Tunataka Kujenga Taifa la Wajenga Hoja, au la Taifa la Wapiga Kelele?

Tunataka Kujenga Taifa la Wajenga Hoja, au la Taifa la Wapiga Kelele?

Azizi Mussa

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2012
Posts
9,186
Reaction score
7,492
Wadau salaam,

Kwa kawaida uamuzi wa kujenga taifa lenye watu wa aina fulani u mikononi mwa wananchi wenyewe na wananchi ni mimi na wewe. Kwa hiyo mchango wako wewe na mwingine na mwingine (uwe hasi au chanya) unachangia kujenga jamii ya aina fulani na hatimae taifa la aina fulani.

Kwa kawaida jambo lolote liwe jema au baya, huanza kama fikra, hutolewa kama hoja, huchambuliwa na kisha hutekelezwa ili kuleta matokeo ya aina fulani.Kitendo cha mtu kuamua kutojilazimisha kufikiri vya kutosha, humfanya asiwe na mawazo yenye mtiririko mzuri ndani ya kichwa chake , kitu kinachomfanya anapoongea ashindwe kutoa hoja na ajikute akipiga kelele tu ambazo kimsingi hazina athari yeyote ya maana katika jamii.

Kasi ya wengi wetu kupiga kelele badala ya kujibu hoja pale tunapoulizwa ni kwanini vyama vyetu havijafanya jambo fulani ambalo vilitakiwa vilifanye, au kwa nini vimefanya jambo fulani kinyume na ilivyotakiwa kufanya au kwani nini vimefanya jambo ambalo halikutakiwa kufanywa kabisa, imeongezeka sana!.

Inavyoonekana tatizo hili kwa kiwango kikubwa huchangiwa na wengi wetu kuamua kutochambua mambo tunayoyaona, kuyasikia au kuyasoma amma kwa makusudi, kwa kusikiliza ya kuambiwa tu badala ya kuchanganya na zetu, au kwa kukosa uwezo (ni jambo la mjadala), au kwa uzembe.Ni kitu cha kawaida sana siku hizi chama, mwanachama au kiongozi anapoulizwa swali, badala ya kujibu swali huibuka na kuanza kupiga kelele.Mara utasikia mnafiki wewe! msaliti wewe,! mburura, kachukue hela yako! wewe mwanamke au mwanaume n.k.

Kwa kuwa taifa hujengwa na wewe na mimi, na kwa kuwa mazoea hujenga tabia; basi ni hiari yetu kuchagua kujenga Taifa la wapiga kelele! kwa kujizoeza kupiga kelele mbele ya hoja au taifa la wajenga hoja kwa kujizoeza kukabiliana na hoja zinapojitokeza.

Wanasema dunia ni yetu chaguo ni letu na akili kumkichwa.

"Let Us Urgue not Shouting, for Our love to The Nation, today and Tomorrow!"
 
Kumbuka kuwa Kupanga ni kuchagua, halafu viongozi wa nchi ni reflection ya wananchi wake.

Kila unaloona Tanzania ni uchaguzi wetu wenyewe na ni reflection ya tabia zetu. Miaka ya sabini tulikuwa na fikra pana sana za mweleko kama ambavyo mwimbaji huyu anavyeoimba, leo hii siamaini kama kuna hata mwimbaji wa kitanzania anayeweza kutunga na kuimba wimbo wenywe ujumbe kama huu.
 

Attachments

Kumbuka kuwa Kupanga ni kuchagua, halafu viongozi wa nchi ni reflection ya wananchi wake.

Kila unaloona Tanzania ni uchaguzi wetu wenyewe na ni reflection ya tabia zetu. Miaka ya sabini tulikuwa na fikra pana sana za mweleko kama ambavyo mwimbaji huyu anavyeoimba, leo hii siamaini kama kuna hata mwimbaji wa kitanzania anayeweza kutunga na kuimba wimbo wenywe ujumbe kama huu.

Na kibaya zaidi ni kwamba kuna watu wengi sana hawaelewi wala wakiambiwa hawataki kuamini kuwa viongozi hawa hawa tulionao ambao badala ya kujenga hoja wanapiga makekele , matusi na fitna ni taswira ya jamii yetu wenyewe kwa kuwa wanapatikana kwa bahati nasibu kutoka kwenye jamii yenyewe.

Vile vile hawa wanajamii , mfano walioko kwenye forums, ambao kazi yao ni makelele ni reflection ya jamii vile vile na kutoka kwao watatoka viongozi watakaoingoza Tanzania. Kwa hiyo ndio maana nasema kupanga ni kuchagua maana viongozi wetu wanatokana na jamii yetu hii hii.
 
