Pre GE2025 Tundu Lissu: Idadi ya unaowawakilisha Vs Mshahara unaopata

Pre GE2025 Tundu Lissu: Idadi ya unaowawakilisha Vs Mshahara unaopata

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Yesu Anakuja

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
12,675
Reaction score
25,924
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, ameendelea kuzungumzia changamoto za mfumo wa uchaguzi nchini, akisema kuwa kura ya mtu mmoja lazima iwe sawa na kura ya mtu mwingine popote ndani ya nchi. Lissu alitoa mifano akisema, "Kama ni kuchagua mbunge, uwe na uwezo wa kuchagua mbunge wa aina moja." Aliongeza kuwa, kwa sasa, tofauti kubwa ipo katika idadi ya watu wanaowakilishwa na wabunge wa majimbo tofauti.

Alisema, "Mbunge anayetoka Zanzibar anachaguliwa na watu elfu kumi na moja, wakati mbunge kutoka Jimbo la Kawe anachaguliwa na watu laki tatu na elfu arobaini na mbili."

Lissu alisisitiza kuwa ingawa wawakilishi hao wanapewa mishahara na marupurupu sawa, lakini idadi ya watu wanayowakilisha inatofautiana sana sawa na ‘Mbingu na Nchi’ jambo linalochafua mfumo wa kidemokrasia.
 
Japokua wabunge wote ni matapel lakini wabunge wa wanywa urojo wamezidi aisee wanakula hela zetu za bure kabisa
 
Hili jambo lishazungumzwa sana,tatizo la watanganyika wamejikita zaidi katika mambo ya masihara masihara.Utasikia jitu zima linakwambia UBAYA UBWELA.

Mama Samia kwa kujua Watanganyika ni watu wa miza miza akaanza utaratibu wa kununua magoli watanganyika walivyowajinga wakaingia kichwa kichwa.
 
mmoja anatania ati kwa zanzibar, mbunge mmoja jimbo lake mtoto akitoa harufu mbaya kama alikula mayai ya kuchemsha, harufu hiyo inaendea jimbo zima, ni kadogo tu. halafu sijawahi kuelewa, kwanini tunawalipa tena wabunge wa zanzibar wakati kule wameshapata mishahara kama wawakilishi. kwa nini walipwe mara mbili?
 
Back
Top Bottom