Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 3,092
- 5,386
Pamoja na kazi nzuri ya Serikali ya kuboresha uchumi na miundombinu,
Nafikiri ipo haja sasa ya kuja na mpango mkakati wa kufufua shirika letu la posta kwani lina uwekezaji mkubwa wa miundo mbinu karibu Nchi nzima wa Mabilioni iliyojengwa kwa kodi za wananchi
Kwanini tusije na mpango mkakati na unaoeleweka wa kodi kwa bidhaa zinazopita posta, hasa kwa hizi bidhaa moja moja hadi tano hivi ambazo ndizo huingizia wenzetu pesa nyingi za kuendesha Shirika.
Hizi formula za kodi zilizopo kwa sasa sio rafiki lakini pia, sio rahisi kwa mteja kuzielewa zinafanya hata mtu asitake kuwatumia kwani hata ukiagiza Bidhaa nje ya Nchi huwezi hata kukadiria kodi itakuwa kiasi gani na ndio hukaribisha mazungumzo pale mzigo unapofika.
Mf; unatumiwa tu zawadi ya viatu/raba unaambiwa kodi 115,000, unatumiwa zawadi ya kasimu ka laki tano, unaambiwa kodi laki 4 nk nk nk hata Wazungu wanakata tamaa kutumia shirika letu kwani wanapotumia watu wa kawaida vizawadi vya kuwasaidia hushindwa kulipia kodi ya kuvitoa hadi aliyetuma tena ajulishwe achangie...
Naona kama tunang’ang’ania kodi kubwa ambayo hata hatuipati tunaacha shirika la Mabilioni linafilisika na kupoteza ajira kwa maelfu za wafanyakazi ambao nao wanalipa kodi kubwa
Nafikiri ipo haja sasa ya kuja na mpango mkakati wa kufufua shirika letu la posta kwani lina uwekezaji mkubwa wa miundo mbinu karibu Nchi nzima wa Mabilioni iliyojengwa kwa kodi za wananchi
Kwanini tusije na mpango mkakati na unaoeleweka wa kodi kwa bidhaa zinazopita posta, hasa kwa hizi bidhaa moja moja hadi tano hivi ambazo ndizo huingizia wenzetu pesa nyingi za kuendesha Shirika.
Hizi formula za kodi zilizopo kwa sasa sio rafiki lakini pia, sio rahisi kwa mteja kuzielewa zinafanya hata mtu asitake kuwatumia kwani hata ukiagiza Bidhaa nje ya Nchi huwezi hata kukadiria kodi itakuwa kiasi gani na ndio hukaribisha mazungumzo pale mzigo unapofika.
Mf; unatumiwa tu zawadi ya viatu/raba unaambiwa kodi 115,000, unatumiwa zawadi ya kasimu ka laki tano, unaambiwa kodi laki 4 nk nk nk hata Wazungu wanakata tamaa kutumia shirika letu kwani wanapotumia watu wa kawaida vizawadi vya kuwasaidia hushindwa kulipia kodi ya kuvitoa hadi aliyetuma tena ajulishwe achangie...
Naona kama tunang’ang’ania kodi kubwa ambayo hata hatuipati tunaacha shirika la Mabilioni linafilisika na kupoteza ajira kwa maelfu za wafanyakazi ambao nao wanalipa kodi kubwa