Tunaoacha kucheza kamari (bonanza au dubwi) tukutane hapa

marandu2010

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2010
Posts
1,201
Reaction score
446
Habari za saa hizi wakuu,

Moja kwa moja kwenye mada,mm nimeathirika na uraibu(addiction) wa kucheza mashine ya kamari (bonanza au dubwi), hasara ninayopata ni kubwa sana. Nimefeli malengo mengi. Sasa leo hii tarehe 16/6/2021, ninaacha rasmi, najua ni vigumu lakini inawezekana.

Naomba kama kuna yeyote kama mimi mwenye nia ya dhati ya kuacha kucheza bonanza tukutane hapa katika uzi huu.

Safari inaanza, DAY 1.

Karibuni
 
Jinsi nilivyoacha vilevi vitatu ikiwemo betting

 
Siku niko bar fulani nakula bia, nikaomba token za 2000, zikaliwa, nikaomba tena elfu mbili zikaliwa, nikaona ngoja nichukue token za buku ili niwe nimeliwa elfu 5, banaeee nikashusha kama 46000 na silesile kadhaa...nikahama bar...kamari siwezi acha...kama ni makato nimecheza sana mpaka nilishaliwa simu ya sista angu
 
Uraibu wa pull table unanitesa sana unanimalizia sana pesa mpaka hapa naandika niko kwenye pull.
Kila nikipita popote palipo na pull lazima nipite, najipa matumain kuwa kuna siku nitaacha lakini wap pengne nafrahia coz inanisogeza kuna wkat nakosa mchongo ila nikicheza nakuwa na uhakika wa kula. One day nitaacha.
 
huko nako sio kwepesi
Unacheza hiyo mashine za wachina wanazoweka mitaani? Mimi kwa Tanzania kwenye mambo ya michezo ya kubahatisha naamini hii michezo yenye matokeo halisi eg kubeti kwenye mpira nk. Haya mambo ya mashine au bahati nasibu za kubahatisha namba sina imani nazo kabisa kabisa. Nchi yetu ina fiksi nyingi sana.
 
Daahh haya makitu nahisi yana uchawi ndani yake, maana kila nikiacha ninarudi tena. Tupeane uzoefu umetumia njia gani kuacha

Sent from my TECNO KA7 using JamiiForums mobile app
tuanze safari kaka,mm siku ya pili leo,cha kwanza ni kuamini ukweli ya kwamba dubwi halina faida kwa mchezaji bali kwa mmiliki.kama hauamini jumlisha hela unazoliwa linganisha na unazokula.pili kuamua kwa dhati kuacha.tatu kaa mbali na vichocheo,nne tafuta vitu vingine vya kufanya.anza sasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…