Napenda kuwashauri ndugu zangu tuwe na utamaduni wa kununua bidhaa kutoka kwa Wamachinga au vijana wa mitaani, sababu kubwa ni kama ifuatavyo;
1. kuunga mkono kazi zao ili wasikate tamaa ya maisha
2. kuwawezesha kiuchumi,
3. kuleta usalama katika jamii, kwa kuepusha wezi na majambazi
4. kuwatengenezea ajira maana hatuwezi kuwawezesha wote, basi hawa wanaojitoa na vibishara vya mkononi tuwaunge nao mkono...
5. ni Uzalendo pia.....
vijana wengi ni wenye afya na nguvukazi kwa taifa kama kungekuwa na shughuli ya kuwapa wafanye lakini tunawaona wanauza maji,chewing gums,magazeti...nk...unaweza kujiuliza kijana mpaka auze chewing gum ngapi apate pesa ya kula kwa siku, au chupa ngapi za maji lakini ameona inamtosha kufanya hivyo, kwahiyo tunapaswa kuwapa pia matumaini kwa njia tofauti za kuonyesha tunawajari na hata kama serikali ina kitu inaweza kusaidia au kuwatumia vijana hawa basi wawakusanye na kuwasaidia.
pia suala la watoto wa mtaani limeongezeka kwa kasi sana, linabidi tuliangalie, watoto wanaokaa kwenye trafik light na kujifanya wanaosha magari wameongezeka sana hasa pale ubungo, kwakuwa hatuna msaada wa kuwapa basi kama unachochote wape tu na kama kuna sehemu unajuwa wanaweza kupelekwa basi toa ushauri, mimi niliwahi kuchukua mmoja lakini akanitoroka baada ya kuanza kufuatilia utaratibu wa kutaka kupata kibali cha ustawi wa jamii ili niishi nae akaona labda nawatafuta wazazi wake ili arudi kwao.....
saidia maskini, Piga vita umaskini kwa vitendo...
1. kuunga mkono kazi zao ili wasikate tamaa ya maisha
2. kuwawezesha kiuchumi,
3. kuleta usalama katika jamii, kwa kuepusha wezi na majambazi
4. kuwatengenezea ajira maana hatuwezi kuwawezesha wote, basi hawa wanaojitoa na vibishara vya mkononi tuwaunge nao mkono...
5. ni Uzalendo pia.....
vijana wengi ni wenye afya na nguvukazi kwa taifa kama kungekuwa na shughuli ya kuwapa wafanye lakini tunawaona wanauza maji,chewing gums,magazeti...nk...unaweza kujiuliza kijana mpaka auze chewing gum ngapi apate pesa ya kula kwa siku, au chupa ngapi za maji lakini ameona inamtosha kufanya hivyo, kwahiyo tunapaswa kuwapa pia matumaini kwa njia tofauti za kuonyesha tunawajari na hata kama serikali ina kitu inaweza kusaidia au kuwatumia vijana hawa basi wawakusanye na kuwasaidia.
pia suala la watoto wa mtaani limeongezeka kwa kasi sana, linabidi tuliangalie, watoto wanaokaa kwenye trafik light na kujifanya wanaosha magari wameongezeka sana hasa pale ubungo, kwakuwa hatuna msaada wa kuwapa basi kama unachochote wape tu na kama kuna sehemu unajuwa wanaweza kupelekwa basi toa ushauri, mimi niliwahi kuchukua mmoja lakini akanitoroka baada ya kuanza kufuatilia utaratibu wa kutaka kupata kibali cha ustawi wa jamii ili niishi nae akaona labda nawatafuta wazazi wake ili arudi kwao.....
saidia maskini, Piga vita umaskini kwa vitendo...