Tunaweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu, viongozi wengi wa zamani wanateuliwa tena na tena kwenye awamu mpya

Tunaweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu, viongozi wengi wa zamani wanateuliwa tena na tena kwenye awamu mpya

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Nafikiri tatizo kubwa la nchi yetu ni kukosa ubunifu na kutokuwa na mifumo imara na hivyo kupelekea kila kiongozi mkuu ajaye kuanza upya.

Awamu iliyopita ilikuwa na viongozi ambao kama Tanzania ingekuwa nchi iliyokomaa kifikra na kidemokrasia basi viongozi wakuu karibu wote wangepaswa kuachia ngazi na kuwajibishwa kwa makosa mengi yaliyotendeka.

La kushangaza viongozi wengi wa awamu iliyopita wameendelea kuteuliwa katika nafasi mbalimbali wakati huo huo tukifikiri tunaweza kuleta mabadiliko kwa kutumia watu ambao wamekuwa wakishindwa siku zote. Tuweke mvinyo mpya kwenye viriba vipya.
 
Alishasema yeye na wa awamu iliyopita ni kitu kimoja, CCM ni ile ile. Hauwezi kumpaka punda rangi ili ageuke kuwa pundamilia.
 
Msitu mpya nyani walewale, ubaya sasahivi hukunamtu wa kuwapigia kelele za hoja kinzani bungeni
 
Wakiwa maofisini hawa wazee wanaanza kuhimiza vijana wajiajiri wakati wao Wana miaka ya kustaafu (60+) lkn bado wanaomba kuteuliwa.
 
CCM ni ukoo mmoja! Ukoo wa fisi. Siku ya kutoka madarakani (iwe ni kupitia sanduku la kura au kwa kutumia mtutu wa bunduki au kwa kutumia mapinduzi ya jeshi/nguvu ya umma), ndiyo itakuwa siku ya kweli ya uhuru wa Mtanzania.
 
Ndo makosa ya mama.Wengi hawakuteuliwa kwa weledi bali kwa cv ya kumfurahisha mwendazake.ukabila,udini, juhudi binafsi ya kuwaumiza wapinzani,nk
 
Nafikiri tatizo kubwa la nchi yetu ni kukosa ubunifu na kutokuwa na mifumo imara na hivyo kupelekea kila kiongozi mkuu ajaye kuanza upya....
Lazima kiriba kipasuke!!!
 
Back
Top Bottom