Kishimbe wa Kishimbe
JF-Expert Member
- Jul 18, 2013
- 5,566
- 5,477
Kama Nyerere alikuwa ni kanuni yao ya IMANI, mbona walivunja AZIMIO LA ARUSHA bila ridhaa yake? Tena katika hotuba yake moja, alieleza huwa anatembea na Biblia pamoja na kitabu cha AZIMIO LA ARUSHA, na alisisitiza kuw hajawahi kuona makosa yaliyokuwepo kwenye AZIMIO la ARUSHA walilolivunja CCM wenyewe kule Zanzibar.
Azimio la Arusha lilivunjwa Nyerere akiwa hai, na kwa ridhaa yake maana hakulikomalia kama lile la G55 na TANGANYIKA yao!
Azimio la Arusha lilivunjwa wakati DUNIA nzima ikifanya kinachoitwa 'STRUCTURAL ADJUSTMENT' baada ya mfumo wa ujamaa DUNIANI ukionyesha kushindwa kuhimili mapigo ya VITA VYA BARIDI mnamo miaka ya 1980 ya mwishomwisho!
KWAHILI LA KUVUNJA AZIMIO LA ARUSHA NAOMBA WATANI ZANGU BORA MNYAMAZE!
NA KUHUSU 'ATI KUNA' WATU NYERERE ALIKUWA HAWATAKI VILEVILE MNAONGEA BILA USHAHIDI, HEBU TULETEENI USHAHIDI NA SAHIHI MTUONYESHE! (TUMEISHAWAONYESHA MKATABA WA MUUNGANO!)