georgeallen
JF-Expert Member
- Jun 3, 2011
- 4,118
- 1,875
Wandugu, ili kujikomboa na halii hii ngumu ya maisha iliyotunyemelea hapa nchini miaka hii, mwenzenu nimejipigapiga na kufanikiwa kujenga mjengo kwa ajili ya biashara ya nyumba ya kulala wageni, bar, na mgahawa. Majengo ya biashara hii yapo kando kando ya moja ya barabara kuu za Tanzania na muda si mrefu itaanza kazi. Tatizo langu kubwa kwa sasa ni jina gani litabamba kwa hii biashara na ukweli ni kuwa kila jina ninalolifikiria naliona kama siyo au tayari linatumika sehemu fulani huko duniani. Majina kama Dynasty club, Ecape six, Elewana, oriental resort, Highway comfort, Hillside hideaway, Palmview motel, Hillsview inn, Darway motel, africana, Bell air, Mel rose Place au hata "Mara lago club" la yule babu anayewania urais USA yote yameishachukuliwa au siyo mageni tena kwenye masikio ya watu. Ni kwa sababu hizo na nyingine za kibiashara au kisheria basi nakuja kwenu kuomba msaada wenu kubuni jina la biashara yangu hii.