania angeunda chombo kama hiki kupanga na kuunda vyombo vingine vya kiutendaji kulingana na mahitaji hata kama watanzania wote wasingepata maisha mazuri katika kipindi chake lakini angetambuliwa kuwa yeye ndiye aliyeleta mageuzi kwa kuweka mifumo iliyogeuza uchumi wa nchi.
 
Tatizo la Tanzania ni uwajibikaji hata uunde nini kitafel.Jiulize hivi mamlaka zilizopo zimesaidia nini? Elimu na wenyewe wanataka mamlaka naona kila wizara sasa iunde mamlaka.
 
Mkuu, mamlaka zinapoundwa zinapewa uwezo wa kubuni vyanzo vya mapato vijiendeshe. Licha ya uzuri wa Mamlaka, lkn zinaongeza mzigo kwa Mwananchi. Ni vizuri kabla ya kufikiria kuanzisha Mamlaka, tuangalie kwa makini umuhimu wake kwenye suala husika.

Tunavyo vyombo vinavyoweka mipango ya maendeleo na kushauri serikali juu ya njia bora kufikia maendeleo kwenye eneo husika. Chombo kikubwa kabisa ni 'Tume ya Mipango' ambayo, kama sijakosea, iko chini ya Wizara ya Fedha kwa sasa. Yenyewe ndio yenye jukumu la kuratibu na kuweka vipaumbele vya maendeleo kuzingatia raslimali zilizopo. Tume inapokea mapendekezo toka Serikali kuu inayoundwa na MDAs (ministries, departments na agencies) ambazo zina vitengo vya kuweka mipango ya maendeleo na kupanga bajeti kulingana na vipaumbele walivyojiwekea. Licha ya kuwepo kwa utaratibu huu, kila mwaka tunashuhudia jinsi wanasiasa wanavyolarua mipango ya Tume pale Bungeni. Ni wazi kwamba hata tukianzisha Mamlaka, wanasiasa wataendelea kutumia kisingizio cha kuwakilisha wananchi kubadiri ushauri wa kitaalamu kwa manufaa yao. Mwisho wake utakuwa ni kuongeza mzigo kwa wananchi pasipo matokeo chanya.

So, kwa utaratibu huu sioni uchawi utakaofanywa na Mamlaka iwapo hata sasa Mwanasiasa anajua wazi kuwa ufinyu wa bajeti ndio unaokwamisha miradi mingi ya maendeleo, yet anakuja na BRN as if hiyo BRN itapata pesa toka mbinguni!!
 
Nafkiri ndc(national development Corporation) ndo inahusika na kuratibu mikakati yote ya maendeleo nchini
 
Tatizo la Tanzania ni uwajibikaji hata uunde nini kitafel.Jiulize hivi mamlaka zilizopo zimesaidia nini? Elimu na wenyewe wanataka mamlaka naona kila wizara sasa iunde mamlaka.

kwanza kabisa mimi naunga mkono ikiwa shughuli zote za serikali zitaundiwa mamlaka.

nikianza na mamlaka hii ya maendeleo tanzania. maendeleo yanakuja kwa kupanga.

serikali inaibuka na mikakati mingi tu ambayo inakwama kutokana na wanaopanga mipango hiyo hawaangalii mambo mengi katika jamii yetu kwa mapana.

mfano wakati inajengwa barabara ya kila wizara ya maji kupitia dawasa walikuwa wameweka bomba la maji kuelekea temeke, bomba la maji limeisha halijaanza kutumika wizara ya ujenzi ikataka kupanua barabara na kutoka katika pesa ya kujenga barabara hiyo wakalipa gharama za kuhamisha bomba kulisogeza pembeni.

serikali inafanya maboresho ya barabara nyingi za dar ili kuondoa msongamano na katika kufanya hivyo inabidi kuharibu barabara nyingine ambazo zilikuwa na uwezo wa kukaa miaka kumi ijayo kitendo ambacho ni kupoteza fedha.

kutokana na kutokuwepo kwa masta plan ya maendeleo ya taifa kila shughuli ya maendeleo tunayotaka kuifanya inakuwa ni ghali sana kutokana na miundo mbinu iliyopo haiingii katika mipango hiyo.

