Tunaoanza Kuaga Kesho tafadhali tumia Sekunde Moja tu unasepa, Jicheleweshe upigwe Mbata ya maana au Kofi ukahadithie vizuri

Tunaoanza Kuaga Kesho tafadhali tumia Sekunde Moja tu unasepa, Jicheleweshe upigwe Mbata ya maana au Kofi ukahadithie vizuri

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Kuna Watanzania baadhi mna Mambo ya ajabu na Kipuuzi sana yaani muda wa Kuaga Marehemu ( Maiti ) ukifika Mtu anataka kuanza sijui kupiga Picha na Kumgusa Marehemu huku akiijua kuwa nyuma yake kuna Msururu wa Watu.

Nawatahadharisheni mapema tu Kesho mtakaoanza Kumuaga Marehemu pale Uhuru ( Shamba la Bibi ) acheni Mbwembwe kwani wanaosimamia Zoezi hilo zima ni Wazee wa Kazi kutoka Kikosi Maalum.

Sasa Wewe anza kwenda kwa mwendo wa Bwana na Bibi Harusi huku ukipiga Picha na kushika Jeneza lake kisha ujikute unapigwa Mbata ya maana au Kofi la Kimedani ( Kijeshi ) kisha Maumivu ya Kuugulia ukaanze kuyasikia ukiwa Sebuleni Kwako na Mkeo.

Binafsi kwakuwa najijua na sitaki Mbata au Kofi nitaagia Lugalo ( kwa kusimama barabarani ukipitishwa ) tena kwa nje pale jirani na Duka la Kuuza Majeneza ya Matajiri ( Kishua ) nikimaliza napotea kwa mwendo wa Kiukakamavu.
 
Waambie mkuu. wasije wakatembea kama wako kwenye bufee la msosi
 
Mna ingilia kazi zetu wapiga picha mama .samia shughulikia hawa

SUBIRI KIDOGO
 
Unaweza ona mtu anatoka huko analia kwa nguvu zote ukadhani ni ana machungu kumbe kelbu imemuingia...

Kweli Arif!!

Ila chalii yangu Ni wewe kweli manake sioni Kama unavyoandikaga


"Ngoja watupe mwongozo"

Cc(sijui Nani)

Umebadilika na serikali?
 
Back
Top Bottom