Turkey, Tanzania sign deals of visa exemption & other trade ties

Kwa mnaoijua Uturuki, ni fursa gani za kibiashara zinapatikana huko?

mkuu mimi nilipata bahati ya kutembelea Uturuki na kufanya mikutano kadhaa ya kibishara kwenye maaneo yangu of interest.
Kwa kusema za ukweli ukiachana na watu wengi hapa wanongea mambo ya sio ya msingi na kuendeleza malalamiko kwenye thread hii,sisi tuna-nafasi kubwa ya ku-benefit na ushirikiano huu ila yatupasa kujituma na kuwa na nia za ukweli ilikufikia malengo.
Kuna wafanya biashara wengi sana wakubwa na wadogo wa kitanzania wanao jazana huko Uchina na nchi nyingi za Asia kufata bidhaanyingi zilizo chini ya kiwango,lakini kama wafanya biashara hao watahamishia mitaji yao kwa nchi kama hii ya Uturuki bila ya shaka ule msamiati ya ZA-KICHINA utafutika kabisa.kwani hao jamaa wanatengeneza bidhaa zilizo na ubora wa hali ya juu sana hasa bidhaa za viwandani kwenye nyanja zote.
Pili,haswa swala hili la kilimo ndio kabisa tunaweza kufaidika sana,kwani,kutokana na kilimo cha muda mrefu huko Uturuki toka enzi zakale ardhi yao imekosa au imeisha rutuba hivyo kufanya kilimo kuwa kigumu na kuwafanya wategemee sana ku-IMPORT mazao ya kilimo kwa kiasi kikubwa.Na hapa nadhani ndio sisi kama Watanzania ndio tunaweza kufaidika kwa kiasi kikubwa kwa kijiongezea pato kwa kupeleka huko mazao yeu.Tukifata na kuutekeleza mpango wa kilimo kwanza ni lazima tutafaidika tu na nchi hii.mimi binafsi nilipata order nyingi za mazao ya kutengeneza mafuta ingwa bado sijaingia kwenye nyanja hiyo.
Ni mambo mengi sana tunaweza kufaidika kutokea nchi hiyo,katika nyanja viwanda,biashara hasa ya vipuri vya magari,maeneo ya madini wao wanalo soko kubwa sana la madini pale Istanbul linakaribia lile la Ujerumani,mambo ya telecommication na tower building ili mladi kila sehemu za kiuchumi
 
Turkey ni nchi iliyoendelea tangu lini?

Economically Turkey is pretty well developed. if you listened to the western media you would think Turkey was all about religious turmoil. Of course this does not mean Tanzania will benefit from better relations with Turkey but it is a start.

[ame]http://en.wikipedia.org/wiki/Economy_of_Turkey[/ame]

 
Hawa Waturkey watatusaidia nini jamani?wao wako desperate kuingia EU,je kitu gani tutatrade na Turkey?Niambieni jamani!
Sana sana Waturuki watakuwa happy kusikia mtu waliomfundisha udaktari kwao Dr Husssein Mwinyi ni kiongozi wa taifa!
watatusaidia kwa mambo mengi sana,kwakuwa wametuzidi sana kiuchumi na kimaendeleo kwahiyo mi nafikiri JK amepiga hatua nzuri.
 
Turkey product zao nyingi ni nzuri sana.(mi napenda sana suti zao.) Kwani wakenya wanaokuja kuwekeza nchini wameendelea? au hamjui kenya ni nchi ya pili ajwa uwekezaji tanzania ikiongozwa na uk?
 
Mhh haya tutasikia mengi tu maana inasifika kwa madawa ya kulevya iyo nchi!
 
Mhh haya tutasikia mengi tu maana inasifika kwa madawa ya kulevya iyo nchi!

Ha! watu wengine bana? si lazima u-comment kama hujui madawa ni huko argentina na merakani ndugu?
 
Turkey product zao nyingi ni nzuri sana.(mi napenda sana suti zao.) Kwani wakenya wanaokuja kuwekeza nchini wameendelea? au hamjui kenya ni nchi ya pili ajwa uwekezaji tanzania ikiongozwa na uk?

