Tupeane elimu kuhusu ununuzi wa viwanja, hususani vya makazi

Tupeane elimu kuhusu ununuzi wa viwanja, hususani vya makazi

bilemasome

Member
Joined
Oct 31, 2016
Posts
48
Reaction score
9
Habari Ndugu, jamaa na marafiki

Sisi sote tumesikia au tumepitia kuhusu kutapeliwa kwenye ununuzi wa viwanja.

Hii hali inachosha na inaumiza sana, hasa kwa yule aliyetapeliwa kwenye ununuzi wa viwanja.

Wengi wetu huwa tunawacheka waliotapeliwa au kununua kiwanja chenye mgogoro (nakuombea usipitie katika hii hali-inaumiza sana).

Hii ni kutokana na watu kukosa elimu juu ya ununuzi wa kiwanja.

Binafsi nimejaribu kutafuta hii elimu walau inisaidie kujua ABCs za kufuata ili niweze kuepuka hizi changamoto (kutapeliwa/kununua kiwanja chenye migogoro) nimekosa, yaani sijaona mtu ameliongelea hili.

Siku hizi kumezuka kampuni mbalimbali zinauza viwanja- yaani wanakuuzia kwa mita za mraba n.k - jinsi ya kuwajua kama ni kampuni yao ni halali au laa unajuaje?

Au ni taratibu zipi mtu afuate, endapo atanunua kiwanja kutoka kwa mtu.

Tena hapa unakuta umepelekwa na dalali kwa huyo mtu. Ni taratibu zipi mtu anabidi afuate.

Ombi Langu:
Najua wadau na wanasheria wa haya mabo ya viwanja mpo wengi humu, ninawaomba, Mtupatie elimu kuhusu ununuzi wa viwanja na mambo ya kuyaepuka ili tuweze kuzikabili hizi changamoto za kutapeliwa na ununuzi wa viwanja vyenye migogoro"

Mchango wako katika hili, utatusaidia Watanzania wengi, nami naahidi elimu nitakayoipata hapa nitaihubiri na kuisambaza kwa watu wote wenye kiu ya ununuzi wa viwanja.

Natanguliza Shukrani

Mungu akubariki wewe utakayeweka mchango wako wa elimu hapa!
 
Ni kweli kabisa aise hii hali
Inaumiza sana nilinunua kiwanja chanika, nikanza ujenzi kufika kwenye kupaua watu wakaja wakasema aliekuzia hichi kiwanja si mmiliki halali nilichoka, mpaka leo sijapata haki yangu nikikumbuka gharama ambazo nimetumia hadi ilipo naishia kuumia tu aisee.
 
Ni kweli kabisa aise hii hali
Inaumiza sana nilinunua kiwanja chanika, nikanza ujenzi kufika kwenye kupaua watu wakaja wakasema aliekuzia hichi kiwanja si mmiliki halali nilichoka, mpaka leo sijapata haki yangu nikikumbuka gharama ambazo nimetumia hadi ilipo naishia kuumia tu aisee.
pole sana mkuu
 
Habari Ndugu, jamaa na marafiki

Sisi sote tumesikia au tumepitia kuhusu kutapeliwa kwenye ununuzi wa viwanja.

Hii hali inachosha na inaumiza sana, hasa kwa yule aliyetapeliwa kwenye ununuzi wa viwanja.

Wengi wetu huwa tunawacheka waliotapeliwa au kununua kiwanja chenye mgogoro (nakuombea usipitie katika hii hali-inaumiza sana).

Hii ni kutokana na watu kukosa elimu juu ya ununuzi wa kiwanja.

Binafsi nimejaribu kutafuta hii elimu walau inisaidie kujua ABCs za kufuata ili niweze kuepuka hizi changamoto (kutapeliwa/kununua kiwanja chenye migogoro) nimekosa, yaani sijaona mtu ameliongelea hili.

Siku hizi kumezuka kampuni mbalimbali zinauza viwanja- yaani wanakuuzia kwa mita za mraba n.k - jinsi ya kuwajua kama ni kampuni yao ni halali au laa unajuaje?

