Uchaguzi 2020 Tundu Lissu huna cha kutufundisha kuhusu Rais Magufuli, ni bora ukajikita kunadi Ilani ya CHADEMA

Uchaguzi 2020 Tundu Lissu huna cha kutufundisha kuhusu Rais Magufuli, ni bora ukajikita kunadi Ilani ya CHADEMA

Elitwege

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
5,294
Reaction score
10,970
Amani iwe nanyi.

Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha Mgombea Urais wa CCM rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, Wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!!

Mfano mgombea urais kupitia CHADEMA Tundu Lisu ameonekana mara kadhaa kwenye majukwaa ya kampeni akijaribu kuwafundisha watanzania kuhusu rais Magufuli alivyo! Yani Lisu badala ya kunadi ilani na Sera ya chama chake anatumia muda wote wa kampeni akitaja jina la Magufuli! Hivi Magufuli ndiyo ilani ya chadema?

Nikuambie tu Tundu Lisu, sisi watanzania huna cha kutufundisha kuhusu rais Magufuli.

1. Magufuli ametutumikia akiwa waziri kwa miaka 20 tangu enzi hizo kwenda Mtwara unatumia siku mbili kwenye meli, mpaka enzi hizi ambazo Mtwara unatumia masaa sita tu kufika ukiteleza kwenye lami, mjenzi wa mabarabara yote hayo ni Magufuli ,hivyo tunamjua huna cha kutufundisha.

2. Magufuli tulimchagua sisi wenyewe October 2015 tukiwa tunamjua na tumehangaika kwa miaka 5 akikomesha rushwa ufisadi,elimu bure, flyover na akirejesha nidhamu serikalini. Wewe Lissu ndiyo uje kutufundisha leo kuhusu Magufuli?

3. Tundu Lisu ulituambia tukibadili sheria za madini tutashitakiwa MIGA tukuulize je tumeshitakiwa MIGA?
Umekuwa mbunge kule Singida kwa miaka 10 je una lipi la kukumbukwa na wananchi wa jimbo lako?
Lisu umekuwa rais wa TLS je una lipi la kukumbukwa hapo?

Kwa ufupi sisi wananchi tunatakiwa tufundishwe kuhusu wewe Lisu ni mtu wa namna gani kwa sababu huna kitu cha kuonekana ulichowafanyia wananchi zaidi ya makelele na kutukana serikali.

Tundu Lisu wewe siyo mzalendo wa nchi yetu hivyo hufai kuwa rais na hutakaa uwe rais wa Tanzania na tarehe 28 October tutakupa fundisho kali la kwamba watanzania siyo wajinga wa kuchagua mtu yoyote hata mtetezi wa mabeberu.
 
Amani iwe nanyi.

Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha mgombea urais wa ccm rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!...
Hizi ndio hoja za watu wenye akili!
 
Amani iwe nanyi.

Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha mgombea urais wa ccm rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!...
Maguful naye hana cha kutufundisha kuhusu Lisu na CHADEMA. Ajikite kujibu tuhuma za upendeleo zinazo mkabili za ubaguzi wa kikanda, kidini, kindugu(nepotism), kivyama na kikabila.

Aache tabia ya kuvunja katiba na kutumia kodi yetu kama anatumia hela ya mshahara wake.

Kupendelea na kufanya miradi isiyo na tija kwa taifa huko kijijini kwake na kuonea watu kisa tu hawakubaliani na mitazamo yake
 
Amani iwe nanyi.

Tangu kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu, ukiacha mgombea urais wa ccm rais Magufuli anayetetea nafasi yake ananadi vizuri ilani ya chama chake, wagombea wa vyama vingine hata ilani ya chama hawana!...
Watanzania wa wapi unawasemea? Sisi wananchi wa wapi hao unawasemea? Labda unawasemea familia yako pekee na waliokutuma kutengeneza propaganda hii ya kishamba, Tambua kuwa watanzania wenye Akili timamu ndiyo pekee wanamuelewa Tundu lisu, lakini watanzania wanufaika wa mfumo kandamizi kama wewe ni vigumu umuelewe lisu kwani hapo ulipo unaishi kwa zidumu fikra zisizo sahihi za mwenyekiti wa CCM
 
Elitwege umekata pumzi mapema sana. Kama vile siyo wewe na yale ma-thread yako ulikuwa unapandisha humu daily
 
2. Magufuli tulimchagua sisi wenyewe October 2015 tukiwa tunamjua na tumehangaika kwa miaka 5 akikomesha rushwa ufisadi,elimu bure, flyover na akirejesha nidhamu serikalini...
Jifunze ukweli wa jiwe hapa chini ndio utagundua kuwa yeye ndiye fisadi nambari one.

Steven Makigo ni Swahiba wa Rais John Pombe Magufuli... hawakukutana barabarani!! Hawa wamesoma pamoja Lake Secondary School.

Akiwa kama waziri wa ujenzi, mwaka 2012 JPM alimteua Steven Makigo kuwa Mjumbe wa TEMESA. TEMESA hii ni ile ile ambayo ilinunua boti kwa mabilioni ya pesa huku boti yenyewe ikiwa na speed sawa na mtumbwi!!

Ni boti ile ile ambayo, ili kuwakata watu midomo wasiijadili, JPM yule yule akaipeleka boti hiyo jeshini! Yaani, Jeshi linapewa boti yenyewe mwendo wa kinyonga!!!

REMEMBER: Zabuni ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Chato iliweka sharti kwamba Contractor LAZIMA awe ni wa Kanda ya Ziwa!!

Yaani "National Project" inaweka condition ya ku-eliminate Watanzania wengine!!!!

Tena hapa tukumbushane kwamba, hiyo ni aina moja wapo ya Grand Corruption! YES, I mean it... a type of the GRAND CORRUPTION ambayo kwa makusudi watu wanaweka baseless conditions only to eliminate other competitors in favor of their guy!!!

SO, Kuna atakayeshangaa tukisema Mradi wa ujenzi wa Chato International Airport uliletwa maalumu ili tenda apewe Mayanga Construction Ltd, and ONLY Mayanga?!

Halafu ngoja, nimekumbuka!!

Hivi mnakumbuka JPM enzi zake akiwa Waziri wa Ujenzi akaja na "Wakandarasi Wazalendo"?!

Hoja tamu kweli kweli ambayo mtu ukiitia doa utaonekana unapingana na mtu anayekusudia kuwainua Wakandarasi Wazalendo lakini ukweli ni kwamba hiyo ilikuwa ni janja janja nyingine ya kui-favor Mayanga Construction!!

Wakati Wizara ya Ujenzi chini ya Magu ilipokuwa na mpango wa kujenga Daraja la Mbutu, Magu alijua kabisa Mayanga hatakuwa na ubavu wa kushindana na kampuni za kigeni na ndipo likaja suala la Wakandarasi Wazalendo, na Mayanga Construction akala shavu akiwa na "wazalendo" wengine!!
 
Haya kwa haya kila siku huku CCM ikiifirigisa nchi. Wananchi wamekuwa kama mashetani wanakula mlo mmoja kwa siku tena kwa shida
 
Lisu hata ilani hana

Umeshiba pilau na soda na kupewa paketi ya sigara na buku saba , hata wakati wa kusikiliza ilani unao?? Unajiona UMEPAAAATAAAna unaona CCM ndio chama
 
Back
Top Bottom