Tanzania inahitaji watu wenye kuangalia yale ambayo hayajatokea na kuyapima kuwa yatakapotokea itakuwaje, na kifanyike kitu gani kuzuia mabaya yasitokee na mazuri yatokee haraka. Kusubiri matukio mabaya yatokee ndipo tupige kelele kila mara tunakuwa tumeshachelewa, na tunapolala kusubiri matukio mazuri yatokee yenyewe wakati mwingine hukuta nchi nyingine zimeshazuia hayo mazuri yasitokee hapa kwetu bali yaende huko kwao!!
 
Tanzania inahitaji watu wenye kuangalia yale ambayo hayajatokea na kuyapima kuwa yatakapotokea itakuwaje, na kifanyike kitu gani kuzuia mabaya yasitokee na mazuri yatokee haraka. Kusubiri matukio mabaya yatokee ndipo tupige kelele kila mara tunakuwa tumeshachelewa, na tunapolala kusubiri matukio mazuri yatokee yenyewe wakati mwingine hukuta nchi nyingine zimeshazuia hayo mazuri yasitokee hapa kwetu bali yaende huko kwao!!
Mkuu Tanzania hakuna uhaba wa mawazo, kuna uhaba wa watu wanaosikiliza mawazo ya wenzao

Angalia bungeni kwa kuanzia. Kuwa na mawazo tofauti kunapelekea 'kunyimwa' huduma
Kwamba, mtu akisema tuanze na maji kisha umeme, huyo ni msaliti kwasababu wapo wanaosema tuanze na umeme kisha maji. Hakuna kusikilizana

Chanzo halisi cha matatizo na nasikitika kusema hili ni kitu kinachoitwa CCM
Watu walionyesha namna gani wizi unafanyika. Kilichofuata ni kuandama mitandao

Suala kama la Escrow, wapo walioitwa Tumbili, wanatumiwa na nchi za nje n.k.
Miaka 16 waliosema hayo wanaunga mkono waliyoyakataa tena kwa matamko makali.

Haya yanafanywa na watu wanaoitwa CCM na ndilo chimbuko la kuvia nchi hii

Watu walisema lazima kuwe na mipango ya kitaifa si ya watu.
Tukasikia elimu kwanza, ghafala Kilimo kwanza, sasa hapa kazi.

Hakuna tathmini inayofanyika kupima kama Taifa lime achieve kile kilichtangulia

Kwa mtazamo huo taifa limegeuka kuwa la matukio.
Leo watu wanazungumzia Tanzania ya viwanda.

Mwaka jana tulikuwa na Kilimo kwanza, miaka michache elimu bure
Katika hali hiyo tumekuwa watu wa matukio na siyo maono

Hatuwezi kukwepa hali hiyo lazima tufumue mfumo uliovia akili zetu na kuweka mpya
Tuangalie mwongozo wetu wa miaka 50 kama utatuvusha miaka 50 mingine ijayo

I mean tuanze na katiba inayotoa mwongozo, tuwe na sera za kitaifa na mipango ya Taifa
 
Ukitaka kupima kiwango cha maendeleo cha nchi yoyote ile angalia pia namna wananchi wake wanavyo-enenda katika mawazo, maneno na matendo. Utagundua kwamba maendeleo ya nchi yana-reflect pia kwenye mwenendo wa wananchi wake kwa mawazo, maneno na matendo.
 
Mfano kujadili sura za watu tunakuwa tunatakiwa kuifanya hivyo?
Naona unakwepa hoja, Kujadili sura za watu hiyo si hoja ni matusi na huwezi kuiita hoja kwasababu unaipa uhalali usiokuwepo. Kama ndilo unafikiri basi mada hii haina maana

Nilidhani kujadili hoja ni mambo yanayotugusa kama Taifa.
Hapo ndipo hoja yangu inaingia, hatuwezi kujadili hoja ikiwa zimewekewa uzio wa kutojadiliwa

Nitakupa mifano, Bungeni kuna hoja ya nyumba zisizotakiwa kujadiliwa. Utajadili hoja gani hapo?
Pili, kuna chombo tumeambiwa ni cha kijeshi, hatutakiwi kujadili. Tutajadili hoja gani hapo?
Tatu, tumejadili kwanini mikutano ya siasa izuiliwe katika muktadha wa katiba. Nani amejibu hilo?
Nne, watu walisema Escrow ni uhalifu, tukaambiwa ni pesa za serikali. Leo tujadili nini ikiwa wamekubali?
Tano, tukajadili kuhusu mfumo wetu wa katiba, tukaambiwa haipo katika ilani , tujadili nini?

Orodha ni ndefu, ninachotaka kukuambia ni kuwa hatuwezi kujadili hoja ikiwa zina uzio

Matokeo yake inawalazimu watu wapige kelele tu maana hakuna anayewasikiliza.

Sasa hoja ya sura za watu ni dhaifu sana kiasi kwamba sikujua hilo ndilo lengo la mada
Hivi kuna ulazima gani wa kujadili sura ikiwa unajua hakuna maana ya kufanya hivyo?
 