Au ni taratibu zipi mtu afuate, endapo atanunua kiwanja kutoka kwa mtu.

Tena hapa unakuta umepelekwa na dalali kwa huyo mtu. Ni taratibu zipi mtu anabidi afuate.

Ombi Langu:
Najua wadau na wanasheria wa haya mabo ya viwanja mpo wengi humu, ninawaomba, Mtupatie elimu kuhusu ununuzi wa viwanja na mambo ya kuyaepuka ili tuweze kuzikabili hizi changamoto za kutapeliwa na ununuzi wa viwanja vyenye migogoro"

Mchango wako katika hili, utatusaidia Watanzania wengi, nami naahidi elimu nitakayoipata hapa nitaihubiri na kuisambaza kwa watu wote wenye kiu ya ununuzi wa viwanja.

Natanguliza Shukrani

Mungu akubariki wewe utakayeweka mchango wako wa elimu hapa!
Unapopata eneo la kununua jiridhishe kwanza na haya machache
1. Pata mmiliki halali wa eneo

2. Pata historia halisi ya eneo hasa kwenye umiliki, migogoro dhamana nk

. Liliwahi kumilikiwa na watu wangapi
.lina mgogoro wa kindugu?
.Je limewekwa kama dhamana bank ama popote?
.Je lina mgogoro wa mipaka?

3. Fika serikali ya eneo husika upate ramani ya mipango miji kujua status ya eneo unalotaka kununua

4. Wafahamu unaopakana nao

5. Mazingira ya kijiografia .. Je linakalika vipindi vyote vya mwaka?

6. kiroho.. Je ni ardhi iliyonenewa mabaya? Ina historia ya nuksi? Haina mapooza? Haijawahi kumwaga damu ya mtu? Haijawahi kuwa kilinge ama madhabahu ya giza? Sio makazi ya maroho na mapepo wachafu?

Hayo mambo sita ni msingi mkuu unapotaka kununua ardhi kwa matumizi yoyote yale yawe biashara ama makazi
 
Ni kweli kabisa aise hii hali
Inaumiza sana nilinunua kiwanja chanika, nikanza ujenzi kufika kwenye kupaua watu wakaja wakasema aliekuzia hichi kiwanja si mmiliki halali nilichoka, mpaka leo sijapata haki yangu nikikumbuka gharama ambazo nimetumia hadi ilipo naishia kuumia tu aisee.
😄😄😄 halafu walivo wangese walikuacha hadi umalize renta 😄😄😄 watu wanapenda mterezo
 
Unapopata eneo la kununua jiridhishe kwanza na haya machache
1. Pata mmiliki halali wa eneo

2. Pata historia halisi ya eneo hasa kwenye umiliki, migogoro dhamana nk

. Liliwahi kumilikiwa na watu wangapi
.lina mgogoro wa kindugu?
.Je limewekwa kama dhamana bank ama popote?
.Je lina mgogoro wa mipaka?

3. Fika serikali ya eneo husika upate ramani ya mipango miji kujua status ya eneo unalotaka kununua

4. Wafahamu unaopakana nao

5. Mazingira ya kijiografia .. Je linakalika vipindi vyote vya mwaka?

6. kiroho.. Je ni ardhi iliyonenewa mabaya? Ina historia ya nuksi? Haina mapooza? Haijawahi kumwaga damu ya mtu? Haijawahi kuwa kilinge ama madhabahu ya giza? Sio makazi ya maroho na mapepo wachafu?

Hayo mambo sita ni msingi mkuu unapotaka kununua ardhi kwa matumizi yoyote yale yawe biashara ama makazi
mkuu kuna hiki kitu kinaitwa ni mali yangu hata km CDA ilipita kugawa lishamba lako kuna watu hawataki kutoka hata mti alioupanda hawataki uungoe hizi sehemu hata ukihoji majirani huwa waoga kusema.
 
Back
Top Bottom