lakini kama tungekuwa na masta plan ya maendeleo ya taifa kila mradi unaotengenezwa ungekuwa kwanza unaingia katika masta plan hiyo hivyo mradi unaofuata sio kufuta uliotangulia na kuanza upya bali ni kuendeleza.

mfano mradi wa mabasi yaendayo kwa kasi tulivutana juu ya kuvunja jengo la tanesco pale ubungo, barabara zote zilizokuwepo zimekwanguliwa ili kuweka mpya. hivi kama tungekuwa na masta plan tangu mwanzo inaonyesha kwanza eneo la barabara au usafirishaji kama tunampango wa kutumia treni katika barabara hiyo ni lipi na hivyo tangu masta plan imetolewa hairuhusiwi kufanya mwendelezo wowote katika majengo yaliyoko katika eneo hili. pili tunaangalia katika miaka 30 ijayo mfumo wa barabara utakuwaje ili kama ni kujenga sehemu fulani kwa sasa tunajenga sehemu moja na baada ya miaka kadhaa tunajenga sehemu ya pili kuongezea na sio kuharibu kilichokuwepo na kuanza upya. maji yanawekwa sehemu yake, umeme unawekwa sehemu yake.

kwa sasa nani apange haya? kila wizara inaangalia mambo yake. na ndio maana kunakuja umuhimu wa kuanzisha mamlaka hii kuziunganisha kazi zote zinazofanywa na wizara zote na hii ni kazi ya waziri mkuu hivyo mamlaka hii inatakiwa kuwa chini ya waziri mkuu.

mpango wa kwanza katika maendeleo ya mji ni kuapnga mji, nani aseme hili? waulize dawasa wanavyahangaika kutoa huduma za maji dar kutokana na mji kutokupangwa, waulize mawasiliano walivyoshindwa kuweka anwani za makazi kutokana na dar kujaa makazi holela, waulize wanaohusika na kurasimisha biashara walivyoshindwa kurasimisha biashara kutokana na biashara kukaa holela bila mpangilio, waulize tanesco wanavyosumbuliwa na makazi holela. ki msingi kila wizara utakayoigusa makazi holela yanawakwamisha.

wote wanakwama kwa tatizo hili lakini kutokana na kutokuwepo chombo kinachoangalia matatizo ya taifa kwa pamoja na kikapanga kuwa mfano ili kuiboresha dar ndani ya miaka 15 ijayo tutaanza na kupanga makazi na kutafuta mpango ambao utapanga makazi yetu kwa gharama ndogo si kufanya dili za kutengeza fedha kupitia miradi mikubwa. bali kuangalia jinsi serikali inaweza kuwawezesha wataalamu wa upimaji kwa kuwapa vifaa, wizara inatoa masta plan wao wanawapimia wananchi kwa kuwatoza ghara ndogo, kila kiwanja kinakuwa na barabara na kila uongozi wa mtaa unasimaia shughuli hii na kuweka utaratibu wa kwenda mpaka ngazi ya taifa kwa gharama ndogo sana. wizara itapata kodi za majengo baadae na wanaweza kuwa na miradi mikubwa ya kuweka sehemu za viwanda na huduma nyingine.

mpango unaelekeza baada ya kumaliza au wakati tukiendelea na mpango huu tunakuwa na mpango wa kuboresha usafiri wa umma tunaweka mikakati, tunaweka ubora wa makazi unaoruhusiwa maeneo fulani fulani, tunaweka mpango wa huduma za jamii.

hapa ni pale tunapozungumzia jiji au mji.

lakini ipo mipango ya kitaifa ambayo mkishafanya hizo skeletoni ni kazi ya mamlaka husika na wizara kujaza nyama ili kukamilisha na wakati huo mamlaka hii inapita kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa mipango ili kufanya maboresho.

lakini bila mipango kila mmoja anafanya anavyojua na akija mwingine anafuta kabisa ya mwenzake anafanya ya kwake hatuwezi kuendelea.

hivyo kuendesha shughuli za taifa kwa kutumia zaidi mamlaka na kupunguza ukubwa wa serikali ni jambo la msini sana na lina tija.

mfano huduma za jamii zote zinaweza kuundiwa kila hiduma mamlaka yake alafu zote zinawekwa katika wizara moja inayoitwa wizara ya huduma za jamii.

shughuli za maendeleo zote zinaweza kuwekwa katika wizara moja kila moja ilikundiwa mamlaka yake. huduma hizi zikiwa katika wizara moja kunakuwepo urahisi wa kuweka kipaumbele, wataalamu kushirikiana na kuona jamii inahitaji huduma gani kwa haraka na malengo ya sekta husika kusimamiwa na mamlaka inafanya mipango endelevu katika sekta na sio kupanga kwa kuangalia mda wa waziri kuwa kwenye uongozi. na mpango huu unaweza kuwaweka viongozi wa kisiasa katika sera zaidi na utendaji ukabaki kwa mamlaka.
 