Mkuu Abizani Turkey product zao nyingi nzuri sana.Je Unazijuwa lakini Mkuu Nyani abizani?Au na wewe unajisemea tu? Turkey product zao karibu zinafanana na za kichina WaTurkey ninavyojuwa mimi wao hupenda kuiga vitu kutoka ulaya wewe uwaletee Mfano tu kitu kimoja basi wao Waturuki ni hodari kwa kufyatua Vitu Feki sema wao kidogo afadhali kuliko huyo mchina kazidi kufyatua na Mali zake huyo Mchina sio imara kwa fikira zangu mimi Mzee Rais J Kikwete alichofanya kuweka mikataba ya Ushirikiano na hao Waturuki waje kuiba Madini na walete Utamaduni wao wa kituruki kuna nchi Mkuu Rais anafaa kwenda huko ulaya zenye Maendeleo kuliko hiyo Turkey. nijuavyo mimi Turkey ni nchi inayotumiwa na Marekani kwa Maslahi yake Amerika katika hapo Mashariki ya kati kwa mfano Marekani ikitaka kuishambulia IRAQ inaitumia Uturuki kama Base Kituo chake kuipiga IRAQ AU Syria Au IRAN au nchi yoyote iliyopo hapo Mashariki ya kati iliyokuwa Aduwi wa Amerika na Mjomba wake ISRAIL. Turkey kiuchumi inategemea sana Viwanda,na Mikopo kutoka katika Benki kuu ya Dunia Uturuki ni nchi pia Masikini Duniani lakini Umasikini wake tofauti na wa kwetu hapo Tanzania. Turkey ni nchi masikini lakini iliyoendelea kwa kila kitu haina Matatizo ya njaa,Umeme,Maji Safi, wananchi wake wanaishi ndani ya nyumba hakuna mtu anae lala nje kwa kukosa nyumba au kukosa kula au matatizo ya Mgao wa Umeme au Maji hakuna kitu kama hicho Uturuki nzima , Turkey inapata Misaada yake mikubwa kutoka kwa Mfadhili wake Amerika kwa ajili ya Maslahi ya Amerika. Turkey ina jeshi kubwa katika jeshi la Nato baada ya Amerika inafuatia Uturuki kwa jeshi lake kubwa hivyo ndivyo ninavyoelewa mimi Nchi ya Uturuki. Waturuki Waje hapo nyumbani kuiba Madini na kuleta Bidhaa zao za Kufyatuwa ingawa ni bora kuliko Bidhaa za Kichina asanteni Ndugu zangu wana JF.
 
Ha! watu wengine bana? si lazima u-comment kama hujui madawa ni huko argentina na merakani ndugu?
Usinibishie ndugu wapo watu kibao wanafanya iyo biashara nasema ninachokijua sawa!!
 
Hawa Waturkey watatusaidia nini jamani?wao wako desperate kuingia EU,je kitu gani tutatrade na Turkey?Niambieni jamani!
Sana sana Waturuki watakuwa happy kusikia mtu waliomfundisha udaktari kwao Dr Husssein Mwinyi ni kiongozi wa taifa!

Ni Kweli unavyosema Waturuki Watasikia Raha sana ikiwa siku moja Wakisikia kuwa Mwanafunzi wao wa Udaktari ndugu Dr Husssein Mwinyi ni kiongozi wa taifa nakubaliana na wewe kwa sababu kisomo alichosoma Ndugu Dr Husssein Mwinyi haikufaa Mheshimiwa Rais J.Kikwete Kuumpa Huyo Dr Husssein Mwinyi kumpa cheo cha kuwa Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa, bora Mzee J Kikwete angempa huyo Dr Husssein Mwinyi cheo cha Naibu Waziri wa afya ingekuwa kafanya jambo la maana lakini kumpa huyo Dr Husssein Mwinyi cheo cha U Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa ni sawa sawa na Bunduki kumpa nyani kisha umwambie huyo Nyani alenge shabaha ataweza kweli kulenga Shabaha huo nyani? Kwa Sababu Mtu aliyekuwa amesomea Udaktari Umpe bunduki aitumie je Daktari ataweza kuitumia hiyo bunduki kweli? inaonyesha hapo Mzee J Kikwete alifanya makosa kumpa cheo cha Uwaziri wa Ulinzi Ndugu yetu Dr Husssein Mwinyi. Kwa mawazo yangu mimi ninafikiri Mheshimiwa Mkuu Rais J Kikwete anamuandaa Dr Husssein Mwinyi kuwa Rais kule Zanzibar kwa kupitia Chama Cha CCM kwa mawazo yangu mimi hayo jamani Mnaonaje hayo mawazo yangu Wana JF? wenzangu.

http://www.afdevinfo.com/htmlreports/peo/peo_464.html
 
waturuki wasio na maendeleo wanafanya mambo haya...naam mtu kauliza tngu lini wameendelea.

CENTER]ANKARA- Esenboğa Int. Airport[/CENTER]

Cap: 10 million pass/year
Completed in: October 2006









thanks to Dinuś








-----




TURKISH AIRLINES






 
Usinibishie ndugu wapo watu kibao wanafanya iyo biashara nasema ninachokijua sawa!!

Uturuki wauza madawa ya kulevya wapo lkn si kama unavyofikiria wewe, Mbona ata Tanzania wapo wengi tu. Kipindi cha nyuma kuna baadhi ya wanafunzi wa kitanzania walijiingiza kwenye madawa ya kulevya lkn baada ya kukamatwa kamatwa mambo hayo yakapungua kwa kiasi kikubwa. Wazee wa kete wapo (wanaitwa beach boys) pale istanbul lakini kiwango kimepungua maana wanakamatwa kamatwa sana. Kweli Turkey ni bridge ya madawa ya kulevya. Huwa yanatoka Afghanistan,iran then turkey kwa ajili ya kuja EUROPE. Lakini Sidhani kama issue ya madawa inanafasi ktk huu mkataba.
Mbona sisi tumekaa for ages na hatujauza lol...si kila mtu yuko after madawa

Kuna mambo mazuri mengii..
 
Mhh haya tutasikia mengi tu maana inasifika kwa madawa ya kulevya iyo nchi!

Wasiwasi wako tu dada!! Kete zipo kila mahali especially afghanstan and spain maana wanabeba kwenye ma container lol...


Regards
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…