Tanzania inahitaji watu wenye kuangalia yale ambayo hayajatokea na kuyapima kuwa yatakapotokea itakuwaje, na kifanyike kitu gani kuzuia mabaya yasitokee na mazuri yatokee haraka. Kusubiri matukio mabaya yatokee ndipo tupige kelele kila mara tunakuwa tumeshachelewa, na tunapolala kusubiri matukio mazuri yatokee yenyewe wakati mwingine hukuta nchi nyingine zimeshazuia hayo mazuri yasitokee hapa kwetu bali yaende huko kwao!!
Kichuguu ishu kubwa kwetu hasa wanaoitwa vijana wa Leo, ni uvivu na kupenda uovu kuliko mema.

Tumezoea ubinafsi na uongo yaani mtu yuko radhi adanganye ili kupata chochote kitu, tukasahau kabisa maslahi ya taifa


Kibaya zaidi vijana kwa ubinafsi wananunulika kama njugu, hakuna mwenye haya. Na hawa ndio hodari wa kupiga kelele

Sent from my Royale A1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Tanzania hakuna uhaba wa mawazo, kuna uhaba wa watu wanaosikiliza mawazo ya wenzao

Angalia bungeni kwa kuanzia. Kuwa na mawazo tofauti kunapelekea 'kunyimwa' huduma
Kwamba, mtu akisema tuanze na maji kisha umeme, huyo ni msaliti kwasababu wapo wanaosema tuanze na umeme kisha maji. Hakuna kusikilizana

Chanzo halisi cha matatizo na nasikitika kusema hili ni kitu kinachoitwa CCM
Watu walionyesha namna gani wizi unafanyika. Kilichofuata ni kuandama mitandao

Suala kama la Escrow, wapo walioitwa Tumbili, wanatumiwa na nchi za nje n.k.
Miaka 16 waliosema hayo wanaunga mkono waliyoyakataa tena kwa matamko makali.

Haya yanafanywa na watu wanaoitwa CCM na ndilo chimbuko la kuvia nchi hii

Watu walisema lazima kuwe na mipango ya kitaifa si ya watu.
Tukasikia elimu kwanza, ghafala Kilimo kwanza, sasa hapa kazi.

Hakuna tathmini inayofanyika kupima kama Taifa lime achieve kile kilichtangulia

Kwa mtazamo huo taifa limegeuka kuwa la matukio.
Leo watu wanazungumzia Tanzania ya viwanda.

Mwaka jana tulikuwa na Kilimo kwanza, miaka michache elimu bure
Katika hali hiyo tumekuwa watu wa matukio na siyo maono

Hatuwezi kukwepa hali hiyo lazima tufumue mfumo uliovia akili zetu na kuweka mpya
Tuangalie mwongozo wetu wa miaka 50 kama utatuvusha miaka 50 mingine ijayo

I mean tuanze na katiba inayotoa mwongozo, tuwe na sera za kitaifa na mipango ya Taifa
Nguruvi3 nijaribu kuwaza tuu. Hivi agriculture development program iliyo asisiwa na Ben, vipi matokeo yake? Na yako wapi? Je kilimo kwanza nacho matokeo yake ni yepi? Haya Sasa Tanzania ya viwandani nini mwitikio wetu kwenye kilimo ambacho ndivyo kinacholisha viwanda?

Tuyaache hayo, hivi tumewah kuwa na kipaumbele? Kama taifa?

Najaribu kuwaza hivi Leo hii waziri wa kilimo atahamasisha kilimo cha umwagiliaji, hapo hapo waziri wa nishat ataenda kwenye vyanzo vya maji na kuhamasisha watu kutunza vyanzo vya maji ili kuconserve yakafue umeme, pembeni yake yupo wazir wa viwanda anataka umeme upelekwe viwandani ili viwanda vizalishe, tanesco nao hawatabaki nyuma wataskia kupandishwa kwa gharama za umeme kwasababu wanstumia gharama kubwa kuzalisha, wazir wa nishat atasema kwasasa tuna gesi tunaileta adi dar so umeme utapungua bei Ewura nao watajibu gharama za umeme zikipungua tanesco itakufa kwani deni inalodaiwa kwa ujenzi wa Bomba la gesi ni kubwa sana na wanatakiwa walilipe.

Mshauri wa uchumi alishauri Bomba ilijengwa kabla hajatathmini gharama zitakazo tumika na malipo yatakayoongezeka kwa mteja.

Nemc nao watakuja na utunzaji wa mazingira watahamasisha kupanda miti. Na watagomea miti isikatwe


Sasa nkajiuliza hivi can't we have kipaumbele cha taifa and each organ ijitahidi Ku fit in kwayo? Badala ya kuwa na kauli kinzani tena toka viongozi wetu wa juu tena tunao wa amini?


Sent from my Royale A1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom