Tupeane Hints za Biashara ya Vyuma Chakavu

Tupeane Hints za Biashara ya Vyuma Chakavu

The Sunk Cost Fallacy

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2021
Posts
19,582
Reaction score
14,167
Hello habari zenu,

Niko interested na biashara ya Vyuma Chakavu, tafadhari mwenye hints Kuhusu faida na changamoto zake tujuzane..
 
Kwamba hakuna wanaofanya hii biashara au?
Nilifanya kwa muda nikaacha kwa changamoto ambazo zilikuwa nje ya uwezo wangu,

Lakini changamoto nilizokuwa nakutana nazo ni polisi pale nimeuziwa vyuma vya wizi,

Mwanzo nilinunua mzani ambao una label ya WMA(unatambulika na wakala wa vipimo Tanzania) sababu ukikutwa na mzani ambao hautambuliki ni makosa, nikawa nanunua kwa kilo sh 550 namimi naenda kuuza NYAKATO STEEL KWA 1,000 kwa kilo, na kuna vyuma vizito ambavyo nilikuwa siuziwi kwa kilo bali tuna-bargain ,kuanzia plate, Angle Iron za milimita tatu na kuendelea.

Ishu nyingine inakuja kwenye mtaji, maana unaweza letewa vyuma ambavyo huwezi kufika bei (hii ni kwenye bargaining) sio vya kupima.

Obvious ni biashara nzuri, ila unatakiwa uwe na kibali ili uifanye bila usumbufu na usinunue nyara za serikali(mifuniko ya chemba za barabarani,vyuma vya Tanesco na vinginevyo)
 
Nilifanya kwa muda nikaacha kwa changamoto ambazo zilikuwa nje ya uwezo wangu,

Lakini changamoto nilizokuwa nakutana nazo ni polisi pale nimeuziwa vyuma vya wizi,

Mwanzo nilinunua mzani ambao una label ya WMA(unatambulika na wakala wa vipimo Tanzania) sababu ukikutwa na mzani ambao hautambuliki ni makosa, nikawa nanunua kwa kilo sh 550 namimi naenda kuuza NYAKATO STEEL KWA 1,000 kwa kilo, na kuna vyuma vizito ambavyo nilikuwa siuziwi kwa kilo bali tuna-bargain ,kuanzia plate, Angle Iron za milimita tatu na kuendelea.

Ishu nyingine inakuja kwenye mtaji, maana unaweza letewa vyuma ambavyo huwezi kufika bei (hii ni kwenye bargaining) sio vya kupima.

Obvious ni biashara nzuri, ila unatakiwa uwe na kibali ili uifanye bila usumbufu na usinunue nyara za serikali(mifuniko ya chemba za barabarani,vyuma vya Tanesco na vinginevyo)
Thanks mkuu kwa ku share hints muhimu..

But ukiacha kwa sababu za changamoto za biashara au? Pili namna ya kuifanya inakuaje kwamba wateje watajuaje wewe unanunua Vyuma Chakavu I mean unapataje huo mzigo?

Mwisho sio kwa umuhimu,mtaji unaotakiwa ni around kiasi gani? Thanks in advance.
 
Thanks mkuu kwa ku share hints muhimu..

But ukiacha kwa sababu za changamoto za biashara au? Pili namna ya kuifanya inakuaje kwamba wateje watajuaje wewe unanunua Vyuma Chakavu I mean unapataje huo mzigo?

Mwisho sio kwa umuhimu,mtaji unaotakiwa ni around kiasi gani? Thanks in advance.
Fungua ofisi yako sehem ambayo ni rahisi kukusanya mzigo wako unaweka tu mzani nje ya ofisi yako, kuna maeneo ya magereji,kuna maeneo ya viwanda n.k hizi ndo sehemu unaweza kusanya mzigo kwa haraka zaidi, kama ni kunnua zile za kupima ukiwa na 2m unaanza kabisa hiyo ni mbali na kukununua mzani,maana NYAKATO STEEL nilikuwa naenda na mzigo kuanzia tani moja na nusu....ila kuna mahala ni wewe tu vibali na mtaji wako vyuma ni vingi mno
 
Fungua ofisi yako sehem ambayo ni rahisi kukusanya mzigo wako unaweka tu mzani nje ya ofisi yako, kuna maeneo ya magereji,kuna maeneo ya viwanda n.k hizi ndo sehemu unaweza kusanya mzigo kwa haraka zaidi, kama ni kunnua zile za kupima ukiwa na 2m unaanza kabisa hiyo ni mbali na kukununua mzani,maana NYAKATO STEEL nilikuwa naenda na mzigo kuanzia tani moja na nusu....ila kuna mahala ni wewe tu vibali na mtaji wako vyuma ni vingi mno
Thanks
 
Sikuona bandiko lako.ila hii biashara ipo kwenye damu kabisa maana wazee wetu ndio waaanzilishi wa hii biashara hapa mjini kipindi hicho hakuna viwanda tanzania kwahiyo walikuwa wakisafirisha kupeleka kenya.......

Yangu ni haya machache kwako....

Kuna mtu kakushauri hapo ukiwa na milion 2 unaanza sio kweli .hapo utakuwa mdundulizaji tu na sio mwenye duka. Ukitaka kuanza kweli ili uone atleast maendeleo basi anza na milion 10 ikiwa tayari una frame na mzani wako.unaweza kukaa mwenyewe au kumtafuta kijana.

Vitu vimepanda bei mno ndio maana nimekuambia mtaji wa milion 10 na tayari uwe na kibali cha mwaka ili usipate usumbufu wa police......

Unaweza kununua juu ya wenzio kwa kuongeza hata 100 au 50 ili kuwavuta.ila kwa mtaji wako mdogo wa milion 10 fungua kidogo kando ya mji buza,chamanzi,kisewe,chanika,gongo la mboto,usigungue maeneo ya temeke au kkoo maana ushindani ni mkubwa kuna watu wana mitaji mpaka milion 300.hao wananunua bei za viwandani kabisa kwahiyo unaweza kuona kama hupati wateja kumbe bei zako zipo chini. Au fungua mkoani kwa milion kumi utakuwa ww ndio unakimbiza mno.

Vitu vinavyonunuliwa sana ni vifuatavyo
Chuma 600
Copper 12,000
Soft/aluminium 3000~4000
Betri 1500
Brasi 5,000
Fufu 1000
Rejeta
Stanley steel

Note....chunga sana usinunue vyuma vya reli itakuwa ndio mwisho wa biashara yako.!

Mizigo ya nje ndio inakulipa sana na ndio ina faida ya haraka haraka.

Kama utamuweka kijana uwe unafanya mahesabu kila baada ya muda maana akikuibia atakufilisi .

Kuhusu kupeleka mzigo kiwandani unatakiwa kuwa na dalali wako ambae atakupa hela baada ya kuingiza mzigo maana kiwandani sometimes huwa hawana hela cash.so dalali wako ndio atakupa cash alaf yeye atasubiria kupewa kiwandani.


Niishie hapo kwa maswali yoyote kuhusu hii biashara msisite kuniuliza mana nimekulia humu.
 
Kuna sehemu mkoani nimeona kuna matrecta mengi chakavu maeneo ya Dodoma vp nikijumlisha na ghalama za kubeba na kusafirisha inaweza ikanilipa?
 
Back
Top Bottom