Tupo Baba Wawili mtoto Mmoja.

Tupo Baba Wawili mtoto Mmoja.

D TARGET

JF-Expert Member
Joined
Mar 18, 2013
Posts
223
Reaction score
98
Kuna binti nilikuwa ninamahusiano naye ya kimapenzi, Binti anaishi mkoa wa Dodoma mi ninaishi Pwani, huyu binti kunakipindi aliniambia anaujauzito wangu, hyo ilikuwa ni baada ya mimi kwenda Dodoma na kushirikiana naye kimwili, then mi nikarudi Pwani, Baada ya kunipa taharifa, muda ulivyokuwa unazidi kuendelea ikawa tunaendelea kuwasiliana na anapoitaji matumizi nikawa namtumia kama kawaida.
Ilivyofika miezi Tisa Binti akajifungua mtoto wa Kiume! Baada ya binti kujifungua akaja Mpk kwangu then nikampeleka mpk Iringa kwa wazazi wangu, ili wapate nafasi ya kumpa pongezi zao, na kumfahamu mjukuu wao. Baada ya binti kukaa kwa wazazi kama wiki tatu hv, zikatokea rumous kuwa binti anatembea na Moja ya wapangaji wa pale nyumbani kwa wazazi wangu, binti nilivyomuuliza akabisha kwamba hakuna kitu kama hcho. Siku chache zilizofuata binti akaondoka Nyumbani na kurudi Dodoma, akada mmiliki wa nyumba aliyopangisha uko Dodoma amempigia simu na kumwambia kuwa anataka kodi ya nyumba yake lasivyo atatoa vyombo vyake nje hvyo ameamua kwenda ili akamalizane na Baba mwenye nyumba.
Ikawa tunaendelea kuwasiliana na kusaidiana kama kawaida ktk kipind chote, na akawa amedai kuwa muda siyo mrefu atarudi kumleta mtoto kwangu kwani baba mwenye nyumba wamesha malizana.
Hv majuzi nimempigia simu nikashangaa simu yake imepokelewa na mwanaume, jamaa akajitambulisha kama yeye ni Mume wa huyo Binti, aikuwa shida nikamwambia mi ni mzazi mwenzake na huyo binti! Jamaa akiniambia ok we ndiyo Baba Akram, ikabidi nigune kidogo, nikamwambia mi siyo baba akram mi Baba Junior! Jamaa akaniuliza Junior ndio nani, sababu jamaa alikuwa mwelewa ikabidi tuanze kujuzana zaidi, mwisho wa siku nikagundua kuwa kumbe kuna Jamaa mwingine ambaya naye pia ni Baba wa Yule Mtoto na ndiye aliyempa yule mtoto ilo jina la Junior, na huyo jamaa ndiye anayeishi na yule mtoto kwa sasa baada ya yeye Binti kupewa ujauzito na huyo jamaa anayeishi naye kwasasa.
Binti nikimpigia simu anabaki anajing'ata ng'ata tu, sasa wadau wa JF haswa wale ambao wanaijua vizuri sheria ya mambo ya uzazi, nimfanyieje huyu binti?
 
Wewe lengo lako hasa nini, unataka mtoto, unataka kumdhuru mama au unapenda nini hasa ili tukusaidie ushauri
 
jipange ukachukue mwanao.kwani mmefunga ndoa??uue kwa sababu ya nini haswa??shukuru mungu umeyaona hayo ungekutana nayo ndani ya ndoa!!na inawezekana hata mtoto hutunzi wewe dada wawatu anahangaika na mwanae
 
mwache mtoto akae na mama yake na huyo baba akram but make sure that mtoto akiwa mkubwa una mpa full story, hii itamjenga saana huyo mtoto na atazidi kuwaheshimu wazazi wake hasa mama yake
 
Mtafute huyo binti akusaidie kumpata juniour mkachukue DNA.
Kama majibu yatakuwa positive utaongea na Akram umchukue juniour wako, kAM NEGA. utasepa kimya na utakuwa umeondokana na mawazo yanayokusumbua.

Kila lakheri baba Juniour in ()
 
na kama kweli mtoto si wako ni wa jamaa wewe si ndiyo unapaswa kushughulikiwa na jamaa?.....wasiliana na jamaa, fanyeni man talk mpange kufanya DNA test.....usikimbilie polisi au kuwa na hasira utakuja kuumbuka.

