Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
Umekuwa nasi bega kwa bega. Hakuna kipindi kama cha awamu ya tano ambacho sisi wafanyabiashara wakubwa tuliishi kwa wasiwasi na mashaka
Hili la kuwajulisha watanzania kuwa vitu vitapanda bei limenipa faraja sana. Maana sasa waelewe kuwa vita vya Russia na Ukraine vinaiathiri dunia sana. Mafuta ya Vyombo vya Usafiri, ya Kula, ya kupaka. Sabuni, Sukari Mchele, Unga, Nyama, Maharagwe n.k lazima vitaathirika.
Awamu ya tano ingetaka kutumia ubabe kuzuia sisi wengine kupandisha bei. Tulinyanyasika sana sisi wafanyabiashara wakubwa. Lakini sasa tunajisikia amani na tunarudisha kilichoibwa na kupotezwa.
Mwaka 2025 hauna Upinzani. Ni wewe tu. Endelea kutukumbuka pia katika kodi....tupunguzie kodi mama. Tunaingiza mizigo mikubwa kodi ipunguzwe. Kodi inaweza ingizwa kwenye tozo na makato mengine. Tuliteseka sana.
Tunashukuru sasa Watanzania watakuwa tayari kukabiliana na bei zetu hizi pasipo manung'uniko au lawama. Maana wanapenda sana lawama.
Hili la kuwajulisha watanzania kuwa vitu vitapanda bei limenipa faraja sana. Maana sasa waelewe kuwa vita vya Russia na Ukraine vinaiathiri dunia sana. Mafuta ya Vyombo vya Usafiri, ya Kula, ya kupaka. Sabuni, Sukari Mchele, Unga, Nyama, Maharagwe n.k lazima vitaathirika.
Awamu ya tano ingetaka kutumia ubabe kuzuia sisi wengine kupandisha bei. Tulinyanyasika sana sisi wafanyabiashara wakubwa. Lakini sasa tunajisikia amani na tunarudisha kilichoibwa na kupotezwa.
Mwaka 2025 hauna Upinzani. Ni wewe tu. Endelea kutukumbuka pia katika kodi....tupunguzie kodi mama. Tunaingiza mizigo mikubwa kodi ipunguzwe. Kodi inaweza ingizwa kwenye tozo na makato mengine. Tuliteseka sana.
Tunashukuru sasa Watanzania watakuwa tayari kukabiliana na bei zetu hizi pasipo manung'uniko au lawama. Maana wanapenda sana lawama.