Nafkiri ndc(national development Corporation) ndo inahusika na kuratibu mikakati yote ya maendeleo nchini

ki msingi hapa tunahitaji chombo cha kupanga na kusimamia maendeleo ya taifa kwa ujumla, silijui hili ndc kitu ambacho kinaweza kuwa kinaashiria kama kipo ni katika karatasi na ofisi yake lakini ki mfumo hakuna mamlaka yoyote.

TDA kiwe ni chombo cha waziri mkuu kumwezesha kufanya kazi hivyo kinatakiwa kiwe chini ya waziri mkuu.
 
Mkuu, mamlaka zinapoundwa zinapewa uwezo wa kubuni vyanzo vya mapato vijiendeshe. Licha ya uzuri wa Mamlaka, lkn zinaongeza mzigo kwa Mwananchi. Ni vizuri kabla ya kufikiria kuanzisha Mamlaka, tuangalie kwa makini umuhimu wake kwenye suala husika.

Tunavyo vyombo vinavyoweka mipango ya maendeleo na kushauri serikali juu ya njia bora kufikia maendeleo kwenye eneo husika. Chombo kikubwa kabisa ni 'Tume ya Mipango' ambayo, kama sijakosea, iko chini ya Wizara ya Fedha kwa sasa. Yenyewe ndio yenye jukumu la kuratibu na kuweka vipaumbele vya maendeleo kuzingatia raslimali zilizopo. Tume inapokea mapendekezo toka Serikali kuu inayoundwa na MDAs (ministries, departments na agencies) ambazo zina vitengo vya kuweka mipango ya maendeleo na kupanga bajeti kulingana na vipaumbele walivyojiwekea. Licha ya kuwepo kwa utaratibu huu, kila mwaka tunashuhudia jinsi wanasiasa wanavyolarua mipango ya Tume pale Bungeni. Ni wazi kwamba hata tukianzisha Mamlaka, wanasiasa wataendelea kutumia kisingizio cha kuwakilisha wananchi kubadiri ushauri wa kitaalamu kwa manufaa yao. Mwisho wake utakuwa ni kuongeza mzigo kwa wananchi pasipo matokeo chanya.

So, kwa utaratibu huu sioni uchawi utakaofanywa na Mamlaka iwapo hata sasa Mwanasiasa anajua wazi kuwa ufinyu wa bajeti ndio unaokwamisha miradi mingi ya maendeleo, yet anakuja na BRN as if hiyo BRN itapata pesa toka mbinguni!!

ufinyu wa bajeti unaweza kusababishwa na kutopanga, na hata siku moja mwanasiasa hawezi kupanga maendeleo ya nchi. wao wanaona mambo katika jamii nyingine ukiyachukua na kuyaweka katika jamii yako kama yalivyo hayawezi kufanya kazi.

jamii unayoiona imefikia hatua fulani kuna hatua walizipia huko nyuma hivyo kwetu sisi hatuweka kuruka mara moja na kufikia hatua hiyo kama bado tuko mbali.

tunahitaji chombo ambacho hata mwanasiasa akisema tunataka kuendeleza kilimo kufikia kuyalisha mataifa ya jirani yote na kusafirisha ngambo ndani ya miaka 10, wao wataalamu wataangalia tuko wapi katika sekita ya kilimo na je tunaweza kufanya nini ili tutimize malengo hayo ndani ya mda mfumpi sana inavyowezekana.

