Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anajaribu kuwadaganya, mpotezee

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu anajaribu kuwadaganya, mpotezee

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
324
Reaction score
649
MGOMBEA WA CHADEMA MH TUNDU ANTIPAS LISU, KAMA HAELEWI!


Na Elius Ndabila
0768239284


Leo nikiwa napitia mitandaoni nimekutana na Twitter ya Mh Lissu ambayo imepambwa na Picha ya Mh Rais Dkt Magufuli na Naibu Spika Mh Dkt Tulia Ackson. Kwenye twitter hii Mh Lisu ameandika maneno haya "Hii ni rushwa ya uchaguzi, tendo lililokatazwa chini ya sheria ya uchaguzi. Popote atakapogombea awekewe pingamizi na wagombea wetu ili aenguliwe kwa mjibu wa sheria. Watao rushwa hawa wafuatiliwe kila mahali waliko na kuwekewa mapingamizi ili uteuzi wao utenguliwe" mwisho wa kunukuu.

Ninaamini Mh Lissu kwa kuwa ni member wa JF atasoma andiko hili. Kwanza Mh Lissu aache kuwapotosha wanachama wa CDM kwa kitu ambacho anajua hakina uhalali wa kisheria. Ninaomba nimkumbushe Mh Lissu kuwa hadi sasa CCM haina wagombea wa Udiwani wala Ubunge, CCM hadi sasa inamgombea Urais tu ambaye ni Mh JPM (bulldozer). Kipindi cha uchaguzi hakizuiliwi watu kufanya kazi za maendeleo, sheria inakataza kufanya kazi za maendeleo ambazo zinaweza kutafsiriwa Kama Rushwa endapo tu utakuwa umeshapewa ridhaa ya kugombea.

Mh Tulia hadi sasa siyo mgombea na hajatangazwa na CCM kuwa ni mgombea popote. Hata hivyo dhana ya mtu kuitwa mgombea ni hadi tume ya uchaguzi imtangaze mtu kuwa ni mgombea. Kwa Katibu ya CCM BADO Mh Tulia ni mtia nia na si mgombea. Michakato ya utia nia husimamiwa na chama na situme kama unavyotaka kuwaaminisha watu. Labda Mh Lissu uniambie lini CCM imetangaza Wagombea wake? Ninadhani andiko langu fupi litawaongezea tafakuri juu ya uelewa wa maswala haya.
 
Daaaah!!

Vijana wa kiume ambao mpo mbioni kutengeneza watoto,chukueni hatua stahiki za kuhakikisha mnatengeneza taifa bora la kesho lisilo na uwezo mdogo kiakili.

Vijana wa kike na wamama watarajiwa wote nanyi jitahidi sana kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha mimba zinazotungwa, zinakuwa na afya njema na hatimaye watoto watakaozaliwa wawe na afya bora kiakili,kimwili na kiroho kwa mustakabari mwema wa kizazi kijacho na taifa kwa ujumla.
 
Mleta uzi nenda chooni ukanye,naona umelala nayo,
Lissu amesema ,hao watia nia,endapo watapitiswa kuwa wagombea,watawekewa mapingamuzi.mwambie Tulia aliyekutuma ,umletee post hii,akununulie chakula kwa mama lishe,ili akili ikusogee
 
Lisu, kipa katoka ndio maana watu hawamjibu.
 
Mleta bandiko, ni vyema ukapata kukisoma kwa makini kifungu namba 21 (a) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi kisha ujitafakari upya kwa kile ulichokiwasilisha hapa.
 
Huyo ni wa KUMPUUZA tu Pakawa. Anajua kuna TEUZI lukuki zinakuja baada ya uchaguzi hivyo anajaribu kutupa kete yake tena ili kujikomba kwa yesu wa lugola ili apate hata uDC kama siyo uRC.

Wataongea hata yasiyoongeleka
Huwa nataka kujua pasikali ana bifu na TL kwani kila andiko la kumkejeli linamgusa
 
Kwa hiyo kwa sababu hajatangazwa kuwa mgombea ndio anaruhusiwa kutoa rushwa?!hizo pesa anazogawa ziliidhinishwa na bunge gani na kwa shughuli ghani?!mada nyingine ni za kujadili na wanachama wenzio huko vikao vya ndani kwenye kudanganyana na sio za kuleta kwenye majukwaa ya watu wenye kufikiri kama JF
 
Sasa namba ya Simu ina kazi gani hapo ? kweli milembe inakuhusu Mkuu
 
Bandiko lako halina hoja hata moja ya kumfanya Great thinker ashtuke hata mtoto aliye competent na somo la Kiswahili darasa la 7 (B) anaandika kukuzidi
Mkuu nakuomba sana, heshimu darasa la 7! Nina binti yangu Yupo darasa hilo, ukianza kuweka darasa analosoma mwanangu kwenye hii thinking capacity, unanikatisha tamaa, wakati nemelipa ada (anasoma private)!
 
Huyo ni wa KUMPUUZA tu Pakawa. Anajua kuna TEUZI lukuki zinakuja baada ya uchaguzi hivyo anajaribu kutupa kete yake tena ili kujikomba kwa yesu wa lugola ili apate hata uDC kama siyo uRC.
Kazi kweli kweli
Mungu wetu ni wa wenye Heri (TL)
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Sana Pakawa ndiyo sababu kasikiliza sala zetu maana ile September 7, 2017 Watanzania wengi tulilia sana. Mimi niliamini tumeshampoteza Lissu na walimsubiri mkewe tu ili itangazwe rasmi lakini Mungu ni mwema sana.

Kazi kweli kweli
Mungu wetu ni wa wenye Heri (TL)
 
Mleta uzi nenda chooni ukanye,naona umelala nayo,
Lissu amesema ,hao watia nia,endapo watapitiswa kuwa wagombea,watawekewa mapingamuzi.mwambie Tulia aliyekutuma ,umletee post hii,akununulie chakula kwa mama lishe,ili akili ikusogee
Tumia hakili kidogo katiba inasemaje na siyo tundu lisu anasemaje
 
Kwa hiyo ni ruksa kwa mtu ambae si mgombea kutoa rushwa
 
Back
Top Bottom