Funny side: ukaenda dodoma, you had sex with a hooker without protection?....LoL. Subiri na mwingine atakwambia ana mimba yako
 
na kama kweli mtoto si wako ni wa jamaa wewe si ndiyo unapaswa kushughulikiwa na jamaa?.....wasiliana na jamaa, fanyeni man talk mpange kufanya DNA test.....usikimbilie polisi au kuwa na hasira utakuja kuumbuka.

Funny side: ukaenda dodoma, you had sex with a hooker without protection?....LoL. Subiri na mwingine atakwambia ana mimba yako

kaka thanxs kwa ushauri, about un safe it was just a mistake!
 
kaka thanxs kwa ushauri, about un safe it was just a mistake!

be careful mkuu, wanawake wana attributes nyingi sana na si rahisi kuwaelewa na kuwacontrol and that is why mahusiano na ndoa nyingi zinakufa hata kama watu wamekuwa pamoja kwa miaka mingi.
 
Wewe lengo lako hasa nini, unataka mtoto, unataka kumdhuru mama au unapenda nini hasa ili tukusaidie ushauri
Nataka ushauri utaonisaidia kama wanaonipa wadau wengine!
 
Zamani nilikuwa nawashangaa wamama wanaowaambia watoto wao wa kiume wasikubali mimba wanazoletewa upesi-upesi, wanawasisitiza kwanza wakatae. Nikawa nashangaa inakuaje wamama hawawaonei huruma wanawake wenzao.
Baadae nika realize kwamba mazingira yanaweza yakam-force mtu kufanya maamuzi ya kinyama hata kama hana roho ya kinyama.
 
Zamani nilikuwa nawashangaa wamama wanaowaambia watoto wao wa kiume wasikubali mimba wanazoletewa upesi-upesi, wanawasisitiza kwanza wakatae. Nikawa nashangaa inakuaje wamama hawawaonei huruma wanawake wenzao.
Baadae nika realize kwamba mazingira yanaweza yakam-force mtu kufanya maamuzi ya kinyama hata kama hana roho ya kinyama.

Ndugu ata usiseme, nilikuwa nachukia sana kusikia mtu ameua, ila sasa hv nishaelewa dunia iko fair ila raia ndiyo wabaya.
 
wee mhehe mwenzangu angalia sana ucje kujinyonga baada ya kupima DNA ka vipi sepa mapema, maana ulikuwa pwani na binti dom, na huyo jamaa hujui alikuwa wapi na alimpanda mara ngapi kwa siku au week! kwa hiyo juhadhari sana nswelaga!
 
Ndugu ata usiseme, nilikuwa nachukia sana kusikia mtu ameua, ila sasa hv nishaelewa dunia iko fair ila raia ndiyo wabaya.

Hapo ndugu yangu tuliza hasira fanya maamuzi ya busara. Kuhusu mtoto, nenda kafanye paternal test (DNA test), akiwa wa kwako mchukue sepa nae.
 
wee mhehe mwenzangu angalia sana ucje kujinyonga baada ya kupima DNA ka vipi sepa mapema, maana ulikuwa pwani na binti dom, na huyo jamaa hujui alikuwa wapi na alimpanda mara ngapi kwa siku au week! kwa hiyo juhadhari sana nswelaga!

Pamoja kaka! Uwa tunajinyonga kwenye kutetea harakati za maendeleo syo ktk kila jambo! na hii ndiyo sababu mpk nimeamua kuomba ushauri kwa wadau wengine kama hv!
 
Nawachukia sana wanawake wanao geuza mtaji mwanaume.
 
be careful mkuu, wanawake wana attributes nyingi sana na si rahisi kuwaelewa na kuwacontrol and that is why mahusiano na ndoa nyingi zinakufa hata kama watu wamekuwa pamoja kwa miaka mingi.

Kwa tabia hii ya kubambikizia watoto, wanawake nawafananisha na jini.
 
Nawachukia sana wanawake wanao geuza mtaji mwanaume.

wanawake ni mashetani yani hii ni kweli kabisa, kama we ni mwanaume na unabisha, Subiri utakuja thibitisha na wewe kama mi ninavyothibitisha.
 
Back
Top Bottom