Tunawasaidaje wanawake ambao wanapitia kwenye ukatili lakini hawaelewi kama wanachokipitia ni ukatili?

Tunawasaidaje wanawake ambao wanapitia kwenye ukatili lakini hawaelewi kama wanachokipitia ni ukatili?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Huyu mama ni tukio lililotokea Dec 27, mkoani Arusha ambapo mama huhu akiwa mjamzito alichezea kichapo cha mbwa koko kutoka kwa mume wake, na baada ya haya yote aliomba polisi wamkanye mume wake apunguze kumpiga kwakuwa bado anampenda. Uzi wa tukio hili uko hapa.


Nimekutana na video hii ikanikumbusha jambo kutana kwa dada ambaye namjua, unaweza kusema ni mtu wa karibu kiasi na mimi, ambaye hali yake haipishani sana na dada huyo hapo.

Hapa ndio nimepata swali la kumuuliza Waziri Dkt. Gwajima D, mtu kama huyu unamsaidiaje ambayo anapitia ukatili lakini haoni kama anaatahili kutendewa vyema na huyo aliyemfanyia hivyo achukuliwe hatua?

Huyu dada ambaye namjua naye utasema karogwa. Mpenzi wake amekuwa akimpiga mara kwa mara, wanasuluhishwa wanaendelea na maisha maana ameshashauriwa mara nyingi amuache mwanaume huyo lakini ni kama unatwanga maji kwenye kinu!

Sasa siku hiyo (kama miezi mitatu hivi iliyopita) alipigwa vibaya sana kiasi kwamba sasa hivi amepata tatizo la kuanguka kama degedege si degedege, kuzimia si kuzimia, alimpigiza kichwa wakati anamtembezea kichapo, lakini yule mpuuzi anakwambia anaogopa kwenda kumripoti polisi sababu anamuonea huruma atakamtwa.... mara aaah atabadilika tu akinioa 😩😩😩.

Baada ya kuchezea kichapo hivyo hakuweza kwenda hospitali sababu pia alikuwa kayumba kiuchumi. Kwahiyo tatizo hilo limeenda bila kuchekewa akiwa hajui nini kinamfanya mpaka anakuwa anaanguka hivyo without warning. Nahofia inaweza kuwa something deadly, ama siku likatokea la kutokea akapigwa na kufanywa kilema au akamuua kabisa.

Sasa kwenye mazingira kama haya unamsaidiaje mtu kama huyu apate msaada stahiki na anayefanya ukatili huo kuchukuliwa hatua stahiki? Dkt. Gwajima D?
 
Ni vigumu kumsaidia kama hatoi ushirikiano mnaweza kwenda kufungua kesi halafu mtendwa akakataa kua hajatendewa. Ukiweza kupata ushahidi wa video nazan itapendeza hapo unaweza kwenda kumshiki mtenda bila hata kumtegemea mtendwa.
 
Sasa,Ubeijing na uanaharakati wote unaowapendelea wanawake lakini bado hamuitwai nafasi hiyo?Uelimishaji wa stadi, haki,wajibu na mienendo ya maisha ufundishwe mashuleni ili kuwajengea kujiamini,kujitambua na uwajibikaji/kuchukua hatua.Sheria nazo zitumike kwa sababu zipo tayari.Wazazi na walezi nao wawe wanatoa maelekezo chanya kwa watoto.
 
sasa yeye mwenyewe ameoma polisi wamshauri mume wake apunguze kupiga kwakuwa anampenda, yeye hayaoni hayo manyanyaso bali anauona upendo
 
Ni vigumu kumsaidia kama hatoi ushirikiano mnaweza kwenda kufungua kesi halafu mtendwa akakataa kua hajatendewa. Ukiweza kupata ushahidi wa video nazan itapendeza hapo unaweza kwenda kumshiki mtenda bila hata kumtegemea mtendwa.
Nilifanikiwa kupata picha baadhi, ndio maana nimetag Dkt. Gwajima D atupe mwongozo, inapotokea hali kama hii inatakiwa tuchukue hatua gani, nina imani kutakuwa na namna
 
Sasa,Ubeijing na uanaharakati wote unaowapendelea wanawake lakini bado hamuitwai nafasi hiyo?Uelimishaji wa stadi, haki,wajibu na mienendo ya maisha ufundishwe mashuleni ili kuwajengea kujiamini,kujitambua na uwajibikaji/kuchukua hatua.Sheria nazo zitumike kwa sababu zipo tayari.Wazazi na walezi nao wawe wanatoa maelekezo chanya kwa watoto.
Ndio hali imeshatokea kama nilivyoelezea hapo, mtu huyo anasaidika vipi?
 
sasa yeye mwenyewe ameoma polisi wamshauri mume wake apunguze kupiga kwakuwa anampenda, yeye hayaoni hayo manyanyaso bali anauona upendo
Ndio inaishia hapo? Chukulia ni mtu wako wa karibu, unamsaidiaje kwenye hali kama hii ukiangalia na mfano nilioongezea hapo?
 
Kuna makabila, mwanamke akipigwa ndio anaona anapendwa ,eti mmewe ana wivu nae, Mara huko...pumbavu kabisa.
Kibinadamu,kwenye mapenzi mtu anapenda aonewe wivu ndio anahisi anapendwa.
 
