LGE2024 Tundu Lissu ataja Sifa za Wakala ndani ya kituo cha Kura, Asema Ubishi ni Muhimu, Atumia Neno la Ubaya Ubwela

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
juzi tarehe 11 ilibidi niwanunulie walau chakula kwakweli kile kitendo viongozi wao waliwafanyia ni unyama wa hali ya juu ilibidi niwanunulie chakula mida ya saa 10 jioni baada ya kufika pale na kuambiwa sintofahamu inayoendelea juu ya wale mawakala nilijaribu kuliza siku inayofuata nambiwa waliingia mitini mtendaji akiwapigia simu hawashiki kabisa
 
CHADEMA wanakosea sn kusema watu wajitolee, mpe mtu hata elf 5 tu kwa siku kwa siku 10 ni 50 kitu ambacho wanaweza kabisa
 
mtu ajitolee kuanzia saa2 hadi saa12 kwa siku kumi yeye ni chizi au hana wategemezi wala shuhuli za kufanya bado umshindishe njaa nauli atoe yake huo sio wendawazimu
Wangeweza kuungana na ACT, kituo hiki wakala anakuwa wa ACT, kituo kile CHADEMA, mbona wangeweza kuchangia, bila mlo hakuna uzalendo ni utapeli tupu
 
Wangeweza kuungana na ACT, kituo hiki wakala anakuwa wa ACT, kituo kile CHADEMA, mbona wangeweza kuchangia, bila mlo hakuna uzalendo ni utapeli tupu
unajiuliza kama wakala hajapata mlo wa mchana ni vipi atafanya wajibu wake kwa ufanisi

sasa kama chama kimeshindwa kutoa mlo wa mchana tuh kwa mawala wao kwa siku kumi ndani ya awamu moja ya miaka mitano hapo kuna watu wenye akili timamu kweli
 
wakala mkorofi kwenye kituo cha kupigia kura atadhibitiwa vilivyo na Kwakweli atakua newtrolized vizuri sana na vyombo vya kutuliza ukorofu, ujeuri, ubishi na ujuaji na atapumzishwa sero vizuri tu..

watu wanatakiwa wapige kura kwa uhuru, uwazi haki, lakini pia wahesabu kura kwa usalama, amani na utulivu wa kiwango cha juu sana..

Yeyote anaejipanga na kujiandaa kuleta ujeuri na ujuaji wake kwenye kituo cha kupigia kura hatavumiliwa hata kwa sekunde moja. Atachukuliwa hatua kali zaidi on the spot, ili akawahadhie HQ kwenye press conference baada ya uchaguzi πŸ’
 
Mawakala wa Chadema wote wanalipwa hela nyingi kuliko wa chama chochote kile
Mkuu hii kitu ni kweli wanalalamika hata siyo utani tangu 2020 nimefanya utafiti Unguja na bara, mimi nasupport sn CHADEMA lakini kuna makosa madogo madogo kama haya, fanya utafiti mkuu. CCM wanatumia kama mwanya kuwapa hela ya lunch na kuingiza kura za watu ambao hawajaenda kupiga kura sababu wanakuwa na record zote kutoka kwa DEDs ni serious
 
Kwa hivi tunavyosema hakuna wakala anayelipwa kama wa Chadema, hao wa ccm wanapewa msosi na ahadi kibao za uongo
 
Na hii kitu inajulikana mapema sn, wangeweza kujipanga kwa mwaka mzima wasikosa milioni 500 za kuwalipa mawakala nchi nzima
hata kila mwanachama wao anewekewa kiwango cha kuchangia cha shilingi 500 kwa mwezi hio ni 6000 kwa mwaka sawa na 24000 kwa miaka 4 kwa wanachama elfu 50 tu ni kama 1.2B
 
Kwa hivi tunavyosema hakuna wakala anayelipwa kama wa Chadema, hao wa ccm wanapewa msosi na ahadi kibao za uongo
mkuu mawakala wa chadema moshi mjini hawapati mlo wa mchana hilo wafikishie akina mbowe acheni ubabaishaji
 
Kwa hivi tunavyosema hakuna wakala anayelipwa kama wa Chadema, hao wa ccm wanapewa msosi na ahadi kibao za uongo
CCM kuna mafisadi, wafanyabiashara wanalazimishwa kuchangia, wakuu wa idara, DEDs, DCs, DASs, RASs, RC, CEOs, wabunge, madiwani n.k, pia pesa zinachotwa kusupport uchaguzi kutoka serikali kuu, vote ya Ikulu haina auditing, per day wanalipwa 40,000 ni taarifa za kweli sababu ninazo za kutosha kusema hivyo.
 
hata kila mwanachama wao anewekewa kiwango cha kuchangia cha shilingi 500 kwa mwezi hio ni 6000 kwa mwaka sawa na 24000 kwa miaka 4 kwa wanachama elfu 50 tu ni kama 1.2B
Yap inawezekana kabisa, pia chama kijipange kuwa na vyanzo vya mapato nje na ruzuku inawezekana kabisa, hata kuwa na kumbi zao, apartments n.k
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…