Tupia hapa salaam zako za Heri ya Krismas na Mwaka Mpya kwa Rais Magufuli!

Tupia hapa salaam zako za Heri ya Krismas na Mwaka Mpya kwa Rais Magufuli!

Ki Mun

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2014
Posts
3,442
Reaction score
4,388
Naanza mimi:

Salaam za Krismas na Mwaka Mpya Mtukufu Rais!Mimi huwa napenda tu kukutazama jinsi unavyoonekana kukifurahia cheo chako cha Urais pengine kuliko Marais wote wane waliokutangulia na pengine kuliko binadamu yeyote ambaye amepata kuwa Rais hapa duniani - kiasi kwamba unaona katiba kwako wewe si lolote si chochote!

Ujumbe: Tenda haki 2017 nawe utaishi na kutawala kwa Amani.
Wako Mtiifu,
Ki Mun
 
JPJM nakutakia kheri ya X-Mass na mwaka Mpya wenye mafanikio na mtizamo Mpya wa kuipeleka Tanzania mbele
 
Mimi nasema kujenga uwanja mkubwa vile Chato wa mita 3000 kwa 46 wakati wananchi kule hata kujenga nyumba za bati wanashindwa which means hawatapanda commercial aircrafts, ni ubinafsi wa hali ya juu. Kwa nini mkuu usimalizie uwanja wa Mwanza halafu kule Chato ujenge uwanja mdogo wa size ya Bombadier, sidhani kama Dreamliner ikija itapata abiria wa kutua Chato....

Anyway heri ya Christmass mtukufu raisi wetu, tunakuombea kama unavyosisitiza
 
Heri ya Krisimasi Mh. Rais nakuombea kwa Mungu ulinzi wake na kama alivyoomba Suleimani hekima ya kuingia na kutoka mbele ya sisi uonaotuongoza. Mungu aendelee kukuongoza na kukutegemeza kama ilivyo siku zote katika maombi yako.

Baraka tele za Noel ziwe nawe pamoja na mama yetu mpendwa pamoja na familia!
 
Wacha nipite kimyakimya tu kuepuka matatizo

Mh. Rais JPM, tunakutakia Hery ya Krismas na Mwaka Mpya 2017. Tunakuombea Mungu akupe Uzima wa Rohoni na Mwilini, ili uendelee kulitumikia hili taifa. Tunaomba usikate tamaa na maneno na unafiki wa Watanzania wachache. Wengi wao ni wapiga dili. Tunakupenda sana.
 
Baada ya solomoni kufariki,mtoto wake rehobam akatawazwa kuwa mfalme,
waisrael ambao walikuwa wamechoshwa na utawala wa mabavu wa solomoni na kodi za kila aina,wakawatuma watu wakamwambie mfalme mpya alegeze kidogo watu wanalalamika asiwe kama babake.
Mfalme mpya kusikia hivyo,akaenda kuomba ushauri kwa viongozi waliokuwa wa umri mkubwa ambao aliwakuta serikalini,wakamwambie wasikize watu wako uwalegezee japo kidogo nawe utatawala vizuri tu.
Mfalme mpya baada ya hapo kawafuata washauri wake wapya wale alioingia nao serikalini,
ambao wengi walikuwa vijana vijana tu wa rika kama la yule mungu wa kariakor.
Wakamshauri na kumwambia wewe wakazie tu bamba to bamba,
mfalme karudi kwa wazee wa kiisrael akawambie.,"mwende muwambie wananchi aliyokuwa akiwafanyia babangu solomoni ,mimi nitawafanyia mara tano zaidi.
Wazee wa kiisrael wakapeleka message kwa watu wao.
Kilichotokea waisrael wakajitenga,makabila 10 yakajichagulia mfalme wao na kuanzisha ufalme wa israel,
wakimuacha mfalme mwana wa solomoni na makabila mawili ambayo yakaunda utawala wa yuda,na hizo nchi mbili ziliishi kwa uhasama na vita mpaka dakika ya mwisho .

Haya maandiko yako ndani ya bibilia sikumbuki kitabu kipi
 
Mimi nasema kujenga uwanja mkubwa vile Chato wa mita 3000 kwa 46 wakati wananchi kule hata kujenga nyumba za bati wanashindwa which means hawatapanda commercial aircrafts, ni ubinafsi wa hali ya juu. Kwa nini mkuu usimalizie uwanja wa Mwanza halafu kule Chato ujenge uwanja mdogo wa size ya Bombadier, sidhani kama Dreamliner ikija itapata abiria wa kutua Chato....

Anyway heri ya Christmass mtukufu raisi wetu, tunakuombea kama unavyosisitiza
utapata matumizi,sio bigdeal kivile,
 
Dah....
Kwa John & Janeth....
Nawatakia furaha, amani na afya njema,
Baba.. umeonyesha njia.... tena kwa dhamira ya kweli... Watanzania wenye nia njema tumekuelewa.... wapiga dili wanasambaratika... hawana namna.. sasa hivi wanatafuta kazi za halal....
Baba... vitendo vyako vimetusaidia sisi kuwajua majirani zako tuliyowaamini... kumbe ni chui waliojivika ukondoo.....
Baba... usirudi nyuma... komaa... wenyenia njema tuko pamoja nawe...
[emoji120] [emoji120]
 
Salamu za nini?atoe mikopo kwa wanafunzi haraka pesa sio zake ni za umma
 
Baada ya solomoni kufariki,mtoto wake rehobam akatawazwa kuwa mfalme,
waisrael ambao walikuwa wamechoshwa na utawala wa mabavu wa solomoni na kodi za kila aina,wakawatuma watu wakamwambie mfalme mpya alegeze kidogo watu wanalalamika asiwe kama babake.
Mfalme mpya kusikia hivyo,akaenda kuomba ushauri kwa viongozi waliokuwa wa umri mkubwa ambao aliwakuta serikalini,wakamwambie wasikize watu wako uwalegezee japo kidogo nawe utatawala vizuri tu.
Mfalme mpya baada ya hapo kawafuata washauri wake wapya wale alioingia nao serikalini,
ambao wengi walikuwa vijana vijana tu wa rika kama la yule mungu wa kariakor.
Wakamshauri na kumwambia wewe wakazie tu bamba to bamba,
mfalme karudi kwa wazee wa kiisrael akawambie.,"mwende muwambie wananchi aliyokuwa akiwafanyia babangu solomoni ,mimi nitawafanyia mara tano zaidi.
Wazee wa kiisrael wakapeleka message kwa watu wao.
Kilichotokea waisrael wakajitenga,makabila 10 yakajichagulia mfalme wao na kuanzisha ufalme wa israel,
wakimuacha mfalme mwana wa solomoni na makabila mawili ambayo yakaunda utawala wa yuda,na hizo nchi mbili ziliishi kwa uhasama na vita mpaka dakika ya mwisho .

Haya maandiko yako ndani ya bibilia sikumbuki kitabu kipi
mbona hujamalozia point yako ni kulingana na huu uzi
 
Back
Top Bottom