Sasa kwenye mazingira kama haya unamsaidiaje mtu kama huyu apate msaada stahiki na anayefanya ukatili huo kuchukuliwa hatua stahiki?
Mkuu kuna tatizo linaitwa ONEitis,
Hii ni ile hali ya mtu kuamini kuwa hakuna mbadala wa aliyenaye kwenye mahusiano, Yaani anaamini kuwa akimuacha huyo hawezi kupata mwanaume mwingine wa kuishi nae, kwenye Dunia hii haamini kuwa kuna maisha nje ya huyo mwanaume. Yeye aliumbwa kwa ajili ya huyo kidume na kidume aliumbwa kwa ajili yake.

Vilevile kuna kitu kinaitwa Sunk-cost-fallacy,
Hii ni hali ya mtu kushindwa kuchukua maamuzi na kuendelea kubaki kwenye mazingira aliyopo(hata kama anaumia,anateseka,anataabika) kwasababu anakuwa amewekeza sana kwenye hilo jambo(mahusiano). Yaani anaona bora aendelee kuumia kuliko akiondoka atapoteza vingi alivyowekeza hapo.

Vilevile pia kuna hii pia Stockholm Syndrome,
Hii ni hali ya mtu kuwa na hisia chanya kwa mtu aliyemtesa kwa kipindi kirefu, Yaani mtu anateswa ila bado anakuwa upande wa anayemnyanyasa (mfano aliposema akienda police anamuonea huruma mumewe atakamatwa).

USHAURI.
Bidada ana tatizo la kisaikolojia, Yaani kuna vitu anaviamini ambavyo kwenye Dunia ya uhalisia havipo sawa na anachoamini yeye, anapaswa atenganishwe kwa muda na huyo mwanaume na kisha akutane na washauri wa kisaikolojia wazuri ndio ataona kuwa hayo ni manyanyaso.
Anaweza ondoka hapo kwa Mwanaume kwa gia ya kwenda kucheki matibabu ya hilo tatizo la kuanguka.

Huyo Kidume mtesaji atashughulikiwa baada ya Mwanamke kuwa sawa, Otherwise ukitaka umshughulikie mwanaume sasa hivi, huyo mwanamke atakuwa upande wa Mumewe na hamna mtakachopata. Labda UBABE utumike, mvunje sheria kidogo.

Thank you.
Cc: Dkt. Gwajima D
 
Kuna makabila, mwanamke akipigwa ndio anaona anapendwa ,eti mmewe ana wivu nae, Mara huko...pumbavu kabisa.
Kibinadamu,kwenye mapenzi mtu anapenda aonewe wivu ndio anahisi anapendwa.
Si bora angekuwa anatoka huko tukajua namna ya kumsaidia kwa kuanzia na mzizi kabisa, yaani ukimuona huyu dada utaamini uchawi upo
 
Mkuu kuna tatizo linaitwa ONEitis,
Hii ni ile hali ya mtu kuamini kuwa hakuna mbadala wa aliyenaye kwenye mahusiano, Yaani anaamini kuwa akimuacha huyo hawezi kupata mwanaume mwingine wa kuishi nae, kwenye Dunia hii haamini kuwa kuna maisha nje ya huyo mwanaume. Yeye aliumbwa kwa ajili ya huyo kidume na kidume aliumbwa kwa ajili yake.

Vilevile kuna kitu kinaitwa Sunk-cost-fallacy,
Hii ni hali ya mtu kushindwa kuchukua maamuzi na kuendelea kubaki kwenye mazingira aliyopo(hata kama anaumia,anateseka,anataabika) kwasababu anakuwa amewekeza sana kwenye hilo jambo(mahusiano). Yaani anaona bora aendelee kuumia kuliko akiondoka atapoteza vingi alivyowekeza hapo.

Vilevile pia kuna hii pia Stockholm Syndrome,
Hii ni hali ya mtu kuwa na hisia chanya kwa mtu aliyemtesa kwa kipindi kirefu, Yaani mtu anateswa ila bado anakuwa upande wa anayemnyanyasa (mfano aliposema akienda police anamuonea huruma mumewe atakamatwa).

USHAURI.
Bidada ana tatizo la kisaikolojia, Yaani kuna vitu anaviamini ambavyo kwenye Dunia ya uhalisia havipo sawa na anachoamini yeye, anapaswa atenganishwe kwa muda na huyo mwanaume na kisha akutane na washauri wa kisaikolojia wazuri ndio ataona kuwa hayo ni manyanyaso.
Anaweza ondoka hapo kwa Mwanaume kwa gia ya kwenda kucheki matibabu ya hilo tatizo la kuanguka.

Huyo Kidume mtesaji atashughulikiwa baada ya Mwanamke kuwa sawa, Otherwise ukitaka umshughulikie mwanaume sasa hivi, huyo mwanamke atakuwa upande wa Mumewe na hamna mtakachopata. Labda UBABE utumike, mvunje sheria kidogo.

Thank you.
Cc: Dkt. Gwajima D
Asante kwa maoni na ushauri huu mzuri Mkuu
 
Back
Top Bottom