Turudi kwenye mstari juu ya hali tete ya Mzee Philip Mangula

Turudi kwenye mstari juu ya hali tete ya Mzee Philip Mangula

GARETHBALE

Member
Joined
Dec 22, 2013
Posts
76
Reaction score
333
TUHARAKISHE KUWACHANGIA CHADEMA ILI TURUDI KWENYE SUALA LA SUMU NDANI YA MWILI WA MZEE MANGULA.

Taarifa ya Kamanda Mambosasa bado inakera kwenye vichwa vya wengi! Tunataka taarifa ya Madaktari wa Muhimbili.

Tunataka wale wote waliokuwa na Mzee Mangula wakati anatoka jasho na kudondoka waandike maelezo kwa sababu hao kwa vyovyote vile ndiyo watuhumiwa namba moja.

Haiingii akilini eti watu hao waachwe huru halafu Polisi waanze kutafuta watuhumiwa nje ya jengo la CCM Lumumba. Waliopo nje ya Jengo la Lumumba ni Wapinzani.

Kama alianguka mara baada ya kikao na ikabainika kuwa alilishwa sumu, kwa akili ya kawaida, Wabaya wa Mzee Mangula walikuwa ndani ya jengo la Lumumba.

Polisi mnashindwa nini kuwahoji wajumbe wote wa Kamati Kuu ili mhusika ajulikane? Aidha watu tunataka kujua hali ya mgonjwa na aina ya sumu aliyopewa.

Na taarifa hiyo itolewe na Madaktari bingwa wanaomtibu! Tumepata habari kuwa Ikulu imekataza watu wasiende kumjulia hali kule alikolazwa. Kwanini? Ikulu inaogopa nini watu wakienda kumwangalia?

Hakika mwaka huu una mengi ya kuchekesha na mengi ya aibu. Tuombe afya, tuone mengi!
 
Hapo naona kuna kitu serikali inataka kuficha.

Ni vizuri madakitari wanaomtibu ndo watoe taarifa maana wanafahamu mambo ya kimatibabu na si polisi wanaofahamu mambo ya bunduki na mabomu ya machozi.

Wakiendelea kuficha ni sumu gani, na kuzuia watu wasiende kumuona, basi watu watasema ana conrona
 
Hii ya ikulu kuzuia asijuliwe khali imekaaje hii wakuu? Maana afadhali ingekuwa ni familia au yeye mwenyewe binafsi amtoa zuio hilo. Au hata polisi kama uchunguzi bado unaendelea. Lakini ikulu? Mhn!
 
Wazee kama awa wadanje tu ni mzigo kwa taifa kwa uongo unafiki na kujipendekeza kwa watawala ambao hawana msaada kwake akipata tatizo. danja tu.
Kwa hiyo mkuu unataka kuwaambia nini bendi ya T.O.T?
 
TUHARAKISHE KUWACHANGIA CHADEMA ILI TURUDI KWENYE SWALA LA SUMU NDANI YA MWILI WA MZEE MANGULA.
Taarifa ya Kamanda Mambosasa bado inakera kwenye vichwa vya wengi! Tunataka taarifa ya Madaktari wa Muhimbili. Tunataka wale wote waliokuwa na Mzee Mangula wakati anatoka jasho na kudondoka waandike maelezo kwa sababu hao kwa vyovyote vile ndiyo watuhumiwa namba moja. Haiingii akilini eti watu hao waachwe huru halafu Polisi waanze kutafuta watuhumiwa nje ya jengo la CCM Lumumba. Waliopo nje ya Jengo la Lumumba ni Wapinzani. Kama alianguka mara baada ya kikao na ikabainika kuwa alilishwa sumu, kwa akili ya kawaida, Wabaya wa Mzee Mangula walikuwa ndani ya jengo la Lumumba. Polisi mnashindwa nini kuwahoji wajumbe wote wa Kamati Kuu ili mhusika ajulikane? Aidha watu tunataka kujua hali ya mgonjwa na aina ya sumu aliyopewa. Na taarifa hiyo itolewe na Madaktari bingwa wanaomtibu! Tumepata habari kuwa Ikulu imekataza watu wasiende kumjulia hali kule alikolazwa. Kwa nini? Ikulu inaogopa nini watu wakienda kumwangalia? Hakika mwaka huu una mengi ya kuchekesha na mengi ya aibu. Tuombe afya, tuone mengi!
Hata mambokale anatakiwa kuhojiwa na vyombo vya usalama
 
Back
Top Bottom