Elitwege
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 5,294
- 10,970
Amani iwe nanyi.
Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha Mgombea Urais wa CCM rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, Wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!!
Mfano mgombea urais kupitia CHADEMA Tundu Lisu ameonekana mara kadhaa kwenye majukwaa ya kampeni akijaribu kuwafundisha watanzania kuhusu rais Magufuli alivyo! Yani Lisu badala ya kunadi ilani na Sera ya chama chake anatumia muda wote wa kampeni akitaja jina la Magufuli! Hivi Magufuli ndiyo ilani ya chadema?
Nikuambie tu Tundu Lisu, sisi watanzania huna cha kutufundisha kuhusu rais Magufuli.
1. Magufuli ametutumikia akiwa waziri kwa miaka 20 tangu enzi hizo kwenda Mtwara unatumia siku mbili kwenye meli, mpaka enzi hizi ambazo Mtwara unatumia masaa sita tu kufika ukiteleza kwenye lami, mjenzi wa mabarabara yote hayo ni Magufuli ,hivyo tunamjua huna cha kutufundisha.
2. Magufuli tulimchagua sisi wenyewe October 2015 tukiwa tunamjua na tumehangaika kwa miaka 5 akikomesha rushwa ufisadi,elimu bure, flyover na akirejesha nidhamu serikalini. Wewe Lissu ndiyo uje kutufundisha leo kuhusu Magufuli?
3. Tundu Lisu ulituambia tukibadili sheria za madini tutashitakiwa MIGA tukuulize je tumeshitakiwa MIGA?
Umekuwa mbunge kule Singida kwa miaka 10 je una lipi la kukumbukwa na wananchi wa jimbo lako?
Lisu umekuwa rais wa TLS je una lipi la kukumbukwa hapo?
Kwa ufupi sisi wananchi tunatakiwa tufundishwe kuhusu wewe Lisu ni mtu wa namna gani kwa sababu huna kitu cha kuonekana ulichowafanyia wananchi zaidi ya makelele na kutukana serikali.
Tundu Lisu wewe siyo mzalendo wa nchi yetu hivyo hufai kuwa rais na hutakaa uwe rais wa Tanzania na tarehe 28 October tutakupa fundisho kali la kwamba watanzania siyo wajinga wa kuchagua mtu yoyote hata mtetezi wa mabeberu.
Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha Mgombea Urais wa CCM rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, Wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!!
Mfano mgombea urais kupitia CHADEMA Tundu Lisu ameonekana mara kadhaa kwenye majukwaa ya kampeni akijaribu kuwafundisha watanzania kuhusu rais Magufuli alivyo! Yani Lisu badala ya kunadi ilani na Sera ya chama chake anatumia muda wote wa kampeni akitaja jina la Magufuli! Hivi Magufuli ndiyo ilani ya chadema?
Nikuambie tu Tundu Lisu, sisi watanzania huna cha kutufundisha kuhusu rais Magufuli.
1. Magufuli ametutumikia akiwa waziri kwa miaka 20 tangu enzi hizo kwenda Mtwara unatumia siku mbili kwenye meli, mpaka enzi hizi ambazo Mtwara unatumia masaa sita tu kufika ukiteleza kwenye lami, mjenzi wa mabarabara yote hayo ni Magufuli ,hivyo tunamjua huna cha kutufundisha.
2. Magufuli tulimchagua sisi wenyewe October 2015 tukiwa tunamjua na tumehangaika kwa miaka 5 akikomesha rushwa ufisadi,elimu bure, flyover na akirejesha nidhamu serikalini. Wewe Lissu ndiyo uje kutufundisha leo kuhusu Magufuli?
3. Tundu Lisu ulituambia tukibadili sheria za madini tutashitakiwa MIGA tukuulize je tumeshitakiwa MIGA?
Umekuwa mbunge kule Singida kwa miaka 10 je una lipi la kukumbukwa na wananchi wa jimbo lako?
Lisu umekuwa rais wa TLS je una lipi la kukumbukwa hapo?
Kwa ufupi sisi wananchi tunatakiwa tufundishwe kuhusu wewe Lisu ni mtu wa namna gani kwa sababu huna kitu cha kuonekana ulichowafanyia wananchi zaidi ya makelele na kutukana serikali.
Tundu Lisu wewe siyo mzalendo wa nchi yetu hivyo hufai kuwa rais na hutakaa uwe rais wa Tanzania na tarehe 28 October tutakupa fundisho kali la kwamba watanzania siyo wajinga wa kuchagua mtu yoyote hata mtetezi wa mabeberu.