fikiria tatizo la ajira, mwanasiasa kutengeneza ajira anafikiri ni swala la kutangaza nafasi za ajira lakini mchumi atakwambia kutengeneza ajira ni kuimarisha uchumi. dhibiti fedha zisitoke nje ya mipaka ya nchi yako. sisi kupitia usafirishaji kama magari na vipuri vyake, mafuta ya kuyaendeshea vyombo vya usafiri, vifaa vya electronic, na mabo mengine tunayoagiza nje yanaathiri uchumi wetu vibaya sana. lakini kuvikosa kabisa vitu hivi tutaathiri uchumi wetu vibaya sana hivyo tunahitaji balansi kwa maana tuagize kulingana na uchumi wetu, lakini bila udhibiti kila mtu anakusanya fedha ndani kimbilia china, dubai na kurundika vifaa hivi kwetu hata ambavyo hatuhitaji vinachukua fedha zetu. ukidhibiti hivi kasi ya ujenzi wa nyumba inaweza kuongezeka na ina maana ajira zaidi. angalia familia zenye kipato kizuri zinaweza kuwalipa watoa huduma wangapi kwa mwezi hivyo ukiweza kudhubiti fedha ikabaki uwezo wa kunua unaongezeka na hizo ndizo ajira zinavyotengenezwa.

angalia miradi ya maendeleo, kwa fedha za ndani ni asilimia ngapi tunazitoa kwa makampuni ya kigeni kutekeleza shughuli za maendeleo. je tunatambua kuwa hii ni njia moja wapo ya kudidimiza uchumi wetu kwa makampuni haya kutumika kutoa fedha hata zetu za ndani kuzipeleka nje. hivi tukiweka mkakati wa fedha za ndani kuzitoa kwa makampuni ya ndani kwanza tunatengeza ajira ngapi, je katika mzunguko wetu wa pesa tutabakiza shilingi ngapi ambazo zitaimarisha uchumi wetu.

je nani anaangalia haya? tunamikakati gani ya kulinda uchumi wetu ? tunahitaji chombo hiki kuangalia maswala ya kiuchumi kwa mapana sana na kufanya maamuzi au kutoa dira kwa wizara
 
Nafkiri ndc(national development Corporation) ndo inahusika na kuratibu mikakati yote ya maendeleo nchini

NDC inaonekana ilikuwepo lakini imejikita katika kuendeleza viwanda tu na kimsingi shirika lenyewe limekufa maana linaonekana lilianzishwa mwaka 1962 lakini viwanda vyote tulivyokuwa navyo huko nyuma vilifilisika hivyo nadhani kama sio limekufa basi litakuwa limelazwa muhimbili likiwa mahututi.

hapa mimi ninachokisema ni mamlaka ya kupanga mipango ya kimaendeleo ya taifa.

hebu angalia eti tumeunda shirika kubwa kama sido likapromoti kusuka vikapu, kutengeneza bidhaa za mianzi, na bidhaa za kipuuzi puuzi tu.

tunahitaji mamlaka ya kuweka mikakati ya kiuchumi ya kitaifa ambayo inaangalia sekita zote kwa pamoja na kutoa mwongozo.

mfano kuendeleza viwanda kunahitaji mitaji, kunahitaji promosheni, kunahitaji ulinzi wa kibiashara dhidi ya bidhaa zanje, kunahitaji incetives kuhamasisha uanzishaji, kunahitaji miundo mbinu ya usafirishaji, umeme, maji na nishati zote.

vitu vyote hivi vinafanyika katika wizara tofauti hivyo ukiunda shirika ukaliweka wizara moja haliwezi kufanya kazi.

inabidi kuwe na chombo kilicho juu ya wizara kinachoweza kupanga kuwa tunataka kufanya uchumi wetu uwe wa viwanda kwa nchi jirani na sisi wenyewe tuache kutegemea asia.

chombo hiki kitaweka mkakati wa kutekeleza jambo hili kwa kuipangia kila wizara jukumu lake na kujua ni wakati gani tufanye nini.

baada ya hicho chombo kinachoratibu mipango ya serikali ya kimaendeleo ndipo chombo kama NDC kinaweza kufanya kazi kwa chenyewe kujikita katika kuhakikisha viwanda vinajengwa kwa kuwatafuta wawekezaji wa ndani na nje na kuwaelezea serikali imeweka mazingira gani.

lakini kama tunaweza kudhani kama nchi fulani walianzisha shirika la kuendeleza viwanda huku sisi tukiwa hatuna miundo mbinu na tukadhani kulianzisha tu nchi yetu inakuwa na viwanda huo ni upofu katika mambo ya utawala wa nchi.
 
Back
Top Bottom