#COVID19 Tupeni mrejesho wa chanjo ya Uviko-19

DALA

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2009
Posts
2,256
Reaction score
4,647
Habari wana jamvi,

Kwa wale wenzetu mliobahatika kupata chanjo tayari, tupeane taarifa.

Ni aina gani ya chanjo ulipewa?

Baada ya kupigwa chanjo umebaini tatizo lolote la muda mfupi?

Chochote cha kuzingatia?

Je, kwa maoni binafsi unaweza kumshauri mtu achanjwe baada ya ulichoki experience?

Tuelimishane, tutoane hofu na tupambane na upotoshaji.
 
Chanjo inakuta miili imedhoufika ya wa Tanzania wengi, hata kama ni nzuri lazima utapata madhara tuna magonjwa mengi miilini hatutaki kuyatibu.
 
Nguvu za kiume kwisha habari yao

Nyie ni wafuasi wa kibwetere hamueleweki mara mtu anakuwa zombie Sasa hivi nguvu za kiume,haya sasa kwa wanawake itakuwa nn nguvu za kike
 
Chanjo inakuta miili imedhoufika ya wa Tanzania wengi, hata kama ni nzuri lazima utapata madhara tuna magonjwa mengi miilini hatutaki kuyatibu.

Tupe mrejesho wa hali halisi sasa
 
Wakisema zinaongeza nguvu za kiume utaona vijana sa 11 alfajiri walishapanga mstari na wakisisitiza wahudumu wafanye chapchap kuwachanja
 
vipi kuhusu wale wanao ishi na maambukizi ya Virusi vya ukimwi na wanatumia dozi? hakuna athari zozote?

Wale kesi yao naona ni tofauti na hii mkuu
 
Hapa nilipo mjegejo haujasimama tangu nichome
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…